Junior Clinton Mr.
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 1,075
- 1,423
Hii ndii historia ya Israel kwa ufupi. Wayahudi Asili yao ni Iraq kutoka kabila linaitwa Huru ya wakaldayo. Ibrahimu ndiye aliyesafari na kuhama Iraq kwenda Nchi ya palestina kwa wakati huo ilifahamika kama nchi ya Kanani Pia Mungu alimhadi atampa nchi ya kanani yeye na uzao wake milele. Neno Israel ni Mungu mwenyewe Alimuita Mjukuu wa Ibrahimu Yakobo.Alimwambia hitaitwa tena yakobo bali Israel maana yake Taifa kubwa. Historia inaonyesha Baadae taifa La Babeli kwa sasa ni Iraq Lilitawala dunia kiuchumi kipindi hicho lilishambulia Israel na kuuteka Mji mkuu Yerusalemu kwa kipindi cha miaka 70. Baada ya hapo taifa la uajemi na waamedi Wakiongozwa na mfalme Koresh wa pili wakaipiku Babeli Iraq ya leo kiuchumu. Waajami kwa kwa sasa Ni taifa la (Iran) Wakawasaidi wayahudi kupata uhuru wao na kuwarejesha mateka wa Israel Yerusalemu. Wayahudi walikaa katika Ardhi ya Yao ya Yerusalemu zaidi ya miaka 470 Ndipo lijatokea shambulio la kutoka Dola ya Rumi ikiongozwa na Kamanda Tito ikaipiga Nchi ya Israel na kuharibu vikali hekalu la Sulemani Yerusalemu. Wayahudi waliosalia ambao hawakuuwawa walikombilia nchi za ulaya Magharibi na Taifa la Siberia ambalo kwa sasa Ni Urusi. Kabla Ya vita ya pili ya dunia Adolfu Hitler Akiongoza chama Cha wanazi na kukua kwa siasa sa Kifashist Alitengeneza Sera moja ya Sera zake ni kutaifisha Viwanda na makampuni yote yaliokua yanamilikiwa na Wayahudi baada ya kuchukua Hitla baada ya kuchaguliwa kuwa Cansela wa Ujerumani ndipo akaanza kutekeleza Sera zake kuwafilisi wayahudi na kuwafungu kwenye makambi ya mateso Inakadiriwa ujerumani kulikua na wayahudi zaidi ya Milioni 10 Sera za chuki za Fashism na Nashism kutoka Italia zilitengeneza chuki ndio ikapelekea mauaji Holcut walikufa wayahudi milioni 7.Mara baada ya Vita ya dunia na kuundwa Kwa Umoja wa mataifa (UNO) William james mwakilishi kutoka Uingereza alipeleka hoja ya wayahudi kupewa nchi yao wenyewe Kura ikapigwa kwa Kwa mataifa yaliokua wanachama na ikapelekea kugawanywa kwa Nchi ya palestina Israel apewe eneo Kaskazin mwa Yerusalem na Magharibi Tel Aviv ndio uwe mji mkuu Na Palestina Akapewa Upande wa kusini na Mashariki mwa Yersalemu. kimsingi Palestina alipewa eneo kubwa Zaidi ya asilimia 75 na Israel aslimi 25 ya ardhi. Jambo hili lilikua chukizo kwa nchi za kiarabu zote 1948-1950 vilikua vita vlivopewa jina (Israel Arab war) Mwaka 1956 Lilisukwa jaribia la kuishambulia Israel likashindwa. Mwaka 1967 mwezi juni Ndio vita ya kihistoria kwa Israel inafahamika Kama (Six day war). Kabla ya vita hii Dunia nzima iliingia kwenye hofu kubwa maana yalikua ndani ta vita hii mataifa mawili makubwa kiuchumi Marekani akishirikiana na Ulaya magharibi Uingereza na Ufaransa walikua upande wa Israel. Urusi ambayo kipindi hicho ndio dola lililokua linatwala dunia kiuchumi Na Muungano wa mataifa ya Ulaya Mashariki (USSR) Yalikua upande wa Waarabu. Waarabu wote wakiongozwa na Rais wa Misri Yasin Gamal Walinunua ndege nyingi na Rada za kisasa kutoka Urusi Bado Mfereji wa Suez Canal Ulibeba Manuwari za kivita nyingi. Waarabu Waliizingara Israel kila idara Kwa upande wa Kaskazini mwa Sirya walitegemea Milima Ya Golan na upande wa Kusini walitegemea milima Ya Sinai na ya Jagwa la Araba Lkn mbinu Israel Aliyotumia ni Kumshambulia adui yako kabla hajakushambuli. Israel Alifanya mashambulizi ya Anga masaa mawili mfulizo na kupelekea kuimiliki na kutawala anga lote kwa kuzipiga ndege za Misri, Sirya, Lebanon, Jordani. Na ndio vita iliyopelekea Palestinina kupoteza Eneo lote la Yerusalem Sirya kupoteza Mabonde na milima ya Golani na Misri kupoteza Mlima sinai Ila Misri alirudishiwa Mlima sinai mwa 1978 Baada ya kukubali maazimio ya Mkataba unaofahamika (Camp Devid Agreement) Moja ya makubaliano ni Misri kutojousisha kijeshi Katika Jangwa la Sinai pili Misri kutoingilia Mgogoro wowote wa Israel. Mwaka 1972 Nch za kiarabu zilipigana na Israel ili kukomboa maeneo yao zikashidwa. Mwaka 1982 Israel ilitangaza Yerusalemu ndio mji wake mkuu. Swali la kujiuliza Je! Israel kwa sasa ataachia Eneo la Palestina Jibu ni Hapana. Kwasababu tangia mwaka 1973 Israel anajijenge kijeshi na kumiliki lundo la Silaha za Maangamizi mpaka sasa Israel Haijakaguliwa ina milikiki silaha za nyuklia kiasi gani. Pili kwa sasa nchi za kiarabu zimegawanyika mfano mzuri ni huu mgogoro wa Irani na Isrel. Saudi Arabia, Baharin, Pakistani, Kazakastani, Jordani, Misri wako upande wa Israel na Saudia Arabia ameshasema Yuko taari kutoa anga yake muirani Apigwe.
Tatu sasa hivi yale mataifa ya kikomunisti yalioyokuwa adui na Israel sasa ni Marafiki mfano ni China Urusi na hata Tanzania.
Nne Kila siku mataifa ya kiarabu yakosa nguvu na kupoteza ushawishi duniani mfano Libya, Iraq, Sirya, Afganistani, Kuwet,
Tano Mataifa ya Magharibi kukua kiuchumi na kiteknolojia Yanazidi kuipa nguvu Israel kwa kutoikemea au kuiwekea vikwazo kwa pindi inapoua wapalestina.
Tatu sasa hivi yale mataifa ya kikomunisti yalioyokuwa adui na Israel sasa ni Marafiki mfano ni China Urusi na hata Tanzania.
Nne Kila siku mataifa ya kiarabu yakosa nguvu na kupoteza ushawishi duniani mfano Libya, Iraq, Sirya, Afganistani, Kuwet,
Tano Mataifa ya Magharibi kukua kiuchumi na kiteknolojia Yanazidi kuipa nguvu Israel kwa kutoikemea au kuiwekea vikwazo kwa pindi inapoua wapalestina.