baraza la mawaziri ni kubwa sana na Mheshimiwa rais alitudanganya kuwa atakuwa na baraza dogo tena makini lakini sasa nashindwa kumwelewa huyu rais ambaye anatudanganya kila wakati.Lakini kwa mtazamo wangu naona rais wetu ataendelea kutudanganya maana anaelewa wenye upeo wa kufikiri kuwa rais anadanganya ni wachache mno maana elimu hamna ndiyo maana alitumia khanga na 5000 huko vijinini na kupata kura na kwa maana nyingine ana mamlaka kikatibu hamna wa kumbadilisha maana katiba inamruhusu hata angechagua 100 tutapiga kelele na mwishoni tutakuwa kimya.KWA HIYO KINACHOTAKIWA HAPA NI KATIBA IBADILISHWE IENDANE NA WAKATI IKIWA KIKUBWA NI KUMPUNGUZIA RAIS MADARAKA YA KUTEUA VIONGOZI NA IWEKWE KWA MASLAHI YA VYAMA VYOTE