Inkoskaz
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 6,360
- 2,389
Wadau,
Clip hii sijui ni shule gani lakini yaonekana ni hapa nchini kutokana na sauti ya dada inayosikika kwenye background.
Hata kama huyo kijana amekosa vipi si angepelekwa vyombo vya sheria?
Wana tofauti gani na wale wanakijiji walioua watafiti?
Sheria ifuate mkondo wake, inaumiza sana.
=======
UPDATE:
Mkuu wa shule ya Mbeya Day pamoja na baadhi ya walimu wamechukuliwa na jeshi la polis kwa mahojiano zaidi. Tukio hilo lilitokea 28. September.
Jumanne tarehe 24 mwalimu wa vitendo alitoa homework kwa kidato cha 3 A, kwa bahati mbaya mwanafunzi huyo hakuwepo, Jumatano wakati mwalimu anakusanya homework yule mwanafunzi alimwambia mwalimu kuwa jana yake hakuwepo alikuwa anaumwa.
Mwalimu alianza kumpiga makofi darasani lakini akaondoka naye hadi ofisini na kuwaambia walimu wenzake kwamba mwanafunzi huyo hakufanya homework ndiyo walimu wakamchangia kumpiga.
Hali ya mwanafunzi bado siyo nzuri kwani aliumia sana sehemu ya kichwa na machoni. Tayari Waziri Mwigulu Nchemba ameagiza walimu hao kuchukuliwa hatua za kisheria.
========
Mnamo Tarehe 28.9.2016, mwanafunzi aitwaye Sebastian Chinguku wa form 3A Mbeya day sec school aishie Uyole alipigwa na walimu watatu, Mwl Frank Msigwa, John Deo UDSM na Sanke Gwamaka wa Nyerere Memorial, wote wakiwa mafunzo.
Mwl Frank alitoa assignment ya Kingereza na baadhi ya wanafunzi hawakufanya akiwepo Sebastian hakufanya, darasani mwl alimpiga kofi kijana na kijana akahoji kwanini anampiga wakashikana koo, ndio walimu wakamchukua na kumpeleka staff room na kuanza kumpiga vile. Tangu tar 29. September mwanafunzi hakuonekana shuleni. Na mwl E.H wa Iringa University ndio aliyekuwa akisema mwacheni mtamuumiza. Ndio aliyechukua video.
Hao walimu wote hawapo wameondoka kwenda kwenye vyuo vyao. POLISI wanaendelea kuwahoji uongozi wa Mbeya Day Sec School na Mwanafunzi aliyeumizwa ikiwepo kumpeleka hospitali. Nimeelekeza vyombo vya dola Dar wawatafute chuoni kwao hao walimu kuhusiana na shambulio hilo kwa mwanafunzi huyo.
MWIGULU Nchemba, W MNN
MKUU WA MKOA WA MBEYA AZUNGUMZIA TUKIO HILO
Taarifa ya awali ya tukio la kupigwa mwanafunzi wa Mbeya Day ndg Sebastian Chingulu.
Tukio lilianza tarehe 26/9/2016 mwalimu Frank Msigwa mwanafunzi kwa vitendo toka chuo kikuu cha Dar Es salaam kutoa assignment ya soma la kingereza kwa wanafunzi wa kidate cha Tatu.
Baada ya kusahihisha aligundua kuwa kuna baadhi ya wanafunzi hawakufanya NA tarehe 28/9/2016 alikwenda darasani NA kutoa adhabu NA alianza kwa kuwapa adhabu ya push up, kupiga magoti NA baadae viboko 2 katika utekelezaji mwanafunzi Sebastian Chingulu alikataa kufanya kutokana NA kuumwa NA goti.
Baada ya kukataa adhabu mwl Frank Msigwa NA wenzake 2 John Deo NA sanke Gwamaka walimpeleka ofisini NA kuanza kumshambulia kwa kipigo NA baada ya tukio hilo walitoeka na wakati wanamshambulia mwalimu mwingine aliwasihi wasimpige NA alirekodi tukio hilo.
Serikali ya mkoa inaendelea kuwashikilia walimu NA mwalimu mkuu kwa mahojiano, kupata maelezo ya wanafunzi waliopata adhabu NA mwanafunzi aliyepigwa.
Nawahakikishia serikali itawasaka popote walipo walimu hawa waliofanya tukio hili NA kufikishwa ktk vyombo vya dola NA sheria.
Aidha mwanafunzi aliyepigwa anaendelea kupimwa NA matibabu.
Hii Ni taarifa ya awali nitaendelea kutoa taarifa kwa kila hatua.
Amos G Makalla
RC Mbeya
======
Walimu waliohusika wafukuzwa Chuo, kwa habari zaidi soma=>Waziri Ndalichako awatimua Chuo walimu wa Mafunzo waliompiga mwanafunzi shule ya Kutwa Mbeya
Clip hii sijui ni shule gani lakini yaonekana ni hapa nchini kutokana na sauti ya dada inayosikika kwenye background.
Hata kama huyo kijana amekosa vipi si angepelekwa vyombo vya sheria?
Wana tofauti gani na wale wanakijiji walioua watafiti?
Sheria ifuate mkondo wake, inaumiza sana.
=======
UPDATE:
Mkuu wa shule ya Mbeya Day pamoja na baadhi ya walimu wamechukuliwa na jeshi la polis kwa mahojiano zaidi. Tukio hilo lilitokea 28. September.
Jumanne tarehe 24 mwalimu wa vitendo alitoa homework kwa kidato cha 3 A, kwa bahati mbaya mwanafunzi huyo hakuwepo, Jumatano wakati mwalimu anakusanya homework yule mwanafunzi alimwambia mwalimu kuwa jana yake hakuwepo alikuwa anaumwa.
Mwalimu alianza kumpiga makofi darasani lakini akaondoka naye hadi ofisini na kuwaambia walimu wenzake kwamba mwanafunzi huyo hakufanya homework ndiyo walimu wakamchangia kumpiga.
Hali ya mwanafunzi bado siyo nzuri kwani aliumia sana sehemu ya kichwa na machoni. Tayari Waziri Mwigulu Nchemba ameagiza walimu hao kuchukuliwa hatua za kisheria.
========
Mnamo Tarehe 28.9.2016, mwanafunzi aitwaye Sebastian Chinguku wa form 3A Mbeya day sec school aishie Uyole alipigwa na walimu watatu, Mwl Frank Msigwa, John Deo UDSM na Sanke Gwamaka wa Nyerere Memorial, wote wakiwa mafunzo.
Mwl Frank alitoa assignment ya Kingereza na baadhi ya wanafunzi hawakufanya akiwepo Sebastian hakufanya, darasani mwl alimpiga kofi kijana na kijana akahoji kwanini anampiga wakashikana koo, ndio walimu wakamchukua na kumpeleka staff room na kuanza kumpiga vile. Tangu tar 29. September mwanafunzi hakuonekana shuleni. Na mwl E.H wa Iringa University ndio aliyekuwa akisema mwacheni mtamuumiza. Ndio aliyechukua video.
Hao walimu wote hawapo wameondoka kwenda kwenye vyuo vyao. POLISI wanaendelea kuwahoji uongozi wa Mbeya Day Sec School na Mwanafunzi aliyeumizwa ikiwepo kumpeleka hospitali. Nimeelekeza vyombo vya dola Dar wawatafute chuoni kwao hao walimu kuhusiana na shambulio hilo kwa mwanafunzi huyo.
MWIGULU Nchemba, W MNN
MKUU WA MKOA WA MBEYA AZUNGUMZIA TUKIO HILO
Taarifa ya awali ya tukio la kupigwa mwanafunzi wa Mbeya Day ndg Sebastian Chingulu.
Tukio lilianza tarehe 26/9/2016 mwalimu Frank Msigwa mwanafunzi kwa vitendo toka chuo kikuu cha Dar Es salaam kutoa assignment ya soma la kingereza kwa wanafunzi wa kidate cha Tatu.
Baada ya kusahihisha aligundua kuwa kuna baadhi ya wanafunzi hawakufanya NA tarehe 28/9/2016 alikwenda darasani NA kutoa adhabu NA alianza kwa kuwapa adhabu ya push up, kupiga magoti NA baadae viboko 2 katika utekelezaji mwanafunzi Sebastian Chingulu alikataa kufanya kutokana NA kuumwa NA goti.
Baada ya kukataa adhabu mwl Frank Msigwa NA wenzake 2 John Deo NA sanke Gwamaka walimpeleka ofisini NA kuanza kumshambulia kwa kipigo NA baada ya tukio hilo walitoeka na wakati wanamshambulia mwalimu mwingine aliwasihi wasimpige NA alirekodi tukio hilo.
Serikali ya mkoa inaendelea kuwashikilia walimu NA mwalimu mkuu kwa mahojiano, kupata maelezo ya wanafunzi waliopata adhabu NA mwanafunzi aliyepigwa.
Nawahakikishia serikali itawasaka popote walipo walimu hawa waliofanya tukio hili NA kufikishwa ktk vyombo vya dola NA sheria.
Aidha mwanafunzi aliyepigwa anaendelea kupimwa NA matibabu.
Hii Ni taarifa ya awali nitaendelea kutoa taarifa kwa kila hatua.
Amos G Makalla
RC Mbeya
======
Walimu waliohusika wafukuzwa Chuo, kwa habari zaidi soma=>Waziri Ndalichako awatimua Chuo walimu wa Mafunzo waliompiga mwanafunzi shule ya Kutwa Mbeya