Mbowe kukamatwa kwa ufisadi

Mbowe kukamatwa kwa ufisadi

Kwa sababu katajwa MBOWE angekuwa CHENGE ungeshangilia, mkuki kwa nguluwe kwa binadamu mchungu.
JPM PIGA KOTEKOTE MAJIPU YATUMBUKE.UKITAKA KUMUUA NYANI USIMWANGALIE USONI.


Mkuu hebu soma attachment aloweka jamaa utaona kwa nini ninapinga huu upuuzi wa hii post, unless kama ni sawa kuchafua mtu kisa ni wa upinzani ama chama tawala. Nilisahau kumbe tunachafuana sababu ni tofauti ya vyama.
 
Iwe marudio au la
nshu kwanini!?
Tunataka ukweli uwekwe wazi huyu naye atumbuliwe


Mkuu ID na hilo signature yako haviendani na unachopost, fedha kibenki hazihamishwi kiivyo anavyosema mtoa mada, halafu ukiangalia hizo fedha zinatoka Dubai to Hong Kong, sasa ubadhirifu upo wapi hapo? tuwe tunaleta uongo unaoendana na ukweli.
 
Hili Ni gazeti jipya?hembu tusomee na hiyo habari ya mkwe WA raisi awa dalali na ufisadi WA polisi
 
Katorosha toka Tanzania kwenda Dubai ,Uswis na Jessey bila kibali cha BOT.

Nikinyume cha sheria ya fedha.


Hahahahahahhhaahhahahahah Kaka hujasoma vizuri hiyo thread, BOT inahusika vipi ilhali hiyo document fake inaonyesha ni standing order inayoelekeza hela zitoke NOOR BANK ya Dubai kwenda bank tofauti tatu huko Hong Kong,.Aliyelalamika ni Dubai ama Tanzania ama Hong Kong?
 
Hahahahahahhhaahhahahahah Kaka hujasoma vizuri hiyo thread, BOT inahusika vipi ilhali hiyo document fake inaonyesha ni standing order inayoelekeza hela zitoke NOOR BANK ya Dubai kwenda bank tofauti tatu huko Hong Kong,.Aliyelalamika ni Dubai ama Tanzania ama Hong Kong?

Kwa hiyo NOOR BANK hizo pesa zinefikaje?. Au zimejiingiza zenyewe?
 
Magazeti ya kufungia vitumbua haya. Hayapaswi kusomwa na wenye akili timamu.
 
Ningefurashi sana kama polisi wangetuambia vile vile zile za ESCROW ( za Chenge,Tibaijuka na Stanbic) uchunguzi umefikia wapi
 
Tulishasema kitambo kuwa ni vema huyu fisadi akamatwe kwa utoroshaji wa pesa hizi na ufisadi wao anaofanya na Lowasa.
 
Billion mbili kumbe. duh mbona mtaani kwangu bush watu wanamiliki kihalali kama Mbowe?
 
Mleta mada leta na majina ya wale ambao zitto amegoma kuwataja mpaka leo ili tukuamini..!!
 
Mtoa mada kabla hujaleta post humu jaribu kufuatilia angalao kidogo kama kuna kinachoendana na unachotaka kuleta. Hii issue ni marudio tuu unaleta hapa, hii imeletwa humu kipindi cha kampeni halafu nawe ukaibeba kama ilivyo bila kujiuliza, Je international cash transfer ndo hivyo huwa zinafanyika kulingana na hicho kipeperushi ulichoweka!?

Ifike wakati tulete mada ambazo siye wenyewe waletaji tumejilidhisha!!

Hiyo document ni nini haswa? Inamuamlisha nani kufanya nini? Document moja inaenda bank zaidi ya moja? Unajua kweli usiri ulioopo kwenye account ya mteja na bank?

Kama ni kajipu atumbuliwe tu, anajifnya kutoa pongezi...ooh mh rais kaanza vizuri, ooh anafanya yale wapinzani tulikuwa tunapigia kelele....! kumbe ana kajipu..! kama kajipu acha tu katumbuliwe.
 
Kwa hiyo NOOR BANK hizo pesa zinefikaje?. Au zimejiingiza zenyewe?


Mkuu me nadhani ungepiga kimya tuu mambo yapite, acha kubisha na kitu usichojua, sema hilo ni gazeti umecopy na kupaste basi hapo utaeleweka zaidi. Maelezo yako hayaendani na swali lako.
 
Back
Top Bottom