Mbilia bell v/s Tshala mwana

Mbilia bell v/s Tshala mwana

yutu

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2013
Posts
1,778
Reaction score
1,226
Mbilia bell akiongoza kwa hits kama Nakei na Nadina, ye Tshala mwana aki-hits kwa Massuwa na Dezo dezo.
Ni kati ya wanamuziki wa kike wa Congo waliowahi kutamba miaka ya 80 mpaka 90 na mpaka sasa.

Japo wote walifanya vizuri, lakini kimizania unafikiri nani anaweza kumzidi mwenzake?
 
unapenda dezo dezo we bwana wee yatakushinda

kodi ya nyumba hulipi maji hutaki kulipa operesheni kata inakujaa...

Tshala Mwana nuksi
 
ivo yondo alikimbiza miaka gani? maana alikuwa anaweza sana
 
Mbilia bell akiongoza kwa hits kama Nakei na Nadina, ye Tshala mwana aki-hits kwa Massuwa na Dezo dezo.
Ni kati ya wanamuziki wa kike wa Congo waliowahi kutamba miaka ya 80 mpaka 90 na mpaka sasa.

Japo wote walifanya vizuri, lakini kimizania unafikiri nani anaweza kumzidi mwenzake?

mkuu naomba niwe mkweli tu.sidhan kama atapatikana mshind hapa.hivi vilikuwa vichwa ni sheeeda.umenikumbusha .mbali mkuu
 
Mbilia bell akiongoza kwa hits kama Nakei na Nadina, ye Tshala mwana aki-hits kwa Massuwa na Dezo dezo.
Ni kati ya wanamuziki wa kike wa Congo waliowahi kutamba miaka ya 80 mpaka 90 na mpaka sasa.

Japo wote walifanya vizuri, lakini kimizania unafikiri nani anaweza kumzidi mwenzake?

Mkuu Unafananisha Rais Wa Nchi Na Diwani Wa Kiaka Nkumbi? Tshala Muana Ni Habari Nyingine Na Hata Mbilia Mbel Analijua Hilo.
 
Hapo ni sheeda kupata mkali kama ilivyo kwa dally Kimoko na diblo dibala kwenye gitaa la solo.

Wote Nawaheshimu Ila Gitaa La Diblo Hata Waliolala Wataamka Na Kucheza Wakati Gitaa La Dally Kimoko ( Dalikike au Gitare Enzanga Likwanza ) Malaika Wote Mbinguni Wanacheza Na Vichanga Tumboni Mwa Mama Zao Vinacheka Huku Miti Nayo Ikitikisika.
 
Dally Kimoko napenda akilipiga gitaa la bass sauti mwaaaa kwenye speaker, Tshala Muana ana style yake na hata Mbilia Bell, sasa ukijaribu kuwafananisha ni kama unafananisha vitu viwili tofauti, kila mmoja ana style yake na hakuna atakayeweza kupiga kiufundi au kiubunifu zaidi yao tena labda atokee mwingine aliyechipukia

Miziki yao mpaka leo inasikilizwa!
 
Dally Kimoko napenda akilipiga gitaa la bass sauti mwaaaa kwenye speaker, Tshala Muana ana style yake na hata Mbilia Bell, sasa ukijaribu kuwafananisha ni kama unafananisha vitu viwili tofauti, kila mmoja ana style yake na hakuna atakayeweza kupiga kiufundi au kiubunifu zaidi yao tena labda atokee mwingine aliyechipukia

Miziki yao mpaka leo inasikilizwa!

Samahani Kidogo Mkuu Na Naomba Nikurekebishe Kidogo Kuwa Daly Kimoko Hapigi Na Hajawahi Kupiga Bass Giutar Isipokuwa Daly Ni Mpigaji Wa Guitar La Solo Isipokuwa Pakitokea ktk Nyimbo Hiyo Mfumo Wake ( Rhythm ) Hauendani Na Upigaji Wake Wake Yeye Hushirikishwa Tu ktk Rhythm Guitar. Kwa Mfano ktk Nyimbo Kadhaa Za Hayati Pepe Kalle Kuna Wakati Yeye Alikuwa Akipiga Rhythm Guitar Kwakuwa ktk Solo Guitar Lenyewe Alikuwepo Bingwa Na Mkonge Le Roi Dilu Dilumona Ambaye Shughuli Yake Inapatikana Haswa ktk Albam Ile Ya Pepe Kalle Yenye Nyimbo Tamu Na Nzuri Ya MAMIE.

Tafuta Pia Album Za Hivi Karibuni Za Aurlus Mabele Na Utagundua Kuwa Daly Ameshirikishwa Karibia ktk Nyimbo Zote Kama Mpiga Guitar La Rhythm Kwakuwa ktk Solo Guitar Sasa Kuna Kijana Mmoja Ambaye Wakongo Wanasema Ni Tishio Kwa Ukung'utaji Wake Nae Ni Cain Madoka Na Anakodiwa Sana Na Wanamuziki Wa Congo DRC Na Congo Brazaville. Tupo Pamoja Mkuu Na Nafurahi Pia Kuona Kumbe Bado Kuna Watanzania Wenzangu Wenye Mapenzi Na Miziki Ya Kizairwaaaa!
 
unapenda dezo dezo we bwana wee yatakushinda

kodi ya nyumba hulipi maji hutaki kulipa operesheni kata inakujaa...

Tshala Mwana nuksi

Huu wimbo originally ni wa Ndala Kasheba. Tshala aliiba kutoka Tanzania
 
Sisi wa Dayamondo na Alikibakuli ngoja tukae kimya tu,tuwaachie manguli..
 
Mbilia Bell ana hits zifuatazo ninazozijua mimi: 1. Eswi Yo Wapi 2. Boya Ye 3. Wendenda 4. Yamba Ngai 5. Nadina 6. Beyanga 7. Nakei Nairobi 8. Africa (sina uhakika na hili jina)

Kwa upande wa Tshala Muana mi nazoziona nzuri ni 1: Karibu yangu 2: Kizongou zoungo.

Mimi binafsi naona Mbilia Bell ni mkali sana dhidi ya Tshala Muana.
 
Mkuu, nashukuru sana kunirekebisha,

Muziki wa Kizairwaa walionifundisha kuipenda ni Mapacha wa bendi ya Tancut na wimbo mmoja hivi wa Monica eee eee Monica eee eeee eee....huu wimbo niliupenda kupitiliza tena nilikuwa darasa la kwanza hapo na tancut wenyewe waliupiga muziki unaoendana na Kizairwaa....

Mimi kwa kusema kweli ni mshabiki wa JB Mpiana kuanzia Kala Yi Boeing...napenda sana zile za live concert za wanamuziki wa kicongo si JB Mpiana tu, na wengineo hata Cindy wa Koffi Olomide
 
Wote Nawaheshimu Ila Gitaa La Diblo Hata Waliolala Wataamka Na Kucheza Wakati Gitaa La Dally Kimoko ( Dalikike au Gitare Enzanga Likwanza ) Malaika Wote Mbinguni Wanacheza Na Vichanga Tumboni Mwa Mama Zao Vinacheka Huku Miti Nayo Ikitikisika.

weweeeeeewwwweeeeeee mikono chiniiiiii miguuu juuuu
 
Papa Mopao

nikusahihishe kidogo papa mopao wimbo wa monica aliimba ndala kasheba, kama utakukumbuka vizuri ilikuwa ni kesi ya kanga na muhusika alilimbilia zambia
 
Last edited by a moderator:
unapenda dezo dezo we bwana wee yatakushinda

kodi ya nyumba hulipi maji hutaki kulipa operesheni kata inakujaa...

Tshala Mwana nuksi

nimekupata mkuu mo11,
kuna huyu dada mwingine anaitwa lady issa japo ana hits chache lakini nae yuko vizuri sana.
 
ivo yondo alikimbiza miaka gani? maana alikuwa anaweza sana

ni kweli KIFUSO yondo nae alikimbiza lakini ilikuwa miaka 94 mpaka 96 ni kwa muda mfupi sana na alikuwa anapiga miondoko ya soukous na isitoshe alibebwa sana kundi la soukous starz na humo ndani kulikuwa na wakongwe kama jimmy balon, shimita, lokasa ya mbongo balou kanta na wengineo wengi
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom