Mbeya yachafuka polisi wapambana na wamachinga

Mbeya yachafuka polisi wapambana na wamachinga

BREAKING NUUZ: Polisi wapiga Risasi wananchi Mbeya washindwa tuliza Vurugu.. Sasa zimefika uyole wananchi wanashusha Bendera za CCM




majeruhi wa risasi za polisi katika vurugu za Mwanjelwa leo hii akiwa kapigwa kichwani. Hadi sasa kuna majeruhi wanne wa risasi, wawili kichwani, mmoja kwenye paja na mwingine mkononi

Mmoja wa majeruhi wa risasi za polisi katika vurugu za Mwanjelwa leo, Abel Mwalukali akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa Mbeya baada ya kupigwa risasi kwenye mkono.



Polisi wakijaribu Kuzuia Ghasia katika eneo hilo na kufukuza Wamachinga

Baadhi ya wananchi wakiwa wameokoka katika eneo hilo

Wamachinga Mbali mbali wakikimbia katika eneo la tukio wakati wa machafuko hayo yamepamba moto


Watu Mbali Mbali wakiwa wanakimbia ili kujiokoa na Hatari katika eneo hilo


Picha zote na Mpiga picha wetu maalum​



Kwa kweli mpiga picha amefanyakazi nzuri na katika mazingira magumu, anastahili pongezi!!!!!

Tiba
 
Kwa kweli mpiga picha amefanyakazi nzuri na katika mazingira magumu, anastahili pongezi!!!!!

Tiba

Kweli kabisa Mkuu maana picha zinatuonyesha hali halisi ya tukio na si ajabu kutakuwa na video ambazo labda zinaweza kuwekwa kule Utube kwenye muda muafaka.
 
Nadhani sasa watanzania wote wanajua ni kwanini Nyerere alimkataa prezidaa kuwa hafai kuwa raisi
 
Mbona watu wenyewe wawili tu?

kama watu ni wawili mbona tokea saa saba mchana wa leo hadi saa hii ya kumi na ushee askari wanaungurumisha mabomu tena kwenye kitongoji kidogo tu cha Uyole. Kinachotokea ni kuviziana na sijui mabomu yataendelea hadi saa ngapi.
 
Kweli nguvu ya umma ni noumer!Lori limetumika sambamba na jiwe kwenye position kuziba barabara.
 
sasa ndio tunatoka ofisini hakuna daladala magari ya watu binafsi wanalazimika kuyaacha maofisini maana hawawezi kupita nayo hiyo njia tunalazimika kutembea kwa miguu vichochoro mdogo mdogo hadi home. risasi barabarani zaendelea mabomu ya machozi na askari magambo jwtz ffu wote wapo njiani jamani nitaendelea kuwaupdate ngoja niingie huko mtaani
 
Kituo cha polisi ilomba,kimevunjwa, watuhumiwa wamekimbia,na kimechomwa moto. Ni kituo cha polisi cha pili kuchomwa,kingine ni cha uyole.Inasemekana watu wengine kutoka Mbalizi wameenda kuungana na wenzao kupambana na askari. Wananchi wanapiga simu redioni, wanasema hawamtaki Kandoro.

Mbunge wa mbeya mjini yupo njiani kuelekea Mbeya.
 
quote_icon.png
By Bundajo
Mbona watu wenyewe wawili tu?
Inaonekana hawa watu wawili ni ma superman wamefanya hadi wajesi waingilie kati.
 
nimeseme kitu kimoja wadau, serikali ya ccm haiwezi kufika 2015 kwa hali ilivyo sasa. kandoro acha ubabe wa kijinga, watz wengi ni masikini sana, hawana uwezo wa kufanya biashara kubwa ambazo zinatakiwa na ccm. mungu ibariki tz, viva cdm, viva tz
 
GUD nimeshaiweka kwenye pc yangu maana moda hawakawii kuinyofoa
Mkuu kuinyofoa ama kutokuinyofoa haina maana kama habari yenyewe ni ya ukweli ama hata kama si ya kweli,basi cha muhimu ni ku hesabu hizo siku 100 walizotowa.

Haya ya Mbeya bado sidhani kama yana uhusiano wowote na hawa watu.

However wananchi wamekuwa very desparate na siwezi kushangazwa kama kuna some orgnaization ya hata wanajeshi waliochoshwa.

Huwezi juwa watu wamevaa kiraia bado.
 
Watakuwa wamfeanya kosa kubwa sana kama wameamua kutumia jeshi liwasaidie polis.....huilo kosa alilifanya Mubarak

Jeshi linapokea amri kutoka kwa amiri jeshi mkuu, rais wa jamhuri ya muungano. Hii ni dalili sasa JK ameamua kutumia jeshi la wananchi ili kuwaangamiza wananchi wenyewe. Huu wote ni ubutu wa kutumia akili unaofanywa na CCM. Kwao wao sasa wananchi si lolote bali wao wanajivunia kuwa na dola. Huwezi kushawishi wananchi wawe watii kwa kutumia dola bali ni haki. Ule wakati wa kutawala watanzania kama vile zizi la ng'ombe umeisha, sasa hivi inahitajita akili zaidi kuliko maguvu.
 
Kituo cha polisi ilomba, kimevunjwa,watuhumiwa wamekimbia,na kimechomwa moto.Ni kituo cha polisi cha pili kuchomwa,kingine ni cha uyole.

Inasemekana watu wengine kutoka Mbalizi wameenda kuungana na wenzao kupambana na askari. Wananchi wanapiga simu redioni, wanasema hawamtaki Kandoro. Mbunge wa Mbeya mjini yupo njiani kuelekea Mbeya.

Wavunje vyote havina mana!!!!.
 
Kituo cha polisi ilomba,kimevunjwa,watuhumiwa wamekimbia,na kimechomwa moto.Ni kituo cha polisi cha pili kuchomwa,kingine ni cha uyole.Inasemekana watu wengine kutoka Mbalizi wameenda kuungana na wenzao kupambana na askari.Wananchi wanapiga simu redioni,wanasema hawamtaki Kandoro.Mbunge wa mbeya mjini yupo njiani kuelekea Mbeya.
This is the time when gov. need reconciliation from the opposition.
 
Back
Top Bottom