Mbeya waapa kumkata Lowassa kwa mara ya pili

Mbeya waapa kumkata Lowassa kwa mara ya pili

Jang Bo Go

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2011
Posts
854
Reaction score
253
Katika pitapita zangu huku mitaani nimekutana na jambo jipya kabisa. Nimekuta watu wakijadiliana jinsi Lowasa alivyohujumu maendeleo ya mkoa huo alivyokua waziri mkuu.

Wananchi hao wanadai Lowasa kwa makusudi kabisa alitaka ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe uzidi kuchelewa au kufa kabisa.

Wanaendelea kwa kudai kuwa bila Mwandosya kusimama kidete basi ujenzi wa uwanja wa Songwe ungeishia njiani.

Wanadai Lowasa hana mapenzi ya dhati na jiji hilo linalokua kwa kasi hivyo wamejidhatiti kumkata kwa mara nyingine na kura zao wanadai watazipeleka kwa Magufuli.

Kwa anaefahamu, je kuna uhusiano wowote kuhusu kusua sua kwa ujenzi uwanja wa Songwe na Lowasa?

Mjumbe hauawi.
 
Katika pitapita zangu huku mitaani nimekutana na jambo jipya kabisa. Nimekuta watu wakijadiliana jinsi Lowasa alivyohujumu maendeleo ya mkoa huo alivyokua waziri mkuu.

Wananchi hao wanadai Lowasa kwa makusudi kabisa alitaka ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe uzidi kuchelewa au kufa kabisa.

Wanaendelea kwa kudai kuwa bila Mwandosya kusimama kidete basi ujenzi wa uwanja wa Songwe ungeishia njiani.

Wanadai Lowasa hana mapenzi ya dhati na jiji hilo linalokua kwa kasi hivyo wamejidhatiti kumkata kwa mara nyingine na kura zao wanadai watazipeleka kwa Magufuli.

Kwa anaefahamu, je kuna uhusiano wowote kuhusu kusua sua kwa ujenzi uwanja wa Songwe na Lowasa?

Mjumbe hauawi.

Kama ni kweli, hayo yote yalikuwa yakifanyika chini ya utawala wa CCM au chama gani!
 
Vijiwe vya wanywa kahawa wa ma ccm ndo wanaongea hivyo
 
Labda Mbeya ya ndoto za mchana, muulize huyo Mwandosya kilichomsibu mwaka 2010 pale jijini ndo utajua hao waliokuwa wanaongea si determinant ya maamuzi ya watu wa Mbeya jiji.
 
Mimi nipo Mbeya na ninafuatilia kwa karibu matukio ya uchaguzi.Lowassa anakubalika Mbeya kwa kiasi kikubwa tangu alipokuwa CCM.Alipohamia UKAWA ndo kajivunia ushindi kabisa.Hakuna kitu kama hicho ulichoandika.Pole sana.
 
Hauna shughuli ya maana ya kufanya zaidi ya kupitapita mtaani?Mbeya unayoiongelea itakuwa ya kusadikika ila yenyewe halisi,Magufuli kaingia leo toka asubuhi lakini wengi wetu habari tumezipata mtandaoni hivi punde.
Siku kaja Lowassa taarifa zilikuwa zinajitangaza.
 
Nawafananisha UKAWA na watu wa SODOMA na GOMORRAH,hawa watu ni wagumu sana kuelewa vitu....
 
hili liko wazi,,,, uwanja wa ndege wa SONGWE ulihujumiwa na kama si MWANDOSYA na MWAKYEMBE huo uwanja wa ndege usingemalizika na walipambana sana bungeni hao the BIG FOUR,,, pia chuo kikuu cha MUST tusingekisikia sasa maana MANDELA UNIVERSITY haikuwa kipaumbela ila kipaumbele ilikuwa MUST lakini bwana mkubwa alishinikiza ikajengwa MANDELA UNIVERSITY,, hili liko wazi tena lilisahaulika kwa watanzania hasa wakazi wa nyanda za juu kusini maana ni kawaida ya wabongo kuwa wasahaulifu,, ila hii ni silaha itakayommaliza EL nyanda za juu kusini kama itatumiwa vizuri...
 
" Mtanzania atakayemchagua LOWASSA anatakiwa kwenda kupimwa akili" by MCHUNGAJI MSIGWA.

nafikili mtakuwa mmesahau hiyo nukuu toka kwa mbunge kipenzi kwa wana CDM..
 
Hivi kweli niache kumchagua DK MAGUFURI niaende kumchagua LOWASSA ambaye nilimkataa toka akiwa CCM,, kiukweli sioni haja ya kumpigia kura LOWASSA na kumuacha MAGUFURI kwa kila aliye mwelevu na awezaye kufikili.

DR MAGUFURI NDIYE ATUFAAYE KWA SASA,, LABDA MTULETEE MWINGINE TENA 2025 na CCM walete nao mwingine atakayekuwa kilaza na wa UKAWA akawa JEMBE kama MAGUFURI vile..

 
Acha uongo wako baraza la mawaziri likipitisha hakuna Wa kukataa usipotoshe watu au sema magufuri ndio kaujenga maana ccm kwa uongo
 
Si atakuja kwenye kampeni ndo tutajua wamemkataa au vii
 
Katika pitapita zangu huku mitaani nimekutana na jambo jipya kabisa. Nimekuta watu wakijadiliana jinsi Lowasa alivyohujumu maendeleo ya mkoa huo alivyokua waziri mkuu.

Wananchi hao wanadai Lowasa kwa makusudi kabisa alitaka ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe uzidi kuchelewa au kufa kabisa.

Wanaendelea kwa kudai kuwa bila Mwandosya kusimama kidete basi ujenzi wa uwanja wa Songwe ungeishia njiani.

Wanadai Lowasa hana mapenzi ya dhati na jiji hilo linalokua kwa kasi hivyo wamejidhatiti kumkata kwa mara nyingine na kura zao wanadai watazipeleka kwa Magufuli.

Kwa anaefahamu, je kuna uhusiano wowote kuhusu kusua sua kwa ujenzi uwanja wa Songwe na Lowasa?

Mjumbe hauawi.

Si Mbeya tu..ila ifikapo 25 Oct watanzania wataongea lugha moja na CCM
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom