Sozo_
JF-Expert Member
- Jun 12, 2022
- 2,790
- 4,958
Tut
Tutaona mengiView attachment 3348690
Aliyekuwa Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia ameshinda kesi aliyoifungua dhidi ya chama hicho, akipinga kuondolewa kwenye uongozi na kuvuliwa uanachama wake.
Mbatia aliemnguliwa madarakani kufuatia mkutano mkuu wa NCCR Mageuzi uliofanyika Septemba 24, 2022, ambapo pia ulimvua uanacama, jambo alilopinga katika shauri la madai nambari 18/2023 (Judicial Review) alilofungua Mbatia dhidi ya Bodi ya Wadhamini ya chama hicho.
Akitoa hukumu hiyo leo Mei 28, 2025, Jaji Jaji A. Kagomba wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masijala Kuu Dodoma, ametengua uamuzi wote wa Mkutano Mkuu wa NCCR-Mageuzi wa Septemba 24, 2022 uliopindua uongozi wa Mbatia na kukubaliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa.
Kwa mujibu wa hukumu hiyo Jaji Kagomba amesema hoja ya kwamba, Ndugu James Mbatia hakuwa mwanachama wa Chama cha NCCR-Mageuzi kwa sababu kadi yake ni ya mwaka 1992 wakati usajili kamili ni wa mwaka 1993; haina mantiki yoyote kwa sababu mwaka 1992 ilikuwa ni usajili wa muda wa vyama vya siasa na ndio wanachama hao waliowezesha chama kupata usajili wa kudumu hata Katiba ya NCCR-Mageuzi ni ya mwaka 1992.
Kuhusu uamuzi ya mkutano Mkuu wa Septemba 24, 2022 Jaji amesema haukumpatia haki ya msingi (Natural Justice) Mbatia ya kusikilizwa hivyo ulikiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Katiba ya chama cha NCCR-Mageuzi na sheria za vyama vya siasa.
Pia, Jaji ametengua maamuzi yote yaliyofanywa na Mkutano huo ya kumuondolea Ndugu Mbatia uanachama na Uenyekiti wa Chama, akikitaka pia chama hicho kulipa gharama zote za kesi.
Akizungumzia hukumu hiyo, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Joseph Selasini amesema wataikatia rufaaa.
“Sisi tumepokea uamuzi huo, lakini tutaukatia rufaa. Ieleweke kwamba Mbatia aliondolewa kwenyekiti na tutafanya utaratibu asirudi kwenye uenyekiti kwa kukata rufaa,” amesema Seasini.