Najua nimepig nyuki ndimu lakini kua na ustahmilivu mkuu! Kumbuka Watanganyika sio sawa na Wanzanzibari, huko ikifika Uchaguzi ukiwa na vijipesa unaweza kuwahadaa watu kwa;
pombe, kanga, pilau, ubwabwa, 'Sadaka', takrima, 'kifuta machofu' na kulichukua jimbo kiurahisi na ama kuwapata wananchi wengi wa kukuwekea kura lakini tofauti kwa Wazanzibari, Wazanzibari kwao siasa ni Ukombozi na hawakubali kununuliwa kiurahisi kwa vitu vya kimaajabu majabu, kwao wao siasa imo ndani ya damu yao! Kitu chengine umesema yule mama alivuliwa mtandio na sio hijabu! Hoja sio hijabu mtandio au kilemba bali ni jinsi walivyomkashifu yule mwanamama!