MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 793
MBATIA aliapa bungeni kwamba Waziri wa Elimu atakapowakilishwa mtaala wa elimu atajiuzulu ubunge kwani haupo tangu tupate uhuru.
Mtaala wa elimu umewakilishwa na kuundiwa Tume ya wabunge 6 itakayodhibitisha mtaala huo chini ya mama Magreth Sitta.
Tugemee nini kama itathibitishwa kwamba mtaala huo upo???
My Take:
Nilimsikia MBATIA kwa kinywa chake akitoa ahidi na kuapa kupitia TBC live kutoka bungeni kwamba ataachia ngazi.
Mdomo nyumba ya maneno. Huwezi kuisukuma gari ukiwa ndani ya gari.
Mbatia hilo unalo timiza ahadi yako endapo itathibitishwa kwamba ulilidanganya bunge na Watanzania. Kama atagoma kujiuzulu basi bunge litumie busara kumfukuza ubunge ili ahadi yake itimie.
huo sasa ni mjadala mwengine mpya.hata kama hiyo mitaala imewasilishwa haina tija kwa elimu ya sasa
MBATIA aliapa bungeni kwamba Waziri wa Elimu atakapowakilishwa mtaala wa elimu atajiuzulu ubunge kwani haupo tangu tupate uhuru.
Mtaala wa elimu umewakilishwa na kuundiwa Tume ya wabunge 6 itakayodhibitisha mtaala huo chini ya mama Magreth Sitta.
Tugemee nini kama itathibitishwa kwamba mtaala huo upo???
My Take:
Nilimsikia MBATIA kwa kinywa chake akitoa ahidi na kuapa kupitia TBC live kutoka bungeni kwamba ataachia ngazi.
Mdomo nyumba ya maneno. Huwezi kuisukuma gari ukiwa ndani ya gari.
Mbatia hilo unalo timiza ahadi yako endapo itathibitishwa kwamba ulilidanganya bunge na Watanzania. Kama atagoma kujiuzulu basi bunge litumie busara kumfukuza ubunge ili ahadi yake itimie.
unatakiwa useme utajiuzulu? Na sio atafukuzwa. Hata hivyo hapa ndo tutajua ni hekaheka za kutaka sifa au uzalendo.mbatia aliapa bungeni kwamba waziri wa elimu atakapowakilishwa mtaala wa elimu atajiuzulu ubunge kwani haupo tangu tupate uhuru.
Mtaala wa elimu umewakilishwa na kuundiwa tume ya wabunge 6 itakayodhibitisha mtaala huo chini ya mama magreth sitta.
Tugemee nini kama itathibitishwa kwamba mtaala huo upo???
My take:
Nilimsikia mbatia kwa kinywa chake akitoa ahidi na kuapa kupitia tbc live kutoka bungeni kwamba ataachia ngazi.
Mdomo nyumba ya maneno. Huwezi kuisukuma gari ukiwa ndani ya gari.
Mbatia hilo unalo timiza ahadi yako endapo itathibitishwa kwamba ulilidanganya bunge na watanzania. Kama atagoma kujiuzulu basi bunge litumie busara kumfukuza ubunge ili ahadi yake itimie.
Someni makala ya dr. Mkumbo gazeti la raia mwema la leo muone tanzania ilivyo na viongozi uchwara. Waziri kawambwa ni kilaza,wabunge pia ni vilaza tu. Suala hili kwetu sisi wataalam ni dogo sana lakini limekuzwa na ukilaza na uvivu wa kufikiri wa wabunge na wafanya kazi wa wizara ya elimu. NASISITIZA KWAMBA TANZANIA HAKUNA DOCUMENTS ZINAZOITWA MITAALA. Kama kuna kitu kilichoandikwa juu yake mtaala either wa shule ya msingi au secondary kilichopelekwa bungeni,ninasikitika kuona kwamba wataalam wa mitaala wanalipotosha taifa. mbatia alipaswa kupewa elimu kuhusu maana ya mitaala
bado Mbatia yuko sahihi; muda aliotaka Mtaala wa Elimu uwasilishwe Bungeni aukuonekana; kwa maana haukuwepo kabisa tangu awali; sasa huu uliowasilishwa juzi kuna uwezekano mkubwa umeandaliwa fastafasta ili kuliondolewa Taifa aibu.
hebu tusaidie wewe sasa; mitaala ni nini?someni makala ya dr. Mkumbo gazeti la raia mwema la leo muone tanzania ilivyo na viongozi uchwara. Waziri kawambwa ni kilaza,wabunge pia ni vilaza tu. Suala hili kwetu sisi wataalam ni dogo sana lakini limekuzwa na ukilaza na uvivu wa kufikiri wa wabunge na wafanya kazi wa wizara ya elimu. Nasisitiza kwamba tanzania hakuna documents zinazoitwa mitaala. Kama kuna kitu kilichoandikwa juu yake mtaala either wa shule ya msingi au secondary kilichopelekwa bungeni,ninasikitika kuona kwamba wataalam wa mitaala wanalipotosha taifa. Mbatia alipaswa kupewa elimu kuhusu maana ya mitaala
ndugu yangu inaelekea hujui maana ya mtaala (neno sahihi mtalaa japo wengi wanaandika mtaala). nikupe mfano mmoja. muhtasari ama syllabus inatokana na mtalaa. katika shule ya msingi kuna syllabus ya kiswahili, kiingereza, hisabati, sayansi, historia, jiografia, uraia, stadi za kazi, tehama. hayo ni masomo 9. ukifanya mahesabu darasa la kwanza hadi la 7, zinahitajika syllabus 63. japo kiswahili la 1 hadi la saba huwa katika kitabu kimoja na masomo mengine ni hivyohivyo.
elimu ya chekchea nayo ina mihutasari yake. elimu ya sekondari nayo ina ya kwake. mihutasari yote inatokana na mitalaa. mitalaa ni mipana zaidi kuliko mihutasari. ndugu yangu hiyo ni kazi ya zaidi ya mwaka mzima. acha utoto kwa kusema fastafasta. mitalaa ilikuepo ila hapakua na vitabu vyake. ilikua kwenye ma files wizarani na taasisi. kinacho hitajika mashuleni ni syllabus siyo curriculum.
mbatia aligusa sehemu ambapo panahitaji utafiti wa kitaalamu siyo kisiasa. alifanya utafiti uliyohodhiwa na siasa siyo taaluma. asijiuzulu bali aombe radhi.
hata hivy, bado tuna kazi kubwa ya kuboresha elimu yetu hapa nchini huanzia sera ya elimu, mitalaa, mihutasari na vitendea kazi. nampongeza mbatia kwa hoja yake binafsi ila namsihi asifuate ushauri wa lissu. lissu atammaliza kisiasa.