Mbona Majanga

Mbona Majanga

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,037
Reaction score
34,741
Eddy ameamua kuondoka nyumbani kwa wazazi wake na kwenda kupanga, kwa bahati nzuri anapata chumba katika nyumba moja yenye vyumba sita maeneo ya Mwananyamala kwa Kopa.

Nyumba hiyo imekaa Kiswahiliswahili kutokana na wapangaji wanaoishi ndani ya nyumba hiyo.

Kila chumba kimoja kilikuwa na mpangaji mmoja aliyekuwa akiishi na familia yake.

Pia katika nyumba hiyo iliyokuwa na mabanda ya uani, waliishi wapangaji ambao hawakuwa na wake wala waume.

Kati yao walikuwepo wasichana wazuri wenye maumbile ya kupigiwa methali, ambao wengi wao hawakuwa na shughuli maalumu za kuwapatia kipato.

Baba na mama mwenye nyumba nao walikuwa wakiishi ndani ya nyumba hiyohiyo.

Siku ya kwanza Eddy alipokuwa akihamia hakuwa na vitu vingi zaidi ya kitanda kidogo, kabati la nguo na vikombe sita vya chai.

Pia alikuwa na sahani mbili za chakula na jiko moja la Mchina. Kijana huyo aliamua kuanza maisha hayo ya usela japokuwa wazazi wake walikuwa na uwezo mkubwa sana.


Baba na mama yake walimsihi sana kuendelea kukaa nao maeneo ya Kinondoni lakini wala hakutaka kusikiliza ushawishi huo.


Kikubwa alichokuwa akikitaka Eddy ni uhuru, kwani alijiona ameshakua mkubwa, hakutaka kufanya mambo ya uhuni ndani ya nyumba ya wazazi wake.


Mbali na hivyo wazazi wake walikuwa wakimdhibiti sana kijana wao kuingia katika maisha ya kupenda wanawake, hawakutaka ajiingize huko mapema.


Eddy alivumilia ucha Mungu wa wazazi wake kwa kipindi kirefu lakini alipomaliza shule tu hata kabla majibu ya kidato cha nne hayajatoka, akaamua kuhama.


Ushawishi huo aliupata kwa marafiki zake, Salim Raha na John Tupatupa ambao walikuwa na uhuru mkubwa wa kuingiza vyumbani mwao kila aina ya warembo.


Naye alitamani uhuru huo, akaamua kuwaaga wazazi wake na kuondoka katika nyumba ya familia.

Lakini kabla ya kuhama, mara kadhaa kijana huyo alikoswakoswa kunaswa na wazazi wake pale alipoingiza msichana chumbani kwake.

Siku ya kwanza alipoingia katika makazi mapya alikutana na Rehema, msichana wa Kizaramo aliyekuwa ameumbika vyema.


Eddy alishtuka kiasi hata Rehema mwenyewe kuhisi mgeni huyo alikuwa amepagawa kisawasawa. Siku hiyo mrembo huyo alikuwa akisugua miguu yake katika jiwe maalumu lililopo karibu na mlango wa kuingilia msalani.


Rehema alikua ametoka kuoga, akiwa amevaa kanga moja tu iliyokuwa imelowana na maji na kumfanya maungo yake ya ndani yaonekane.


Ndiyo, kanga ilikuwa imeshikana na mwili na kila Rehema alipokuwa akisugua kisigino chake, ndivyo alivyokuwa akimpagawisha Eddy kutokana na kuzalisha mtetemeko wa haja katika mlima aliokuwa ameufungashia nyuma ya mgongo wake.

Kijana huyo alibaki ameduwaa kwa kitambo kirefu akimwangalia Rehema huku akiwa ameshika sahani mikononi mwake lakini Rehema ndiyo kwanza akajifanya kama vile hakuwa amemuona.

Binti huyo akaendelea kufanya kile alichokuwa akikifanya, mara alishtuka aliposikia mlio wa vyombo vikipasuka.

Ndiyo, Eddy alikuwa ameziachia sahani alizokuwa amezishika mikononi mwake bila ya kutarajia.

Kufuatia mlio uliotokana na sahani kuvunjika, Rehema alimgeukia Eddy na kumuuliza kulikoni ndipo kijana huyo alimwambia zilimteleza kwa bahati mbaya
.

Ndiyo kwanza mchezo unaanza, unataka kujua zaidi? Weka Like chini ndio nitajuwa munaipenda hii hadithi pasipo weka like sitoweza kuendelea na Hadithi Mpya mnasemaje kuhus hadithi mpya?
 
We Mzizi wewe mbona hadith zako zinahamamasisha mambo fulani.....
 
iko poa...mbona manapenda kutumia sana hilo jina la tupatupa kwenye hadidhi..?
 
Hii kitu mbona inataka kufanana na clip moja hivi kwenye Inye ya kina Majuto, Masele, Senga n.k
 
MziziMkavu

hahahaa umerudi tena na hadithi?karibu sana tulizimisi,ila kwa nini usitoe kakitabu fulani maana una uandishi mzuri saaaana hongera
 
Last edited by a moderator:

Rehema alikua ametoka kuoga, akiwa amevaa kanga moja tu iliyokuwa imelowana na maji na kumfanya maungo yake ya ndani yaonekane.


Ndiyo, kanga ilikuwa imeshikana na mwili na kila Rehema alipokuwa akisugua kisigino chake, ndivyo alivyokuwa akimpagawisha Eddy kutokana na kuzalisha mtetemeko wa haja katika mlima aliokuwa ameufungashia nyuma ya mgongo wake.

Kijana huyo alibaki ameduwaa kwa kitambo kirefu akimwangalia Rehema huku akiwa ameshika sahani mikononi mwake lakini Rehema ndiyo kwanza akajifanya kama vile hakuwa amemuona.



mmmnnnhh... makusudi mabaya hayo... hakunaga mjanja hapo
 
Majangaaa Mbona Majangaaa! - 2-


Binti huyo akaendelea kufanya kile alichokuwa akikifanya, mara akashtuka aliposikia mlio wa vyombo vikipasuka.
Ndiyo, Eddy alikuwa ameziachia sahani alizokuwa amezishika mikononi mwake bila ya kutarajia.
Kufuatia mlio uliotokana na kuvunjika kwa sahani hizo, Rehema alimgeukia
Eddy na kuumuliza kulikoni, ndipo kijana huyo akamwambia zilimteleza kwa bahati mbaya.

HEBU NENDA NAYO…


“Vipi kaka…?” Rehema alimuuliza Eddy.
“Aaah, sahani zimeniteleza kwa bahati mbaya…”
“Pole sana…,” alisema Rehema na kisha kuendelea kusugua visigino vyake huku akitingisha wowowo lake katika staili ile ya hamsini hamsini mia.
“Majangaaa…!” Eddy alisema kwa sauti ya upole na kujilazimisha kuingia ndani ya chumba alichokuwa amepanga.
Kichwani mwake alikuwa akimfikiria Rehema, akawa anajiuliza kama anaweza kuachana na wanawake wote ili awe na huyo.
“Sasa hapa nitamletaje Amina, nitamletaje Anita?” alijiuliza na kuwa na wasiwasi na mwonekano wa Rehema kwa kuwa alikuwa akionekana kama ni mkorofi fulani hivi.
“Anaonekana mshari-mshari sana, sijui kama nitamuweza,” alizidi kufikiria Eddy na kujitupa katika kitanda kilichokuwa kimemaliziwa kufungwa muda mchache na watu waliofika kumsadia.
Ghafla akiwa hapo, alisikia sauti nyingine ya msichana ikimwita Rehema.
“Dada mkubwa… dada mkubwa…”
“Abee,” Rehema aliitikia kwa kuwa ni yeye ndiye aliyekuwa akifahamika kama dada mkubwa ndani ya nyumba hiyo iliyokuwa wakiishi wasichana wengi.
Wengi wao walikuwa wakimheshimu Rehema kutokana na umri wake na uzoefu wake katika masuala ya mapenzi, pia ndiye aliyekuwa mshauri mkuu wa kila jambo kwa mabinti wengine mtaani hapo.
“Njoo uone mambo huku…,” alisema msichana aliyekuwa akimwita Rehema.
“Kuna nini jamani?”
“Patra kafumaniwa huku…,” alisema msemaji huyo na miguu yake kusikika akitoka nje kwa mlango mkubwa wa upande wa barazani.
“Patra…!” alishangaa Rehema na kufanya binti yule kurudia kusema kwa msisitizo.
“Ndiye yeye kwani mtaani kuna Patra wangapi?”
Eddy alikuwa akitaka sana kumuona huyo binti mwingine ambaye alikuwa na sauti nzuri kama kinanda, akili yake ilimtuma kama angemuona angeweza kufanya uchaguzi bora kati ya Rehema na huyo binti.
Ingawaje moyoni Eddy alikuwa amekufa kwa Rehema lakini wasiwasi wake ulikuwa ni jinsi alivyokuwa amekaa kimtoto wa mjinimjini sana.
Hata hivyo hakuweza kutoka kumwangalia msichana aliyekuwa akimwita Rehema, hakutaka kuonekana kama vile ni mmbeya kwa kufuatilia mambo ya watu, akauchuna kwa kuendelea kulala kitandani pake huku akitafakari jinsi atakavyoendesha maisha yake katika makazi hayo mapya.
Mara miguu ya Rehema nayo ikapita katika chumba chake kwa kasi na kutoka nje kupitia mlango wa barazani.
“Daaa huyu mtoto mkali sana lakini…,” alijisemea moyoni Eddy.
****
Siku hiyo Eddy hakutoka nje, kwa kuwa ilikuwa ni jioni hakuona umuhimu wa kufanya hivyo, alikuwa ameshakula na hakujisikia kuoga. Akaamua kuendelea kulala.
Asubuhi siku ya pili, mapema sana Eddy alikuwa ni mtu wa kwanza kutoka nje, akakutana na baba mwenye nyumba na kusalimiana naye.
“Za asubuhi baba?”
“Nzuri tu, umeamkaje?
“Sijambo, shikamoo.”
“Marhaba… tena afadhali umewahi kwenda kuoga ukichelewa hapa… utajuta,” baba mwenye nyumba alisema na kumpongeza Eddy aliyebaki na maswali kibao baada ya kusikia kauli hiyo.
Huku akishindwa kupata jibu, Eddy moja kwa moja akaingia msalani na kumaliza haja zake muhimu na kisha kuelekea bafuni.
Lilikuwa ni bafu la kiswazi ambalo ungeweza kuchungulia na kumuona mtu wa nje kwa kupitia pachipachi za mlango na sehemu za kidirisha kidogo.
Akaanza kujimwagia maji. Hazikuchukua hata dakika tano akasikia milango ikigongana, akaacha kujimwagia maji na kuchungulia nje.
Walikuwa ni wasichana watatu, mmoja alikuwa ni mrefu na mwembamba lakini pamoja na wembemba wake, alikuwa amejengeka vyema katika kiuno kwani alikuwa amekatika na kuwa na kiuno kama cha nyigu.
Mwingine alikuwa ni mnene, mfupi kiasi lakini alikuwa na mvuto wake kutokana na rangi ya mwili wake ambayo ilikuwa iking’aa kwa weusi wake.
Wa tatu alikuwa ni msichana mrefu na mnene ambaye kwa harakaharaka Eddy aliweza kumbaini kuwa ni yule aliyekuwa akimwita Rehema jana yake na kumwambia kwamba Patra kafumaniwa.
Wote watatu walikuwa wakigombania kuingia msalani lakini kwa kuwa yule msichana mrefu na mnene alikuwa na nguvu zaidi yao, akawawahi na kwenda kuingia msalani.
Alipofanikiwa kuingia msalani, wala hakuchelewa kwa kuwa alikuwa amevaa khanga, aliweza kujiachia na kuanza kumwaga haja ndogo kama kuachia bomba la maji huku akisema maneno ya kuwananga wenzake aliokuwa amewashinda.
Kujiachia kwake bomba la maji litiririke bila ya mpangilio, Eddy akajua kuwa huyo binti hakuwa amepata mafunzo ya kutosha.
Eddy alikumbuka siku moja aliwahi kuambiwa na jimama moja kwamba anayekwenda haja ndogo kwa staha ni yule anayejua kujibana na kujiachia taratibu bila ya kusikika sauti kama vile mbwa au ng’ombe.
Hata hivyo, Eddy alikuwa amempenda msichana huyo, ingawaje moyo wake ulikuwa pia umedondokea kwa Rehema. Akawa anasisimka kwa jinsi alivyokuwa akiiachia bomba lake kwa fujo.
“Daaa! Huyu naye sijui ni mtoto wa mwenye nyumba?” alijiuliza.
Hadi alipokuwa akitoka, Eddy aliendelea kumwangalia kupita upenyo, badala ya huyo wakaendelea wasichana wengine waliokuwa wakigombea naye kuingia msalani.
Baada ya hapo, wakafuatia wengine wengi ambao kwa jumla yao wangeweza hata kufikia timu ya mpira wa miguu.
Eddy alishangaa wote hao walikuwa wakiishi vipi katika nyumba hiyo, kama vile haitoshi akajiuliza mbona jana yake wakati alipokuwa akifika, hakuwaona.
“Majangaaa, jamani mbona Majangaaa!,” alisema Eddy kimoyomoyo wakati alipotoka nje na kukutana na wasichana hao kibao wakiwa wamejipanga uwani kwa ajili ya kwenda kuoga.
“Samahani kaka naomba sabuni…” alisema yule msichana wa kwanza aliyewawahi wenzake kwenda msalani akimwambia Eddy.
“Bila wasiwasi,” Eddy alisema na kumkabidhi binti huyo sabuni yake ya kuogea.
“Daa! Unaanza kujipendekeza kwa mgeni,” alisema msichana mwingine na kuwafanya wengine nao waongeze maneno yao kedekede ambayo hata hivyo binti yule hakuyajali.


Itaendelea Alkhamisi ijayo..............
 
Back
Top Bottom