johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,933
- 141,902
Mwekezaji mzawa katika sekta ya mifugo huko Ihefu mkoani Mbeya amekutwa amejinyonga kwenye mti porini baada ya ng'ombe wake 50 kukamatwa na askari wa Idara ya Maliasili.
Baba wa marehemu amesema mwanae amejinyonga kwa kuhofia ufukara na umaskini baada ya kunyang'anywa ng'ombe wake wote ambao wamehifadhiwa ofisi ya wilaya.
Naye mkuu wa mkoa wa Mbeya mh Chalamila amekiri kupata taarifa za tukio hilo na ametaka Serikali isihusishwe kwa namna yoyote ile na uamuzi wa mwekezaji huo kujinyonga kwani huo ni uamuzi wake binafsi hakuna aliyemshinikiza.
Chanzo: ITV habari
Maendeleo hayana vyama!
Baba wa marehemu amesema mwanae amejinyonga kwa kuhofia ufukara na umaskini baada ya kunyang'anywa ng'ombe wake wote ambao wamehifadhiwa ofisi ya wilaya.
Naye mkuu wa mkoa wa Mbeya mh Chalamila amekiri kupata taarifa za tukio hilo na ametaka Serikali isihusishwe kwa namna yoyote ile na uamuzi wa mwekezaji huo kujinyonga kwani huo ni uamuzi wake binafsi hakuna aliyemshinikiza.
Chanzo: ITV habari
Maendeleo hayana vyama!