Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 71,360
- 127,739
Wanachokifanya CCM wanawapa nguvu Vyama vingine kama hivyo vya Nccr,CUF ili Chadema ikigoma mpk tume huru ya uchaguzi ipatikane then CUF,Nccr,Act wataendelea na uchaguzi kama kawaida na kupewa vijimbo viwili vitatu then chadema wakilalamika huko kwny jumuiya za kimataifa CCM itasema mbona wenzao wameshiriki uchaguzi fresh tu.
Inabidi kui counter attack hii strategy ya CCM kwa mbinu za kimedani.
Kwanza sidhani kwamba cdm wanadai tume huru kwa kuwa jumuiya ya kimataifa itahoji. Ila haya ni madai halali tena ya muda mrefu. Hata ccm wanajua fika muundo wa tume hii una walakini, ila kwakuwa msukumo wa kuidai ni mdogo, na baadhi ya vyama vinatumika kuhadaa umma, basi ccm wanaendelea kutumia mwanya huo. Iwapo tume hii itadaiwa kwa nguvu zote haitaepukika bila kujali hivyo vyama kama vitatumika. Ni bora cdm wasishiriki huo uchaguzi kwa kuidai hiyo tume huru ya uchaguzi, miaka mitano ni nini, mbona CUF. ya Maalim ikisusia uchaguzi uliobakwa na sasa muda umeisha bila ccm huko Zanzibar kuwa kwenye uhakika wa kushinda uchaguzi huu? Ni vyema kusimamia madai halali bila kuyumba kwa hizo trick za vyama visivyo na nguvu.