Mentor
JF-Expert Member
- Oct 14, 2008
- 20,328
- 23,879
Jumatatu asubuhi.
Saa kumi na mbili kasoro nipo kituoni Mbagala kuu...
Kinachonishangaza ni wingi wa wanafunzi waliopo hapo wakingojea magari kwenda mashuleni.
Ni wengi sana kwa kweli..wangetosha kujaza madarasa mawili hivi...hapo sijaongezea tuliokutana nao vtiuo vilivyofuata;
Njia panda, upendo, zahanati, kijichi, misheni!
Tukaanza kugombania nao magari...
Kuingia ndani nashangaa kuwaona wanasinzia huku wameshikilia chuma, wengine wamelaliana.
Nikajiuliza swali..
IWEJE HIVI? Yani mtu unatoka Mbagala kuu mpaka Posta kwenda shule tu?
Na shule yenyewe ni hizi hizi za St. Kayumba?!
Je, ni kutafuta elimu bora?
Je ni shinikizo la wazazi ama watoto wenyewe?
Je huko kote hakuna shule za kuwapeleka mpaka aende posta?
Nikajisemea kabla sujahukumu, najua kuna wadau watakua wanao uelewa labda kwanini haya yanatokea.
Naombeni mnisaidie jameni...
Halafu mwanafunzi huyohuyo unakutana naye jioni akigombania magari...
mara afukuzwe na kondakta
mara apigwe kikumbo na mkaka anayegombania kuingia pia kwenye gari awahi kujipikia matembele yake ale apumzike ajiandae hekaheka za kesho pia,
kufika kwake nyumbani mwanafunzi huyu ni saa mbili usiku.
Akifika nyumbani anakuwa na uwezo kweli wa kusoma zaidi?
au hata muda wa kukaa na kuongea na wazazi ataupata kweli?
Saa kumi na mbili kasoro nipo kituoni Mbagala kuu...
Kinachonishangaza ni wingi wa wanafunzi waliopo hapo wakingojea magari kwenda mashuleni.
Ni wengi sana kwa kweli..wangetosha kujaza madarasa mawili hivi...hapo sijaongezea tuliokutana nao vtiuo vilivyofuata;
Njia panda, upendo, zahanati, kijichi, misheni!
Tukaanza kugombania nao magari...
Kuingia ndani nashangaa kuwaona wanasinzia huku wameshikilia chuma, wengine wamelaliana.
Nikajiuliza swali..
IWEJE HIVI? Yani mtu unatoka Mbagala kuu mpaka Posta kwenda shule tu?
Na shule yenyewe ni hizi hizi za St. Kayumba?!
Je, ni kutafuta elimu bora?
Je ni shinikizo la wazazi ama watoto wenyewe?
Je huko kote hakuna shule za kuwapeleka mpaka aende posta?
Nikajisemea kabla sujahukumu, najua kuna wadau watakua wanao uelewa labda kwanini haya yanatokea.
Naombeni mnisaidie jameni...
Halafu mwanafunzi huyohuyo unakutana naye jioni akigombania magari...
mara afukuzwe na kondakta
mara apigwe kikumbo na mkaka anayegombania kuingia pia kwenye gari awahi kujipikia matembele yake ale apumzike ajiandae hekaheka za kesho pia,
kufika kwake nyumbani mwanafunzi huyu ni saa mbili usiku.
Akifika nyumbani anakuwa na uwezo kweli wa kusoma zaidi?
au hata muda wa kukaa na kuongea na wazazi ataupata kweli?