fimboyaasali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 8,416
- 7,969
Kwa sasa inahitajika mbinu nyingi ili kupata mke au mume. Mkibaki kusubiri kuchumbiwa au kuchumbia, mtazeeka bika kuoa au kuolewa. Sasa jaribuni mbinu hizi:
1. Msikae ndani wiki nzima, toka nje, kama kuna matamasha nenda, mikutano mbalimbali nenda, kila aina ya mikusanyiko unayoweza kwenda basi wewe nenda.
2. Mikutano au vikao vya kidini, nenda bila kukosa labda kama umesafiri au unaumwa. Kwenye hivyo vikao jitahidi kuongea usikae kimya.
3. Kusali ni muhimu sana, kwa hiyo dini yako. Viongozi wako wa kidini wafanye kuwa marafiki na uwe muumini mzuri, mwenye nidhamu kubwa maana huwa wanaombwa sana kuwatafutia wenza
4. Kwa kuzingatia bajeti yako toka kwenye pub mwisho wa wiki hata kama hunywi bia,nenda kanywe juice, kula nyama,ongea na watu, kubadilishana mawazo.
5. Kuvaa vizuri, kila siku vaa vizuri bila kujali kama ni nguo za gharama, vaa kwa mpangilio na ni muhimu sana kuvaa viatu vizuri kila siku.
6. Dating sites jiandikishe na kujaribu bahati yako pia huko, hapa pia zingatia bajeti yako maana zingine ni za kulipia.
7. Usiogope kuongea na marafiki zako kuulizia kama kuna mtu anatafuta mke au mume, na ukiwajua nenda kaongea nao kuonesha utayarifu wako kuoa au kuolewa.
8. Tengeneza vigezo vyako vya mume au mke unayemtaka, ili iwe rahisi kuchagua.
9. Shiriki mazishi kadri unavyopata nafasi na uwe umevaa kiheshima.
10. Shiriki jogging mbalimbali ambazo hutangazwa na huko jichanganye na watu wa kila aina.
11. Chagua timu ya mpira moja uishabikie na uwe unaenda viwanjani na uwe umevaa vizuri.
12. Siku zote uwe msafi kwa mwili na nguo,usinuke mdomo, kikwapa na jasho kwani hiyo itakunyima mke au mme.
13. Chunguza uwajue ni wanawake wepi au wanaume ambao hawajaoa au kuolewa, ukiwajua fanya urafiki nao mpaka umpate mmoja ambae unaweza kuongea nae.
14. Jitahidi sana kutotembea na wanawake hovyohovyo au wanaume hovyohovyo, usimvulie kila mtu auone uchi wako.
15. Jifunze sex vizuri, uwe na stamina, na mbinu nyingi za kujamiiana, ili unapopata mpenzi umpe manjonjo ya hatari.
16. Fanya urafiki hapo mtaani unapokaa na wazazi ambao wana watoto wa kike na kiume ambao hawajaoa au kuolewa ili uwaambie upo tayari kuoa au kuolewa
17. Jitahidi sana kuongea kwa hadhari kila unapopata fursa kuongea.
18. Sali kila siku kuomba Mola wako akupe mme au mke.
19. Usisite kuja inbox kupata usaidizi uoe au uolewe na ni bure. Msikae ndani kusubiri, tokeni.
20. Kwa wanawake jitahidi sana usizae nje ya ndoa.
1. Msikae ndani wiki nzima, toka nje, kama kuna matamasha nenda, mikutano mbalimbali nenda, kila aina ya mikusanyiko unayoweza kwenda basi wewe nenda.
2. Mikutano au vikao vya kidini, nenda bila kukosa labda kama umesafiri au unaumwa. Kwenye hivyo vikao jitahidi kuongea usikae kimya.
3. Kusali ni muhimu sana, kwa hiyo dini yako. Viongozi wako wa kidini wafanye kuwa marafiki na uwe muumini mzuri, mwenye nidhamu kubwa maana huwa wanaombwa sana kuwatafutia wenza
4. Kwa kuzingatia bajeti yako toka kwenye pub mwisho wa wiki hata kama hunywi bia,nenda kanywe juice, kula nyama,ongea na watu, kubadilishana mawazo.
5. Kuvaa vizuri, kila siku vaa vizuri bila kujali kama ni nguo za gharama, vaa kwa mpangilio na ni muhimu sana kuvaa viatu vizuri kila siku.
6. Dating sites jiandikishe na kujaribu bahati yako pia huko, hapa pia zingatia bajeti yako maana zingine ni za kulipia.
7. Usiogope kuongea na marafiki zako kuulizia kama kuna mtu anatafuta mke au mume, na ukiwajua nenda kaongea nao kuonesha utayarifu wako kuoa au kuolewa.
8. Tengeneza vigezo vyako vya mume au mke unayemtaka, ili iwe rahisi kuchagua.
9. Shiriki mazishi kadri unavyopata nafasi na uwe umevaa kiheshima.
10. Shiriki jogging mbalimbali ambazo hutangazwa na huko jichanganye na watu wa kila aina.
11. Chagua timu ya mpira moja uishabikie na uwe unaenda viwanjani na uwe umevaa vizuri.
12. Siku zote uwe msafi kwa mwili na nguo,usinuke mdomo, kikwapa na jasho kwani hiyo itakunyima mke au mme.
13. Chunguza uwajue ni wanawake wepi au wanaume ambao hawajaoa au kuolewa, ukiwajua fanya urafiki nao mpaka umpate mmoja ambae unaweza kuongea nae.
14. Jitahidi sana kutotembea na wanawake hovyohovyo au wanaume hovyohovyo, usimvulie kila mtu auone uchi wako.
15. Jifunze sex vizuri, uwe na stamina, na mbinu nyingi za kujamiiana, ili unapopata mpenzi umpe manjonjo ya hatari.
16. Fanya urafiki hapo mtaani unapokaa na wazazi ambao wana watoto wa kike na kiume ambao hawajaoa au kuolewa ili uwaambie upo tayari kuoa au kuolewa
17. Jitahidi sana kuongea kwa hadhari kila unapopata fursa kuongea.
18. Sali kila siku kuomba Mola wako akupe mme au mke.
19. Usisite kuja inbox kupata usaidizi uoe au uolewe na ni bure. Msikae ndani kusubiri, tokeni.
20. Kwa wanawake jitahidi sana usizae nje ya ndoa.