omarilyas
JF-Expert Member
- Jan 24, 2007
- 2,130
- 145
Inasikitisha sana.
Vitendo hivi vya kutumia nguvu ni vya hatari sana. Kama kawaida hakuna hata kemeo moja kutoka serikalini hii inamaanisha kuwa serikali inavipalilia vitendo hivi vya kihuni na jinai. Kikwete na CCM jukwaani wanahubiri amani lakini matendo yanayofanywa na watu wao yanatuambia vingine.
Ni lazima kila mtu kulaani vitendo hivi kwani kama vikiachiwa hatutakuwa na nchi bali jehanamu. Ni lazima watu wote wenye mapenzi mema na nchi yetu tukemee kwa nguvu vitendo vya vijana hawa wa kihuni na kudai mara moja kuvunjwa kwa vikundi vyote vya ubabe na uhuni kama green guard. Jeshi la Polisi ni lazima lisimamie hili mara moja bila kujivuta au kutuambia kuwa linaunda timu ya uchunguzi. Vyama na watu wote wanastahili ulinzi na usalama katika kipindi hiki.
Mimi kama Mtanzania na mzalendo wa nchi yangu ninalaani kwa nguvu zote vitendo hivi vya vijana hawa wa Green Guard na ninalitaka Jeshi la Polisi kuwashika na kuwafungulia mashtaka wote waliohusika na vitendo hivi ikiwa ni pamoja na viongozi na makamanda wao wa uovu.
Kaka,
Hivi tofauti na Taarifa hii iliyoletwa na KAMENDE ambaye ni kigogo wa CHADEMA, Mgombea na pia mratibu wa kampeni za chadema huko kuna taarifa nyingine tofauti uliyoitumia katika kutengeneza na kutoa msimamo wako?
Nasubiri taarifa kutoka kwa watu na vyombo tofauti kufikia mtazamo wangu katika suala hili lakini sio hii ya KAMENDE pekee...Na nginegshauri ndugu zangu wengine humu ambao mnaheshimika kufanya hivyo. Hizi nyakati sio za kukimbilia kila habari.....upupu mwingi na SANITY has vanish into partisan air...