Chris_Mambo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2010
- 596
- 119
Jamaji dada zetu, mbona hivi? Zile blauzi ndogo zinazoacha sehemu kubwa ya mwili mbona zinavaliwa bila kuzingatia hali ya hewa? Leo asubuhi nilikuwa nashangaa njiani baada ya kupishana na wadada kibao wakiwa na viblauzi vyepesi, wakati baridi inapuliza ile mbaya mpaka mimi nilishindwa kutoka home bila ya sweta.
Jumapili pia nilikuwa kwenye sherehe ya arusi mahali fulani. Cha kushangaza, bado watu walionekana wakiwa wamevaa viblauzi vyepesi, wakati usiku ule kulikuwa na baridi pia. hamuoni kama mnajitesa? Hata kama mnatuwekea mazingira ya kutuvutia, lakini si kwa namna hiyo. Mnaweza mkavaa nguo nzito na bado mkavutia tu, hamuoni fashion show za wenzetu huko majuu? Kila msimu una aina yake ya mavazi. Msijiumize kwa kuvaa mavazi ya joto hata katika msimu huu wa baridi. hata mkifunika kila kitu na kuacha uso, tutawapenda tu kwa kuwa mliumbwa ili mtuvutie (You are flowers)!
Jumapili pia nilikuwa kwenye sherehe ya arusi mahali fulani. Cha kushangaza, bado watu walionekana wakiwa wamevaa viblauzi vyepesi, wakati usiku ule kulikuwa na baridi pia. hamuoni kama mnajitesa? Hata kama mnatuwekea mazingira ya kutuvutia, lakini si kwa namna hiyo. Mnaweza mkavaa nguo nzito na bado mkavutia tu, hamuoni fashion show za wenzetu huko majuu? Kila msimu una aina yake ya mavazi. Msijiumize kwa kuvaa mavazi ya joto hata katika msimu huu wa baridi. hata mkifunika kila kitu na kuacha uso, tutawapenda tu kwa kuwa mliumbwa ili mtuvutie (You are flowers)!