Mbowe asita kususia posho

NINANUKUU...... "Soda na chai kwa wageni wa KUB ni Tshs. 2,000,000.00 kwa mwezi na kwa mwaka Tshs. 24,000,000.00!! Wakati kima cha chini ni Tshs. 120,000.00 kwa mwezi na mwaka ni Tshs. 1,440,000" MWISHO WA KUNUKUU



Kambi ya upinzani ikipokea idadi ya wageni 30,000 kwa mwaka = 24,000,000/30,000=800 kwa kila mgeni
 
Uellewa mdogo kwa magamba,kupunguza posho zisizokuwa na tija.zile za msingi ni muhimu kufanikisha maendeleo au ufanisi.mlitaka atumiemshahara wake kuendesha shughuli za ofisi kama kiongozi wa kambi ya upinzani?

Hivi hapa kuna magamba na wasiokuwa na magamba ama tunaongelea suala la kitaifa. Kupunguza matumizi serikalini ni muhimu sana. Hivi soda na chai vya Tshs. 2,000,000.00 kwa mwezi si matumizi makubwa hayo? Angesema pia nazo zipunguzwe na tuambiwe na mawaziri wanapata kiasi gani ili nazo zipunguzwe. Huenda mawaziri wanapata zaidi ya hizi. Hivi inaingia akilini kweli kwamba mtu anatumia Tshs. 2,000,000.00 pesa za walipa kodi kwa mwezi kuwanunulia wageni wake soda na chai katika nchi hii masikini wakati mwingine anapata Tshs. 120,000.00 kwa mwezi?
 
unatumia akili gani mtu mjinga wewe kwani hayo mahesabu umepiga na makalio au., ...? bunge linakuwaga miezi yote au hujui unaloongea . ndezi.....
 

Mimi siyo mjuzi wa mambo yanavyofanyika bungeni, hivi wabunge wa upinzani au CHADENA wakikutana kuna gharama zozote kama maji ya kunywa? kama zipo zinalipiwa na fungu lipi?
 
unatumia akili gani mtu mjinga wewe kwani hayo mahesabu umepiga na makalio au., ...? bunge linakuwaga miezi yote au hujui unaloongea . ndezi.....

Tatizo lako matusi sasa. Toa hoja. Huu mtindo wa kutoa matusi hautujengi. Ujinga wangu uko wapi hapa? Mimi siyo mbunge wala siingii bungeni. Nimemsikia Chief Whip akisema bungeni (kupitia TV) kwamba KUB anapewa Tshs. 2,000,000.00 kwa mwezi kwa ajili ya viburudisho na hakuambiwa kwamba amesema uongo. Kwa hiyo kwa mwaka ni kiasi gani hapo? Kuna wakati Ofisi ya KUB inafungwa kwa hiyo haihudumiwi? Kumbe wakati wa Bunge tu ndio Ofisi ya KUB inahudumiwa na serikali? Acha matusi wewe. Matusi hayajengi, toa hoja ili uwaelimishe na wenzako huu si uwanja wa matusi. Tukianza kutukanana hapa hapatatosha
 
Mimi siyo mjuzi wa mambo yanavyofanyika bungeni, hivi wabunge wa upinzani au CHADENA wakikutana kuna gharama zozote kama maji ya kunywa? kama zipo zinalipiwa na fungu lipi?

Mkuu nami sina ujuzi wowote labda tupate mtu anayejua atuambie serikali inaigharimia kwa kiasi gani ofisi ya KUB.
 
Mkuu, hapa pana shida kdg Mbowe ameonesha mfano kwa kuthubutu kivitendo wkt Pinda alishindwa (ie.bucking dog never hut!!!!) lkn ikumbukwe mfumo uliopo bungeni ni wa kifisadi kwa manufaa ya wana-magamba hivyo kwa kuwa Mbowe kaanza kwa kishindo Big Up!!! mengine ya mchakato wa posho yatajipanga accordingly!! ktk hili ni muhimu villevile ku-review kanuni na taratibu za bunge kama inavyokuwa ktk katiba ndiyo tutafika vinginevyo itakuwa kilio cha samaki!!!!
THINK TWICE!!!!!
 
 
"Mwezi huu amepokea Sh2 milioni kwa ajli ya viburudisho kwenye ofisi yake kama kiongozi wa kambi ya upinzani. Ninamwuliza na hizo nazo atazirudisha? na je, ataendelea kupokea au hatapokea?" alihoji Nchemba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.
 
hawa ccm waetnga pesa yote hiyo kwa ajili ya viburudisho? mama weeeeee
 
Tatizo watu mnaleta hoja juu ya hoja. Kwanza tumalize hili la shangingi. Je, ni sawa mbowe kukataa gari hilo kama namna ya kuonesha kwa vitendo hoja ya Chadema ya kutaka serikali iache kutumia magari hayo ya bei kubwa?
Kisha, ndo tujadili posho hiyo ya ofisi ya KUB kama ni sawa au si sawa. Hii ni hoja nyingine. Na tusianze na Mbowe, maana yeye aliikuta pale, hakujipangia mwenyewe- hakuomba. Tuanze na CCM ya akina Samwel Sitta walioanzisha kiasi hicho walifikiri nini. Tukimalizana nao ndo tuje kwa bosi wangu mbowe, tumwulize kama zinazidi au zina pungua. Ila kwa sasa tuna deal na shangingi kwanza.
 
Jaman, hizo ni kwa ajil ya kukarimu wagen..nyie kwenu hamkarim wagen?..kila cku wana wagen kutoka nje na ndan ya nch
 
Kambi ya upinzani ikipokea idadi ya wageni 30,000 kwa mwaka = 24,000,000/30,000=800 kwa kila mgeni


Tuwaulize walioweka kiwango hicho kwanza ambao ni CCM kabla ya kumwuliza Mbowe ambaye amezikuta na hakuziomba. Tujidali kwanza kama ni sawa serikali kutumia shangingi au la, hilo la posho mliibue baadaye. Msipindishe hoja ya msingi.
 

Heri yako una hoja mkuu
 
Tuwaulize walioweka kiwango hicho kwanza ambao ni CCM kabla ya kumwuliza Mbowe ambaye amezikuta na hakuziomba. Tujidali kwanza kama ni sawa serikali kutumia shangingi au la, hilo la posho mliibue baadaye. Msipindishe hoja ya msingi.

Mkuu mbona Mbowe kakuta posho za vikao, kakuta Shangingi (Alikuwa anatumia Hamad R. Mohamed former KUB), amekuta nyumba mbili za KUB, per diem na kila kitu anachostahil kama KUB, n.k. Mbowe amefanya sahihi kukataa shangingi lakini pia inatakiwa aangalie na vingine pia kama hiyo posho ya viburudisho ya Tshs. 2,000,000.00 na posho zingine ambazo zinaendana na ofisi ya KUB ili kuzipunguza katika kupunguza matumizi ya serikali.
 

Mkuu mimi nadhani tunatakiwa tuongelee marupurupu, posho na stahili zingine za watumishi wa serikali ikiwa ni pamoja na wabunge na KUB kwa ujumla wake. Vingewekwa pamoja vyote tukavijadili ingekuwa safi sana. Vimekuwa vikija kwa mafungu mafungu! Tulianza na posho za vikao, zikaja per diem kwa mawaziri, imekuja magari ya fahari, juzi limekuja hili la posho ya viburudisho na huenda bado kuna marupurupu mengine. Nilisikia pia sijui wenyeviti wa kamati nao wanalipwa responsibility allowance sijui ni kiasi gani. Hizi posho ni nyingi mno tukainza moja moja itatuchukuwa muda mrefu kuzimaliza na tutasahau mambo mengine muhimu.
 
Kuna thread moja kuhusu posho nilisema waTZ wengi ni mbumbumbu wa ajabu kweli! Kwa mwandishi na msomaji mwenye akili timamu, angeuliza idadi ya ofisi za serikali zinazotengewa hilo fungu la viburudisho kama wanavyojaribu kutudanganya hapa kuwa ni la viburudisho, tungeambiwa kiasi cha hela na idadi ya ofisi halafu wananchi, (siyo chadema tu), wananchi tungekomaa na serikali. Lakini sasa wanafiki wanajaribu kupotosha kama kwamba Mbowe akikataa hilo fungu kazi imeisha! Hivi tujiulize hata hiyo hoja ya kukataa fungu hilo ikiwekwa mezani, kati ya ccm na Chadema nani atalilia fungu lisiondolewe?! Uadilifu wa vyama vikubwa vya upinzani vilivyopita uko wapi? walifanya nini? Si walikula kimyakimya kama mchwa? Bado wananchi tuviamini vyama vilivyotangulia kuongoza KUB?? NA WALAANIWE WOTE WANAOPOTOSHA UMA NA WANAOLETA UNAFIKI NA MIZAHA KWENYE MAMBO MUHIMU YA TAIFA HILI.
 
Mbona hakusema ofisi ya spika chai ni shilingi ngapi? au ya waziri mkuu, au ya mwanasheria mkuu? CCM Hovyoooo! Waziri mkuu alipewa shangingi akajifanya kulikataa wala hakusema liuzwe au lirudishwe lilikonunuliwa, mbona hawakumwambia aachie ofisi pia, au asichukue na posho zote pia? Mbona nyie vibaraka wa ccm mnakua wavivu wa kufikiri? Bajeti ya mwaka huu vibaraka wa ccm wameipitisha na matumizi ya posho ni zaidi ya Bilionii 800, sasa mbowe kupanga kutumia ( hazijatumika) milioni 24 kwa mwaka kuwapa chai wageni wanaomtembelea ofisini kwake kama kiongozi wa upinzani bungeni ndiyo tatizo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…