Mbowe bana!No wonder wenzio katika WARAKA WAO WA USHINDI walikuita wewe ni Kiongozi usiye na maono (vision).Hivi utawezaje kulinda kura nchi nzima kama Viongozi Chadema hamtaki kukiimarisha Chama katika ngazi za chini kabisa huko Mikoani?Fedha mnapewa na Wafadhili,WanaChadema wanachangia Chama katika Mikutano na Serikali inatoa fedha za ruzuku zaidi ya shilingi 300,000,000 kila mwezi sasa mnashindwaje kuimarisha shughuli za Kichama katika ngazi hizo?Leo unazungumzia kuhusu kulinda kura huku Chama kikiwa hakina mtaji wa muundo wa uongozi katika ngazi za chini.Kuwepo kwa Viongozi wa matawi na mashina mikoani kurahisisha Chadema kuratibu mipango mbalimbali ya kujenga ya Chama kama vile kuwatambua mawakala waaminifu watakaoweza kukisaidia Chama kulinda kura zake nyakati za Uchaguzi kwakuwa Viongozi wa haya Matawi watakuwa wanawafahamu hawa Mawakala vizuri zaidi.Shughuli nyingine za kujenga Chama zinaweza kufanywa na hawa Viongozi wa Mikoani hivyo kuwawezesha Viongozi wa Kitaifa ku-focus katika masuala ya Kitaifa.