Mlengo wa Kati
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 2,730
- 492
Wao ni kazi tu...propaganda tupa kule. Umoja wao,uongozi wao na ubunifu wao ndiyo unaokusanya mafanikio ya CHADEMA yanayoendelea kuonekana. Ni kama Messi na Xavi. Hapana chezeya!
Mbowe na Dr. Slaa ni miiba mikali kwa chama tawala. Ndiyo maana kila aina ya hila,propaganda na uongo unaendelea kusemwa kuwasambaratisha. Na ubunifu na utayari wao wa kuwa sehemu ya UKAWA ni kitisho kwelikweli.
CHADEMA sasa imepiga hodi na kuitikiwa vijijini. Kilichobaki ni kujitangaza zaidi na kuelekeza nguvu mwakani. Kila chama cha upinzani duniani kilipitia njia ya CHADEMA kuelekea Ikulu na kuwa chama tawala.
CCM yaweza kuwa imeshinda kwa mahesabu ya jumla. Kuendelea kuporomoka kwa takwimu zao ni kitisho kisichoweza kupuuzwa nao.
Binafsi niliukubali uongozi wa Mbowe na Dr. Slaa siku CHADEMA walipoweka wagombea mitaa na vitongoji vya mkoa wa Pwani. Big up Mbowe na Dr. Slaa. Ishikeni UKAWA maana ni nguvu yenu.
Tatizo Mbowe na Slaa hawana nyota