Mbinu za kivita zinavyompaisha Membe

Mbinu za kivita zinavyompaisha Membe

Mkuu hizo negativity ulizozungumza kuhusu Membe ni kweli kabisa, ila ni nusu tu ya tabia za jiwe, ila tu humzungumzi kuhusu hizo tabia kisa huwa unajipendekeza kwa kiongozi aliye madarakani.
Hoja yako ni ipi hapo ndugu ?? Maana umezungumzia mambo mawili yasiyo na uwiano.
 
Hoja yangu hapo ni acha kujikomba boss.
Hiyo siyo hoja ni kioja.

And next time Kama unaona unakereka na hoja zangu it's better ukaachana nazo.

Natumia Uhuru wangu wa kutoa maoni Kama wewe; tusipangiane Cha kuandika.

And please don't cross that line.
 
sijaona mahusiano ya hizo mbinu za kivita na ulichokizungumzia juu ya Membe.

Membe nitamkumbuka kama aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje kipindi tulichokuwa na migogoro na nchi za Rwanda na Malawi, zaidi ya hapo sina ninachokumbuka kumhusu huyu mtu.

Ninachoona kwake ni mtu anaye endekeza siasa za makundi na anayeamini katika matabaka.

Vile vile asiyemvumilivu kisiasa kwani kipindi kile anataka kugombea alituambia wazi kuwa akifanikiwa kuwa Rais maadui Zake 11 watahama nchi.

Vile vile kesi yake na Musiba ni kiashirio kingine cha ukosefu wa uvumilivu kisiasa unless anataka kuitumia hiyo kesi kama Jukwaa la kumrejesha katika lingo za kisiasa.

ili kujua kuwa Membe sio mvumilivu kisiasa kauli ndogo tu ya Rostam imetosha kabisa kumfanya aweke hadharani mipango yake ya kugombea Urais 2020.
Ila Magufuli atakuwa zaidi ya Membe,kwa matukio tunayoshuhudia awamu hii?
 
Back
Top Bottom