Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 60
- 1,237
Ndugu zangu majira ya asubuhi leo 3rd November 2023 tukiwa katika mkutano wetu na waandishi wa habari tulivamiwa na kukamatwa na askari kadhaa wakiongozwa na Kamishina msaidizi wa jeshi la polisi kutoka ofisi ya RPC Mbeya. Askari hao walitukamata sisi pamoja na waandishi wa habari tuliokuwa nao katika press conference.
Masaa matano baada ya kushikiliwa tuliitwa ofisi kwa RPC kwamba tulikamatwa ili tupewe barua ya inayotuzuia kuandamana kwa amani tarehe 9 Nov 2023.
RPC alidai kuwa OCD hajui tunapopatikana ili atuletee barua ya majibu ya maandamano hayo hivyo ikalazimika tukamatwe ili tupewe barua ijapo OCD huyo alikuwepo wakati wa ukamataji wetu.
Kwa sasa tupo tunaandaa barua ya rufaa kwenda kwa waziri wa mambo ya ndani kupinga zuio haram la OCD na baada ya hapo tutatoa tamko rasmi.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Masaa matano baada ya kushikiliwa tuliitwa ofisi kwa RPC kwamba tulikamatwa ili tupewe barua ya inayotuzuia kuandamana kwa amani tarehe 9 Nov 2023.
RPC alidai kuwa OCD hajui tunapopatikana ili atuletee barua ya majibu ya maandamano hayo hivyo ikalazimika tukamatwe ili tupewe barua ijapo OCD huyo alikuwepo wakati wa ukamataji wetu.
Kwa sasa tupo tunaandaa barua ya rufaa kwenda kwa waziri wa mambo ya ndani kupinga zuio haram la OCD na baada ya hapo tutatoa tamko rasmi.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.