MBEYA: Walimu warekodiwa Video, wakimfanyia unyama Mwanafunzi

MBEYA: Walimu warekodiwa Video, wakimfanyia unyama Mwanafunzi

Inkoskaz

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2010
Posts
6,360
Reaction score
2,389
Wadau,

Clip hii sijui ni shule gani lakini yaonekana ni hapa nchini kutokana na sauti ya dada inayosikika kwenye background.

Hata kama huyo kijana amekosa vipi si angepelekwa vyombo vya sheria?

Wana tofauti gani na wale wanakijiji walioua watafiti?

Sheria ifuate mkondo wake, inaumiza sana.

=======

UPDATE:

Mkuu wa shule ya Mbeya Day pamoja na baadhi ya walimu wamechukuliwa na jeshi la polis kwa mahojiano zaidi. Tukio hilo lilitokea 28. September.

Jumanne tarehe 24 mwalimu wa vitendo alitoa homework kwa kidato cha 3 A, kwa bahati mbaya mwanafunzi huyo hakuwepo, Jumatano wakati mwalimu anakusanya homework yule mwanafunzi alimwambia mwalimu kuwa jana yake hakuwepo alikuwa anaumwa.

Mwalimu alianza kumpiga makofi darasani lakini akaondoka naye hadi ofisini na kuwaambia walimu wenzake kwamba mwanafunzi huyo hakufanya homework ndiyo walimu wakamchangia kumpiga.

Hali ya mwanafunzi bado siyo nzuri kwani aliumia sana sehemu ya kichwa na machoni. Tayari Waziri Mwigulu Nchemba ameagiza walimu hao kuchukuliwa hatua za kisheria.

========

Mnamo Tarehe 28.9.2016, mwanafunzi aitwaye Sebastian Chinguku wa form 3A Mbeya day sec school aishie Uyole alipigwa na walimu watatu, Mwl Frank Msigwa, John Deo UDSM na Sanke Gwamaka wa Nyerere Memorial, wote wakiwa mafunzo.


Mwl Frank alitoa assignment ya Kingereza na baadhi ya wanafunzi hawakufanya akiwepo Sebastian hakufanya, darasani mwl alimpiga kofi kijana na kijana akahoji kwanini anampiga wakashikana koo, ndio walimu wakamchukua na kumpeleka staff room na kuanza kumpiga vile. Tangu tar 29. September mwanafunzi hakuonekana shuleni. Na mwl E.H wa Iringa University ndio aliyekuwa akisema mwacheni mtamuumiza. Ndio aliyechukua video.

Hao walimu wote hawapo wameondoka kwenda kwenye vyuo vyao. POLISI wanaendelea kuwahoji uongozi wa Mbeya Day Sec School na Mwanafunzi aliyeumizwa ikiwepo kumpeleka hospitali. Nimeelekeza vyombo vya dola Dar wawatafute chuoni kwao hao walimu kuhusiana na shambulio hilo kwa mwanafunzi huyo.

MWIGULU Nchemba, W MNN




MKUU WA MKOA WA MBEYA AZUNGUMZIA TUKIO HILO




Taarifa ya awali ya tukio la kupigwa mwanafunzi wa Mbeya Day ndg Sebastian Chingulu.

Tukio lilianza tarehe 26/9/2016 mwalimu Frank Msigwa mwanafunzi kwa vitendo toka chuo kikuu cha Dar Es salaam kutoa assignment ya soma la kingereza kwa wanafunzi wa kidate cha Tatu.

Baada ya kusahihisha aligundua kuwa kuna baadhi ya wanafunzi hawakufanya NA tarehe 28/9/2016 alikwenda darasani NA kutoa adhabu NA alianza kwa kuwapa adhabu ya push up, kupiga magoti NA baadae viboko 2 katika utekelezaji mwanafunzi Sebastian Chingulu alikataa kufanya kutokana NA kuumwa NA goti.

Baada ya kukataa adhabu mwl Frank Msigwa NA wenzake 2 John Deo NA sanke Gwamaka walimpeleka ofisini NA kuanza kumshambulia kwa kipigo NA baada ya tukio hilo walitoeka na wakati wanamshambulia mwalimu mwingine aliwasihi wasimpige NA alirekodi tukio hilo.

Serikali ya mkoa inaendelea kuwashikilia walimu NA mwalimu mkuu kwa mahojiano, kupata maelezo ya wanafunzi waliopata adhabu NA mwanafunzi aliyepigwa.

Nawahakikishia serikali itawasaka popote walipo walimu hawa waliofanya tukio hili NA kufikishwa ktk vyombo vya dola NA sheria.

Aidha mwanafunzi aliyepigwa anaendelea kupimwa NA matibabu.

Hii Ni taarifa ya awali nitaendelea kutoa taarifa kwa kila hatua.

Amos G Makalla
RC Mbeya

======

Walimu waliohusika wafukuzwa Chuo, kwa habari zaidi soma=>Waziri Ndalichako awatimua Chuo walimu wa Mafunzo waliompiga mwanafunzi shule ya Kutwa Mbeya
 
Wakuu katika pitapita zangu huko kwenye makundi ya WhatsApp nimekutana na video inayowaonyesha Waalimu wakimuadhibu kijana wa kiume katika njia ya kikatili sana.

Kiukweli aina hii ya adhabu si sawa ndugu waalimu kuna wazazi wengine mtaishia kugawana majengo ya serikali wewe mwalimu unaelekea hospitali na mzazi anaelekea kituo cha polisi.

 
Halafu unataka huyo kijana wa kayumba akiwa mkubwa awe na akili na mafanikio kama mo dewji aliyesoma IST ambaye adhabu yake ilikuwa kula keki wakati huyu anakula makofi....

Akitoka hapo anaingia udsm huyo kijana anakula mabomu ya maaskari kwenye migomoooooo kisha anaajiriwa halmashauri anapigwa mikwara na mkuu wa wilaya...ha ha ha mo dewji katoka zake ist chuo kapiga zake georgetown....kweli binadamu hatupo sawa japo wanasema tupo sawa
 
Wakuu katika pitapita zangu huko kwenye makundi ya WhatsApp nimekutana na video inayowaonyesha Waalimu wakimuadhibu kijana wa kiume katika njia ya kikatili sana.

Kiukweli aina hii ya adhabu si sawa ndugu waalimu kuna wazazi wengine mtaishia kugawana majengo ya serikali wewe mwalimu unaelekea hospitali na mzazi anaelekea kituo cha polisi.


Uwiii Polisi njooni haraka!!
 
Wakuu katika pitapita zangu huko kwenye makundi ya WhatsApp nimekutana na video inayowaonyesha Waalimu wakimuadhibu kijana wa kiume katika njia ya kikatili sana.

Kiukweli aina hii ya adhabu si sawa ndugu waalimu kuna wazazi wengine mtaishia kugawana majengo ya serikali wewe mwalimu unaelekea hospitali na mzazi anaelekea kituo cha polisi.


Ni shule gani hiyo? Mzazi wa huyo mwanafunzi akiwatokea na panga hao walimu atakuwa amekosea? Hasa yule mpigaji?
 
Wakuu katika pitapita zangu huko kwenye makundi ya WhatsApp nimekutana na video inayowaonyesha Waalimu wakimuadhibu kijana wa kiume katika njia ya kikatili sana.

Kiukweli aina hii ya adhabu si sawa ndugu waalimu kuna wazazi wengine mtaishia kugawana majengo ya serikali wewe mwalimu unaelekea hospitali na mzazi anaelekea kituo cha polisi.




Hawa wanatakiwa muda huu wako kitu cha Polisi tena kwa hiari yao! Upuuzi wa aina gani huu. Yaani anamzibua kijana wa watu masikio kama mnyama. Wazazi wengine amkeni watoto wanatendewa ndivyo sivyo. adhabu gani hiyo ni imani yangu yaliyomkuta Polisi wa Zenji na hawa walimu wiki haipiti nao wanashughulikiwa
 
Back
Top Bottom