Mbao ya mti wa mwa40

Mbao ya mti wa mwa40

muhinda

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
348
Reaction score
237
Katika pitapita zangu, nimekutana na jamaa anauza miche ya mwa40 inayotoa mbao. Yeye alinieleza kuwa mbegu hiyo ni tafofauti na ile ya mwa40 tuliozoea kwa maana kwamba mti wake unakua kwa kunyooka kwenda juu.
Anasema unachukua miaka 5 tu kukomaa kwa ajili ya mbao. Mbao zake ni soft na nyekundu and therefore inatumika kwa ajili ya furniture za nyumbani.

Kama Maelezo ya huyu bwana yapo sawa, miti hii inaweza kuwa mkombozi kwa wale wakulima wa misitu, maana mavuno ni baada ya miaka michache compared to miti mingi ya mbao tuliyoizoea.

Nimenunua kama miche 20 ya kuanzia kwanza nione maendeleo yake.
Ila sijajua soko na bei ya mbao yake zikoje

Kama kuna yeyote mwenye info/ experience zaidi kuhusu mti huu atuwekee hapa ili tujifunze zaidi.

Natangiliza Shukrani.
 
Siamini kama inawezekana mti wa mbao kama mwarobaini ukavunwa ndani ya miaka 5, ila kuna mti mmoja unaitwa mwarobaini nusu(melia azedarach) huo unakua kwa haraka sana katika ecological zone yake(kanda ya ziwa maeneo ya musoma vijijini) huu unaweza kupasua ndani ya miaka 10 nadhani ndio hiyo aina unayoisema na inanyooka lakini sio mwarobaini(neem) kama ulivyopost

ukitaka miti inayokua haraka tafuta eucalyptus inayooteshwa kwa kutumia clones(hii inaoteshwa na wakala wa mbegu za miti tanzania(TTSA) morogoro inaweza kukua kwa miaka 9 na unapasua mbao na unauza nguzo

nawasilisha
 
mwarobaini, melia azedarach na jamii zake. (mboyo)kwa kisukuma, (mburumatale) kikelewe, kijita, nijuavyo mimi miti jamii hiyo hapo juu unao kua haraka ni melia azedarach,ukiupanda sehemu nzuri utavuna baada ya miaka 8, na gogo la chini utatoa 1x8=8
 
naukiukata juu maji yataingia na gogo litaoza kwa miaka 8 utakuta nusu ya mti ktkt umeoza, na ukikaa zaidi ya hapo gogo linaoza linakuwa na tundu kubwa mpaka chini. japo kwa nje mti utaonyesha unakua na kustawi, na unaweza kupanda mizizi yake
 
miziziyake inakua haraka kuliko kupanda miche inayotokana na mbegu, kipindi cha masika fukua kwenyeshina la mti mkubwa katamzizi uache nje ukichipua ulefu wa futi 2 kata kipande kidogo cha mzizi kapde, mzizi ulio uacha nao utachipuka katatena kapande
 
so huyu jamaa alieniuzia atakuwa anavutia biashara tu, anyway ngoja niangalie iyo niliyopanda ukuaji wake.
ila nakumbuka hata Malila alishazungumzia kuhusu mbao ya mwa40
 
Last edited by a moderator:
so huyu jamaa alieniuzia atakuwa anavutia biashara tu, anyway ngoja niangalie iyo niliyopanda ukuaji wake.
ila nakumbuka hata Malila alishazungumzia kuhusu mbao ya mwa40

Ni kweli Mwarobaini unatoa mbao za fanicha nzuri. Tatizo lililopo ni aina ya mti/spishi hasa. Si kila mwarobaini unaweza kuvunwa mapema kila mahali. Ni kama Mitiki inavyosumbua watu, ni kweli inamea ukanda wa Pwani, je soil properties, au humidity au kiwango cha mvua kimewekwa wazi?

Mkuu hujasema umeotesha wapi hiyo miarobaini ya majaribio. Na mimi nielekeze nikachukue mbegu za huyo jamaa, plan ni kuotesha eka mbili mwaka huu Mkuranga. Na bei nipe kabisa nimfuate.
 
Ni kweli Mwarobaini unatoa mbao za fanicha nzuri. Tatizo lililopo ni aina ya mti/spishi hasa. Si kila mwarobaini unaweza kuvunwa mapema kila mahali. Ni kama Mitiki inavyosumbua watu, ni kweli inamea ukanda wa Pwani, je soil properties, au humidity au kiwango cha mvua kimewekwa wazi?

Mkuu hujasema umeotesha wapi hiyo miarobaini ya majaribio. Na mimi nielekeze nikachukue mbegu za huyo jamaa, plan ni kuotesha eka mbili mwaka huu Mkuranga. Na bei nipe kabisa nimfuate.

Miti nimepanda huko huko Mkuranga, nilinunua miche pale mbagala mwisho nafikiri, kuna bonde moja wanaotesha miti, ukiwa unatokea mjini wako upande wako wa kulia. Bei kwa mche no 500. Nimeotesha michache ya majaribio, nitatoa feedback
 
Miti nimepanda huko huko Mkuranga, nilinunua miche pale mbagala mwisho nafikiri, kuna bonde moja wanaotesha miti, ukiwa unatokea mjini wako upande wako wa kulia. Bei kwa mche no 500. Nimeotesha michache ya majaribio, nitatoa feedback

Si pale kabla ya kuvuka daraja kama unakwenda Kongowe? Wale madogo waongo,waliniacha hoi waliponipa bei zao, yaani mtiki unauzwa nafuu kuliko Mwarobaini, week jana nimechukua miche ya mitiki kwao pale, basi wakaanza kuniambia sifa za miti mpaka mwenyewe nikachoka mbaya. Nilijifanya sijui hata mti mmoja.
 
mwarobaini, melia azedarach na jamii zake. (mboyo)kwa kisukuma, (mburumatale) kikelewe, kijita, nijuavyo mimi miti jamii hiyo hapo juu unao kua haraka ni melia azedarach,ukiupanda sehemu nzuri utavuna baada ya miaka 8, na gogo la chini utatoa 1x8=8
Habari za Songea??
 
Back
Top Bottom