kandamatope
JF-Expert Member
- May 19, 2018
- 589
- 627
Asilazwe yeye nani?Acha upumbav,kama ni kuhojiwa kwanini alazwe lupango?Washenzi kabisa hawa polisi
Sent using Jamii Forums mobile app
Asilazwe yeye nani?Acha upumbav,kama ni kuhojiwa kwanini alazwe lupango?Washenzi kabisa hawa polisi
Hajalala sasa,pasuka!!!!
I know , but you must understand that from Mbeya to Katavi was Demotion , Kwa mtu wa mjini kama pedesheee Makalla kumtupa Katavi ( njia panda ya kuzimu ) ilikuwa ni kama adhabu
Demotion kama angekuwa mkuu wa wilaya lakini amebaki na cheo chake kile kile,kweli utasema demotion mkuu?I know , but you must understand that from Mbeya to Katavi was Demotion , Kwa mtu wa mjini kama pedesheee Makalla kumtupa Katavi ( njia panda ya kuzimu ) ilikuwa ni kama adhabu
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
KAULI YA KULAANI MBUNGE SUGU KUSHIKILIWA, KUNYIMWA DHAMANA KWA KUTIMIZA MAJUKUMU YAKE*
Leo Alhamis, Februari 21, 2019, saa moja asubuhi, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Sugu', aliitikia wito wa Jeshi la Polisi, aliopewa jana kupitia kwa Kamanda wa Polisi Mkoa (RPC) wa Mbeya na Mkuu wa Upelelezi Makosa ya Jinai (RCO), wote kwa nyakati tofauti, wakimtaka kufika Kituo Kikuu cha Polisi mkoani humo kwa ajili ya mahojiano.
Hadi jioni hii, tunapolazimika kutoa taarifa Jeshi la Polisi mkoani Mbeya limeendelea kumshikilia chini ya ulinzi Mbunge huyo na baada ya kwenda naye eneo la Ikuti jijini humo, ambapo inadaiwa alitoa maneno ya uchochezi siku ya Jumamosi, Februari 16, mwaka huu alipokuwa akijibu malalamiko ya kero mbalimbali za wananchi wa jimboni kwake, polisi wamemrejesha Mbunge Mbilinyi Kituo Kikuu cha Polisi na amenyimwa dhamana bila kuwepo kwa taarifa yoyote ya kunyimwa haki yake hiyo ya msingi kwa mujibu wa sheria za nchi.
Chadema kinalaanii vikali kitendo cha Mbunge kushikiliwa, kuhojiwa na sasa kunyimwa dhamana kwa kuwaahidi wananchi wake kuwa atakwenda kuhoji bungeni suala la Wamachinga kuuziwa vitambulisho, ambao ni wajibu wake akiwa mwakilishi wa wananchi.
Chama kinafuatilia jambo hili kwa ukaribu kupitia kwa wanasheria wa wake, kikilitaka Jeshi la Polisi mkoani Mbeya kumfikisha Mbunge huyo mahakamani haraka iwezekanavyo kwa mujibu wa taratibu za nchi ili apate haki yake ya dhamana.
Kwa taarifa tulizonazo, mahojiano aliyofanyiwa yalijikita kutaka kujua tafsiri ya maneno aliyoyatumia Mbunge huyo siku hiyo ya Februari 16, ambapo akisikiliza malalamiko ya wapiga kura wake, baada ya kutoa msaada wa saruji, nondo na mabati, katika Shule ya Ikuti, aliwaahidi wananchi kuwa atakwenda kuhoji bungeni suala la vitambulisho wanavyouziwa 'Wamachinga' kwa bei ya shilingi 20,000/= ili kujua msingi wake na kwanini limeanza kufanyiwa kazi bila kuwashirikisha wadau ili kuwa na uelewa wa pamoja.
Mbunge Mbilinyi alitoa majibu hayo baada ya wananchi hao, hususan wafanyabiashara ndogondogo wanaojihusisha na uuzaji wa mboga kumlalamikia usumbufu wanaoupata kwa kulazimishwa na mamlala za kiserikali mkoani humo kununua vitambulisho vya wafanyabiashara ndogondogo kwa bei hiyo wasiyoweza kumudu kutokana na udogo wa mitaji, biashara yao na hata mapato wanayopata. Walihoji mantiki iliyotumika kuwapangia wauza mboga wanunue vitambulisho hivyo kwa bei hiyo moja, sawasawa na wafanyabiashara ndogondogo wengine wenye mitaji mikubwa kwa kuwalinganisha na wauza mbogamboga.
Imetolewa leo Alhamis, Februari 21, 2019 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
========
UPDATES:
Mbunge Joseph Mbilinyi (Sugu)CHADEMA, Muda wa saa 01: 03 PM, Amepewa dhamana kwa masharti ya kudhaminiwa na mtu mmoja ambaye amesaini bond ya shilingi Milioni 5 na atatakiwa kufika polisi kesho saa nne Kamili asubuhi.
Hajachoma ila amehamasisha watu waliouziwa vitambulisho wavichome motoAcha upumbav,weka ushahidi hapa kama amevichoma!Nyie watu ni mamburula sana!
Kama natuhumiwa kuvunja sheria sina tatizo kukamatwa na kuachiwa ikithibitika sijafanya kosa lolote afu mimi siyo Hopeless you fcukin CUNT.Kwahiyo na wewe wakukamate tu kutekeleza haki yako kesho kutwa mahakama ikuachie! Hopeless.
Hivi polisi wapo kwaajili ya wapinzani pekee?Siyo mara ya kwanza Sugu kukamatwa,Tanzania ni nchi ya Demokrasia na haki,kama hajatenda makosa mahakama itampa haki yake.
Mimi siyo mwanasiasa mkuu,hilo swali waulizwe polisi.Hivi polisi wapo kwaajili ya wapinzani pekee?
Ccm huwa hawakosei?
Wao ni malaika sio?
Cc Mnyeti.
Sent using Jamii Forums mobile app
una kichwa kigumu sana !Demotion kama angekuwa mkuu wa wilaya lakini amebaki na cheo chake kile kile,kweli utasema demotion mkuu?
Sent using Jamii Forums mobile app