Mbowe: Jk aungwe mkono na kila chama

Mbowe: Jk aungwe mkono na kila chama

Kama maneno halisi ya Mh. Freeman Mbowe yalikuwa "kumuunga mkono kwa ajili ya maslahi ya Taifa na si vyama" na SI VINGENEVYO, Cha ajabu ni nini hapo?
Au kwa sababu ni Upinzani kupinga hata mambo yenye tija?

acha ulimbi ww,toka lini mchaga akawa na maslahi na taifa,hyo sahau
 
Huo ni mtego kwa KIKWETE coz hawezi kutekeleza anachokisema ili baadae akosolewe ipasavyo

Pia CCM wanataka wapitishe katiba inayojali maslah ya chama chao hivyo basi KIKWETE anapoigiza kusema maneno ya busara wakati hatekelezi lazima aungwe mkono ili baadae maneno yake mwenyewe yamuhukumu mbele ya watu wazalendo na Taifa hili la Tanzania

KIKWETE NDUMILA KUWILI ANANG'ATA NA KUPULIZA TUSUBIRI TUTAONA UONGO WA MANENO YAKE HAYA.
 
Kumbe kuna watu humu mabogus!Hivi JK akisema jambo jema asiungwe mkono kwasababu tu ni wa chama tawala? mbowe anapokuwa jukwaani anazungumza mambo ya kitaifa ambayo hata JK akiwa chamani anayapinga akitoka nje ya box anayakubali.kama mnafikiri siasa ni utani,matusi mkafanyie kwenye familia zenu.Najua viposho ndo vinawasumbua huku.Historia iwahukumu baadae.
 
Hi sred tayari ishavamiwa na mi trojans ya lumumba
 
Mbowe anawasema akina Juma Nkamia "Siongei na Mbwa bali naongea na Mwenye Mbwa" na Livingstone Lusinde "Kibajaji" mabingwa wa kuongea na kushabikia jambo bila kutafakari. Walitmia ubabe kupitishaule Muswada wa marekebisho ya Rasimu ya Katiba hadi Wapinzani kuungana na kufanya mkutano wa kihistoria pale Jangwani. Wassira na Mkuchika walitamka hadharani kuwa wapinzani wasitegemee tena kuitwa Ikulu na wala Muswada hautarejeshwa Bungeni kurekebisha kasoro na Lissu kutukanwa na Werema kuwa hana akili. Wapinzani walitwa Ikulu na Muswada ulirejeshwa Bungeni na kufanyiwa marekebiso stahiki. Simiyu na wenzako wote acheni ushabiki usiyo na tija kwa Taifa
 
kama ni katika swala la kuhakikisha maoni ya wananchi yanazingatiwa basi sawa .
 
mimi nimpinzani lakini nampongeza sana mheshimiwa Rais kwa msimamo thabiti hasa kuhusu mambo ya masilahi kwa Taifa. kumbuka amerudisha sheria mara mbili ili zifanyiwe mabadiliko pia amewela kifua katiba mpya ipatikane ingawaje CCM wenzake mpaka leo wanalalamika kuwa haikuwemo kwenye sera ya CCM.Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
 
Mbowe ni mnafiki akiwa kwenye majukwaa anazungumza uchochezi lakini akikutana na viongozi wenzake anajifanya mwema hafai kanisani wala msikitini.

Kama ulimsikiliza mh. Rais kwa makini, usingeleta ushabiki huu. Rais amewasema wote wanaofikiri maamuzi ya vyama vyao ndiyo iwe sura ya KATIBA mpya wanakosea sana. Ametaadharisha kuwa vipo vipengele vingi vyenye utata na siyo swala la serikali mbili ama tatu tu. Sasa kati ya Mbowe aliyetaka mawazo ya wananchi yaheshimiwe na yule aliyesema wanaotaka serikali tatu ni wahuni na wana uchu wa madaraka, nani MNAFIKI?

 
Last edited by a moderator:
"Ccm ijiandae kisaikolojia kuwa chama pinzani na uwepo wa serikali tatu" Hotuba ya JK.
 
Sisi tunataka muundo wa serikali mbili, na huo ndio msimamo wa CCM, "Raisi J M Kikwete 2/2/2014: Mbeya"

Kikwete ni Rais wa kwanza Tanzania kuwa na kauli mbili mbili kwa maswala nyeti ya nchi au mpenda kuridhisha pande zote zinazosigana. Kumbuka ndani ya ccm ameshindwa kuyakemea na kuyavunja makundi kwa tabia yake ya kutaka apendwe na kila kundi!
Ndivyo hivyo hivyo anafanya kwenye hili swala la katiba mpya. Akiwa ccm anasema kuwa sera yao ni serikali mbili na ndiyo inabidi ilazimishwe, lkn jana akiwa na vyama vya upinzani anazungumzia utaifa kwanza! Ni undumila kuwili huu ie double standards. Mh Mbowe hapa naona amedanganyika, Kikwete has taken them for a ride!!
 
mkuu soma habari vizuri, mbowe ameunga mkono kauli ya muheshimiwa ya kuvitaka vyama vya siasa kutoingiza agenda za kichama kwenye katiba, hili nalo ni la kushangaza? kwani kaunga mkono hutuba nzima?

nakubaliana na unachokisema, boss. lakini ukiangalia kwa jicho la tatu kamanda Mbowe hakupaswa kupepesa macho wala kumung'unya maneno juu ya kauli ya JK kule Mbeya wakati akielezea msimamo wa chama chake (CCM) kuhusu suala la muungano. hapo tayari JK ameji-compromise na anakosa moral authority na credibility.....ushauri wowote anaoutoa kwa vyama vingine unakosa mashiko.

JK must not only walk but also must be seen to walk the talk of "vyama vya siasa kutoingiza agenda za kichama kwenye katiba" kabla Mbowe & co hawajaanza kumkubali kama kiranja wa mchakato.

......also mindful of the fact that kuandikwa katiba mpya si ajenda iliyoasisiwa na CCM!!
 
Back
Top Bottom