Mbowe na Dr. Slaa,the greatest combination!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,249
25,784
Wao ni kazi tu...propaganda tupa kule. Umoja wao,uongozi wao na ubunifu wao ndiyo unaokusanya mafanikio ya CHADEMA yanayoendelea kuonekana. Ni kama Messi na Xavi. Hapana chezeya!

Mbowe na Dr. Slaa ni miiba mikali kwa chama tawala. Ndiyo maana kila aina ya hila,propaganda na uongo unaendelea kusemwa kuwasambaratisha. Na ubunifu na utayari wao wa kuwa sehemu ya UKAWA ni kitisho kwelikweli.

CHADEMA sasa imepiga hodi na kuitikiwa vijijini. Kilichobaki ni kujitangaza zaidi na kuelekeza nguvu mwakani. Kila chama cha upinzani duniani kilipitia njia ya CHADEMA kuelekea Ikulu na kuwa chama tawala.

CCM yaweza kuwa imeshinda kwa mahesabu ya jumla. Kuendelea kuporomoka kwa takwimu zao ni kitisho kisichoweza kupuuzwa nao.

Binafsi niliukubali uongozi wa Mbowe na Dr. Slaa siku CHADEMA walipoweka wagombea mitaa na vitongoji vya mkoa wa Pwani. Big up Mbowe na Dr. Slaa. Ishikeni UKAWA maana ni nguvu yenu.
 
Mh. Dr. P w slaa na mh. Elikaeli freeman mbowe mkirudi nyuma mtatutambua sisi tumejitoa kuwa nyuma yenu kulikomboa taifa hili na tunawategemea sana tunawaamini sana tunawaombea sana .. mungu awaondolee jini la usaliti na tamaa ya pesa . Hata sisi tunahongwa tuisaliti cdm tumegoma tunatishiwa maisha tumekubali ..maana kufa ni siku moja na kuzaliwa ni siku moja na hata atakae tuuwa nae atakaufa ...mungu awabariki sasa naenda kupumzika baada ya kukesha kulinda kura ya mwenyekiti wangu jana...nimeshehwrekea vya kutosha leo....
 
Wao ni kazi tu...propaganda tupa kule. Umoja wao,uongozi wao na ubunifu wao ndiyo unaokusanya mafanikio ya CHADEMA yanayoendelea kuonekana. Ni kama Messi na Xavi. Hapana chezeya!

Mbowe na Dr. Slaa ni miiba mikali kwa chama tawala. Ndiyo maana kila aina ya hila,propaganda na uongo unaendelea kusemwa kuwasambaratisha. Na ubunifu na utayari wao wa kuwa sehemu ya UKAWA ni kitisho kwelikweli.

CHADEMA sasa imepiga hodi na kuitikiwa vijijini. Kilichobaki ni kujitangaza zaidi na kuelekeza nguvu mwakani. Kila chama cha upinzani duniani kilipitia njia ya CHADEMA kuelekea Ikulu na kuwa chama tawala.

CCM yaweza kuwa imeshinda kwa mahesabu ya jumla. Kuendelea kuporomoka kwa takwimu zao ni kitisho kisichoweza kupuuzwa nao.

Binafsi niliukubali uongozi wa Mbowe na Dr. Slaa siku CHADEMA walipoweka wagombea mitaa na vitongoji vya mkoa wa Pwani. Big up Mbowe na Dr. Slaa. Ishikeni UKAWA maana ni nguvu yenu.

Mkuu hapo umesema, na hasa kwa mtu mwenye uchungu na nchi hii pamoja na watu wake anaonekana kwa matendo yake. Huyu Mhs Mbowe anealewa maana ya CHADEMA (imetoka wapi, inakwenda wapi na itafika wapi) Hivyo hivyo Dr wa watu anajua anachokifanya kwa sababu anaipenda nchi hii pamoja na watu wake. Anatenda ya kweli na ndiyo maana hana mchezo kwani fukuza fukuza yake ianzidi kuleta matundu endelevu.
 
The best combination ever na ni bad news kwa watu wote wanaotaka Chadema itetereke, hamna cha zitto wala nyepesi kudadadeki chama ni institution kubwa haiwezi kuyumbishwa na mtu mmoja. Waliotabiri Chadema itakufa before 2015 Mungu amewaprove wrong. Chama kinaendelea kuwa concrete each and every-day.
 
Ni viongozi ambao Historia itawaenzi na mchango wao kati ya wengi umeonekana.
Long and safe live.
 
Mh. Dr. P w slaa na mh. Elikaeli freeman mbowe mkirudi nyuma mtatutambua sisi tumejitoa kuwa nyuma yenu kulikomboa taifa hili na tunawategemea sana tunawaamini sana tunawaombea sana .. mungu awaondolee jini la usaliti na tamaa ya pesa . Hata sisi tunahongwa tuisaliti cdm tumegoma tunatishiwa maisha tumekubali ..maana kufa ni siku moja na kuzaliwa ni siku moja na hata atakae tuuwa nae atakaufa ...mungu awabariki sasa naenda kupumzika baada ya kukesha kulinda kura ya mwenyekiti wangu jana...nimeshehwrekea vya kutosha leo....
Amen kamanda...
 
Hivi Mbatia, Prof Lipumba kumbe hawana lolote UKAWA ni drama tu.
 
Back
Top Bottom