Mbowe asalimu amri kwa Slaa

Mbowe asalimu amri kwa Slaa

Status
Not open for further replies.
duh... kimenuka Ukawa😂😂😂😂
Mbatia Amekuwa Kunguni wa Ukawa 😂😂😂
 
Ukawa no zaidi ya mbowe na slaa,ukawa ni mamilioni ya watanzania wapenda mabadiliko.Kama mlidhani matumizi ya pesa yanaweza kuzika ndoto za Watanzania kuleta mabadiliko ya Kimfumo,mlijidanganya.Ni hivi,hata mvunje benki kwa kuwanunua wapambanaji wote,Umma wa Watanzania wapenda mabadiliko hautarudi nyuma,utasimama kidete kuhakikisha mkoloni mweusi anang'oka.

kwani mwenyekiti wa chama ni nani? na akiamua kukifuta utafanya nini unapopewa taarifa kama hii fikiri kisha chukua hatua mbowe ameuza chama kwa wamasai
 
Yani kutokumuona mbowe makujukwaani tayari mnatengeneza propaganda. Kweli mnawafuatilia ukawa
 
Baada ya mwenendo wa Kampeni kuonekana kuwa mgumu huku kila alichoahidi Lowassa kutotimia mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe aamua kukutana na aliyekuwa katibu wake Dkt. Wilbroad Slaa nchini Marekani.

Taarifa za uhakika ni kuwa Mbowe aliondoka nchini toka juzi na kupokelewa na wanachama wa Chadema tawi la DMV aliposhuka Uwanja wa Kimataifa wa Dulles huko Marekani ambapo Dkt. Slaa alimtangulia muda kidogo.

Taarifa zilizopatikana toka kwa moja ya viongozi wa tawi hilo aliyejulikana kama Kalley Pandukizi amesema ni kweli Mbowe na Slaa tumewapokea na wapo hoteli moja hapa Ohio kwa ajili ya mazungumzo binafsi. Amekiri baada ya kumpokea Mwenyekiti wao Mh. Mbowe walimpeleka moja kwa moja hotelini ambapo ndipo walipomkuta Dkt. Slaa.

Tetesi zaidi zinasema Mbowe amemuomba msamaha sana Dkt. Slaa na kumueleza walipotoka kwani mgombea waliomchukua anadhoofika kiafya kila kukicha kiasi kwamba mikutano mingine wananchi hawamsikii anapohutubia vile vile hakuna hata moja alilotimiza katika makubaliano kabla hatujampokea zikiwemo fedha za kampeni hivyo chama kinapata wakati mgumu wa kufanya kampeni kikamilifu.

Inasemekana Mbowe amemueleza Slaa kuwa ujio wa Lowassa umeigharimu Chadema kwani mpaka sasa John Mnyika hajakubali kupanda majukwaani kumnadi Lowassa kitu ambacho ni tabu zaidi kwao. Pamoja na vijana wa Lowassa kuuteka mchakato mzima wa kampeni hali inayokiuka makubaliano tuliyompa.

Kikubwa ni kuwa taarifa za ujumbe mfupi toka kwa Bi. Helen Ongara ambaye ni katibu wa BAWACHA tawi hilo la DMV ni kuwa Mwenyekiti huyo amepoteza tumaini hasa alipowapa video ya Mgombea akiomba kura kwa kigezo cha ulutheri kimewagharimu zaidi hivyo amedai watapigana ili wapate viti vya ubunge ila urais watapoteza.

Hata hivyo aliwadokeza kuwa kampeni zinaratibiwa na Lissu lakini wanafikiria kuchukua maamuzi magumu ya kuwatosa UKAWA ili wabaki wao kama wao kuliko sasa ambapo wanavibeba vyama vya NCCR MAGEUZI, NLD na CUF. Ambapo hata hivyo hali ya mpasuko imeanza kuonekana kupitia vyama vya CUF na NCCR MAGEUZI.

Walisahau Majuto ni mjukuu huja baadae!!

Vipi, hicho chanzo chako hakijakwambia kwamba Mbowe amempigia magoti Dr. Slaa arudi ili apewe Yeye nafasi kuwa mgombea na kwamba ataongea na NEC ili mbadlishano huo uhalalishwe kisheria? Au chanzo chako kimekwambia kaenda kwa Slaa KUJUTA TUUU?
 
Too cheep to believe! Yawezekana kweli Mbowe kaenda Marekani na inawzekana kabisa akawa alienda kumwona Dr. Slaa na inawezekana kabisa kua ameenda kufanya nae mazungumzo but kusema kwamba eti wajitoe UKAWA au kampeni zimepooza, hilo unatudanganya mkuu, jamaa anatwanga hadi Chato we unazungumzia kupooza?
 
Nipo hapa kayanga karagwe sasa hivi ni nooomaa aisee hakuna pa kukanyaga watu ni wengi saaana wanamsubiri raisi mtarajiwa Ndugu Edward Lowasa kwa mwitikio huu ni bora dr.slaa na hawara yake wabaki huko huko wasije kweli mabadiliko ni lazima mwaka huu..
 
Uongo km huu hata watoto walio ktk daipa hawawezi kukubali.
Eti DMV na hotel ipo Ohio ?? Mnadhiirisha Hali ni mbaya sana kwenu...
Cha kuchekesha, wengi mmejiunga from July 2015..!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom