[Ushahidi hutolewa sehemu husika na kama munavyofikiria. Mbona tume huru ya kimahakama haijaundwa kuchunguza, ingefanyika hivyo na ushahidi ungetolewa mahakamni. Mbowe ni njembe na mtu makini sana.QUOTE=Ghosryder;10096847]Kama ilivyo ada na kawaida ya Mh Mbowe kutoa matamko ya kiulaghai na uongo kwa kudai kwamba huwa ana ushahidi wa mambo mbalimbali yanayotokea ktk mustakbali wa siasa za nchi yetu, kama alivyowahi kudai siku zilizopita, ambapo alidai ana video ya ushahidi wa Bomu la Olasiti Arusha, na pia Maswala ya Mwangosi na yale matukio ya waandishi kumwagiwa tindikali, ushahidi ambao hajawahi kuutoa kwenye vyombo vya sheria, leo kaja na mpya baada ya kudai ana ushahidi kutoka vikao vya ndani vya ccm kwamba eti hawataki kutekeleza mchakato wa katiba mpya bali wanawalaghai tu ili waingie ndani ya bunge la katiba na kisha waamue kufanya watakavyo. My take, kwa kuwa huyu mh Mbowe amekuwa ni mtu wa kudai kuwa ana ushahidi wa mambo mengi tena yeye tu, itabidi vyombo vya dola vimbane ili aisadie polisi katika mengi ambayo yanahusisha jinai ili haki ipatikane kwa wahanga.