Mbatia akabidhiwa Mitaala FEKI

Mbatia akabidhiwa Mitaala FEKI

George J Minja

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
289
Reaction score
203
mbatia+makinda.jpg


Mbatia amsema kuwa hakubaliani na mitalaa iliyowasilishwa ambayo ni ya elimu ya awali, msingi na sekondari.
Alisema kilichowasilishwa siyo alichokidai bungeni, mtalaa alioudai ulikuwa wa mwaka 1997 hadi mwaka 2005 wakati uliowasilishwa ni wa mwaka 1998 hadi 2008 ambao unasema ni kwa ajili ya Tanzania Bara.

"Huwezi kusema Mtalaa wa Elimu ya Sekondari ni wa Tanzania wakati huu uliopo unaonyesha ni wa Tanzania Bara wakati hata mtihani unaofanyika wa darasa la saba ni wa Tanzania.

"Kasoro nyingine ni kwamba katika vitabu vya mwongozo inatakiwa kuwa na Alama Ubora (ISBN) kwa kuidhinishwa na Bodi ya Maktaba, sasa mtalaa wa jana hauna hayo yote."
Kasoro ya tatu, Mbatia alisema alikataa muhtasari kwa kuwa haukuwa na saini ya Kamishna wa Elimu.
Alisema kuwa bado anasimamia hoja yake kuwa hakuna mitalaa ya elimu Tanzania na atasimamia hapo na atamwomba Spika suala hilo lijadiliwe na Wabunge wote kwa masilahi ya taifa, kwani mtalaa wa taifa hauwezi kutolewa kwa waraka
 
Vipi Tundu Antipas Lissu wamempa adhabu gani hao?huyu maam speaker dawa yake ni lissu tu
 
hili swala mm naona ni vyema likajadiliwa bungeni ili liwe na mapana yake watu tulielewe, kwani kuna mambo yanaitaji majb mfani ISBN waziri anaitaji kujb kama hutolewa ktk vitabu gani.nawasilisha
 
Kweli hii imedhihirisha wazi kwamba Magamba ni mabingwa wa kuchakachua! Kumbe waliyoleta haikupasishwa na haina hata ISBN! Kweli walikurupuka bila kujua kwamba wameacha mianya mingi sana ya kuweza kugundulika.

Hawa Magamba naona sasa wanacheza na elimu za watoto wetu kwa sababu wa kwao hawawapeleki kwenye hizi shule zisizo na mitaala.
 
mbatia+makinda.jpg


Mbatia amsema kuwa hakubaliani na mitalaa iliyowasilishwa ambayo ni ya elimu ya awali, msingi na sekondari.
Alisema kilichowasilishwa siyo alichokidai bungeni, mtalaa alioudai ulikuwa wa mwaka 1997 hadi mwaka 2005 wakati uliowasilishwa ni wa mwaka 1998 hadi 2008 ambao unasema ni kwa ajili ya Tanzania Bara.

“Huwezi kusema Mtalaa wa Elimu ya Sekondari ni wa Tanzania wakati huu uliopo unaonyesha ni wa Tanzania Bara wakati hata mtihani unaofanyika wa darasa la saba ni wa Tanzania.

“Kasoro nyingine ni kwamba katika vitabu vya mwongozo inatakiwa kuwa na Alama Ubora (ISBN) kwa kuidhinishwa na Bodi ya Maktaba, sasa mtalaa wa jana hauna hayo yote.”
Kasoro ya tatu, Mbatia alisema alikataa muhtasari kwa kuwa haukuwa na saini ya Kamishna wa Elimu.
Alisema kuwa bado anasimamia hoja yake kuwa hakuna mitalaa ya elimu Tanzania na atasimamia hapo na atamwomba Spika suala hilo lijadiliwe na Wabunge wote kwa masilahi ya taifa, kwani mtalaa wa taifa hauwezi kutolewa kwa waraka
Nimeshiriki kuandaa mitaa mingi, siami hivi tuvijatabu tunaweza kuwa mitaala ya chekechea mpaka form six, haswa kwa CEBET system. Hataaaaaa. Kitabu hicho kimoja kinaweza kuwa mtaala wa chekechea, na cha pili labda kwa darasa la kwanza. Nahisi tunachanganya kati ya Curriculum na Syllabus. Watanzania tuwe makini na hili suala.

Situation analysis (though this may a separate document)
Principal learning out come

Sub enabling outcome
Related tasks
Assessment methods
Assessment instrument
Bench-marking of assessment criteria
Assessment criteria
Marks distribution
Description of courses
Reference materials


I find it hard to have less than forty pages for each class
Kama mnataka kuona mfano nendeni VETA au NACTE, mtaikuta. Na hifichwi kabatini, inatakiwa itumike na walimu na wakaguzi
Ohhh my Gog bless this country.
 
Hivi huyu spiker wa bunge ana watoto/mtoto?Hivi kwanini wabunge wa Ccm wanapenda kuona Taifa linaangamia?Hivi watanzania wamewakosea nini mpaka watuburuze kwa kiwango hiki?Lakini naamini siku inakuja mtakapo weka sawa akili kwa kushuhudia mkienda mahakamani kwenye machela kama Hosn Mubaraka..Huna hata aibu wewe Spiker.
 
ni feki na hii inapatikana tz tu........
 
yani kuileta hadi watu watoke nje?hivi huo si ndio uhuni?hivi kwanini tusiamini kuwa hiyo mitaala ni feki?
 
inawezekana ni draft document tu ndiyo maana waziri hakuwa na majibu mwanzoni!! Chezea Mafisadi wa CCM wewe!!
 
Hii nchi kila kitu ni Feki! Ndege ya Raisi Feki! Rada Feki!Mitaala Feki!Madaam Spika Feki! Raisi wa nchi naye........... AAH mimi nachoka sana!
 
uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii ngoja nicheke tu ccm bana itakufa
 
Kama kweli serikali amefanya hivyo, ni wazi kuwa serikali ya CCM haina nia njema kwa taifa hili. Hii hali watanzania tunapaswa kuikataa kwa nguvu zote tena bila ya woga,,,, ccm sio watu wazuri hata kidogo na hatupaswi tena kuendelea kuwachekea .

Kama hilo ni la kweli ni vema waziri wa elimu akajiuzuru, kwani nia aibu! Tena atuombe radhi kwa kutaka kuchezea akili zetu.
 
mwanasheria mkuu wa serikari 'fake', yaani yupo pale kutunga sheria za kufunika na kutetea makosa yanayofanywa na serikari, spika na naibu makinda. Haonyeshi umahiri isipokuwa ujuha.
 
ni feki maana wamekwenda kuchapa wiki iliyopita sasa wamesahau walau hata kuweka nembo ya SBN na wala kamishna hawajampata kuwagongea saini maana aliwaambia hawezi kudharirika kijinga
 
Hivi huyu spiker wa bunge ana watoto/mtoto?Hivi kwanini wabunge wa Ccm wanapenda kuona Taifa linaangamia?Hivi watanzania wamewakosea nini mpaka watuburuze kwa kiwango hiki?Lakini naamini siku inakuja mtakapo weka sawa akili kwa kushuhudia mkienda mahakamani kwenye machela kama Hosn Mubaraka..Huna hata aibu wewe Spiker.

wachawi huwa hawana watoto.
 
Jamani.....hivi Tanzania na viongozi wake wamelaaniwa na kitu gani? Hivi kweli mtaala wa elimu unachezewa kiasi hicho.....Asante Mbatia kwa kutufumbua macho na hao watawala (CCM) wanaumbuliwa na Mwenyezi Mungu kwa udhalimu wao.
 
Nimeshiriki kuandaa mitaa mingi, siami hivi tuvijatabu tunaweza kuwa mitaala ya chekechea mpaka form six, haswa kwa CEBET system. Hataaaaaa. Kitabu hicho kimoja kinaweza kuwa mtaala wa chekechea, na cha pili labda kwa darasa la kwanza. Nahisi tunachanganya kati ya Curriculum na Syllabus. Watanzania tuwe makini na hili suala.

Situation analysis (though this may a separate document)
Principal learning out come

Sub enabling outcome
Related tasks
Assessment methods
Assessment instrument
Bench-marking of assessment criteria
Assessment criteria
Marks distribution
Description of courses
Reference materials


I find it hard to have less than forty pages for each class
Kama mnataka kuona mfano nendeni VETA au NACTE, mtaikuta. Na hifichwi kabatini, inatakiwa itumike na walimu na wakaguzi
Ohhh my Gog bless this country.
 
Back
Top Bottom