Nawezaje kuepuka ugali
Nawezaje kuepuka wali
Maisha ya kigeto kgeto
Ugali una wanga ambao ni hatari
Wali una sukari ambayo ni hatari Sasa ntafanyaje mana migahawani hakuna diet wenzangu mnawezaje?
Ki-Tanzania ni vigumu kuepuka vyakula vya wanga kama vile Ugali, wali, viazi, mihogo n.k.
Vitu vya kufanya :-
Epuka kula kila muda. Endapo una Njaa, Tenga muda maalumu kwaajili ya kula na ukashiba sio kuonja onja mfano Chakula cha mchana na Usiku.
Tumia matunda ya msimu na epuka kula mchanganyiko wa matunda mengi kwa wakati mmoja, kula Tunda la aina moja kwa wakati moja.
Epuka kula Asubuhi, fiziologia ya Binadamu haikubaliani na Kula asubuhi mara baada ya kuamka. Unaweza kula muda wowote kuanzia mchana saa 6 mchana hadi Jua linapozama saa 12 jioni au 1 usiku. Ikikushinda sana mwisho saa 2 Usiku.
Kunywa maji ya kutosha Asubuhi na wakati unasikia Njaa au hamu ya kula nje ya muda wa kula.
Fanya mazoezi ya mwili mara 3 mpaka 4 kwa wiki kulingana na ratiba yako, Mapumziko ni muhimu kama ilivyo kwa mazoezi.
Unaweza kuchagua kutumia kanuni hii
A:N. Ambapo A ni muda wa kutokula(fasting) na N ni muda unaoweza kula(Feasting). Chagua
16:8 au 18:6 zinafaa Ki-Tanzania.
Mfano kama ni 16:8 unakula lunch saa 6 mchana basi supper ni saa 2 usiku. Kama ni 18:6 utakula lunch saa 6 mchana na supper saa 12 Jioni au utakula lunch saa 8 mchana na supper 2 usiku.
Punguza mawazo na hofu kuhusu vyakula, Muhimu ni mwili Upate wakati wa kufanya marekebisho na matengenezo yaani Wakati bila chakula. Mwili unapokuwa na chakula Tumboni hujikita katika umeng'enyaji wa chakula kilichopo na huahirisha shughuli nyingine kama matengenezo na marekebisho ya mwili
mfano kuimarisha kinga, kuondoa sumu zitokanazo na vyakula na shughuli nyingine n.k.
Mwili wa Binadamu unaweza kujitibu pekee yake, Muhimu ni kuupatia Muda wa kufanya kazi hiyo.
Relax, Don't complicate, Avoid Obsession and Goodluck Lad.