mbadala wa ndoa

Ndoa zinabadilika. Zamani, kabla dini hazijaingia, dhana ya ndoa ilikuwa tofauti sana na ilivyo sasa katika jamii nyingi za kiafrika (Tanzania ikiwemo).

Katika jamii nyingi, ndoa za wake wengi ilikuwa sio 'dhambi'. Ingawa mfumo huu ni mbaya na haukubaliki (kwa mawazo ya sasa), lakini ulikuwa unampa uhuru mwanaume kuoa atakavyo tofauti na sasa. Hivyo katika 'mji', baba (mwenye mji) alikuwa na nyumba yake na kila mke alijengewa nyumba yake na watoto wakubwa na nyumba yao (hivyo mji unakuwa na nyumba at least tatu!). Hii ilipunguza kwa kiasi kikubwa mwanaume kuwa chini ya himaya mwanamke mmoja (kama ilivyo sasa).

Jingine ni separation kati ya wanawake na wanaume. Kulikuwa hakuna kukutana kwa mara kwa mara kati ya wanawake na wanaume katika social activities kama ilivyo leo. Kumbuka hakukuwa na shule kwa maana tunayoijua leo au kazi za maofisini nk ambazo zinawakutanisha wanaume na wanawake katika njia ambayo inarahisisha sana kufanyika kwa zinaa. Kutengishwa huku kulifanya iwe vigumu kufanya zinaa kama ilivyo sasa. Kama umempenda binti route ya kumpata ilikuwa ni kuoa(hata kama ni mke wa pili au tatu) na si vinginevyo!

Nimesema hayo machache, kujaribu kuonesha kuwa huwezi kuitizama ndoa peke yake kama unataka kuleta mabadiliko. Ni lazima uangalie social system yote na mabadiliko ni lazima yawe kwenye system nzima. Mimi naamini mabadiliko haya yanatokea yenyewe taratibu kadri muda na driving factors zote kwenye social system zinavyobadilika.

great thinking hii mkuu, big up
 
Ndoa zinabadilika. Zamani, kabla dini hazijaingia, dhana ya ndoa ilikuwa tofauti sana na ilivyo sasa katika jamii nyingi za kiafrika (Tanzania ikiwemo).

Katika jamii nyingi, ndoa za wake wengi ilikuwa sio 'dhambi'. Ingawa mfumo huu ni mbaya na haukubaliki (kwa mawazo ya sasa), lakini ulikuwa unampa uhuru mwanaume kuoa atakavyo tofauti na sasa. Hivyo katika 'mji', baba (mwenye mji) alikuwa na nyumba yake na kila mke alijengewa nyumba yake na watoto wakubwa na nyumba yao (hivyo mji unakuwa na nyumba at least tatu!). Hii ilipunguza kwa kiasi kikubwa mwanaume kuwa chini ya himaya mwanamke mmoja (kama ilivyo sasa).

Jingine ni separation kati ya wanawake na wanaume. Kulikuwa hakuna kukutana kwa mara kwa mara kati ya wanawake na wanaume katika social activities kama ilivyo leo. Kumbuka hakukuwa na shule kwa maana tunayoijua leo au kazi za maofisini nk ambazo zinawakutanisha wanaume na wanawake katika njia ambayo inarahisisha sana kufanyika kwa zinaa. Kutengishwa huku kulifanya iwe vigumu kufanya zinaa kama ilivyo sasa. Kama umempenda binti route ya kumpata ilikuwa ni kuoa(hata kama ni mke wa pili au tatu) na si vinginevyo!

Nimesema hayo machache, kujaribu kuonesha kuwa huwezi kuitizama ndoa peke yake kama unataka kuleta mabadiliko. Ni lazima uangalie social system yote na mabadiliko ni lazima yawe kwenye system nzima. Mimi naamini mabadiliko haya yanatokea yenyewe taratibu kadri muda na driving factors zote kwenye social system zinavyobadilika.


umejaribu kufafanua vya kutosha, mkuu. Nilisoma post ya mdau mmoja hapa na wazo kama hilo la kubadili mfumo mzima likanijia na hapo nikachoka. Tatizo ni kuonana kila muda na kuzoeana
 
Kitu tunachokisahau kabla ya kufunga ndoa,unapokuwa kwenye mapenzi makali,unafikiri kila kitu kinawezekana. Unasahau kuna siku urafiki huu utakwisha...utachoka na tabia ya huyu mwenzako uliyoivumilia ili mwe pamoja (kwa kipindi cha mapenzi makali)....utasahau kwamba mlikutana ukubwani na hamkulelewa na mama mmoja....na vitu vingi kibao ambavyo watu wengi hawavifikirii kabla. tunadhani mtu anaweza kubadilika....how? kama alikuwa akibadilisha wanawake/wanaume kama nguo,wewe ni nani wa kumfanya atulie? hatujiulizi maswali lukuki yanayoweza kutufanya kamwe tusiingie kwenye huu mkataba wa milele.
Uvumilivu unaotakiwa kwenye ndoa una-cost maisha,afya na rasilimali ulizonazo. na je watu wanapendana kweli au wanatamaniana tu? wanaposema I DO! inatoka moyoni au wanaogopa umati unaowatazama?
Wenzetu wa Magharibi baada ya kuona matatizo haya,waliamua kuihamishia ndoa kwenye mkataba. Unasaini kwa kipindi fulani halafu mkiona kuna haja ya kuongeza muda then mnaongeza. Mkichokana/ukichoka unaondoka kabla ya ngumi na maneno.
Nafikiri ungekuwepo mbadala hasa kwa wanawake kwa kiafrika nafikiri wengo wangekuwa na tabasamu midomoni mwao,maisha marefu ya furaha!
 
niliwaza sana haya zamani lakini kuna kipindi kinakuja chenyewe pale unapohitaji msaidizi katika maisha

Msaidizi wa nini? Maana sijasema usiwe na uhusiano. Nachosema ni kutokuoa ama kuolewa. Unaweza kabisa ukawa na uhusiano na mwenzako bila kuoana na mka define terms za uhusiano wenu. Ila mkishaingia kwenye ndoa kunakuwa na matarajio kibao ambayo mengine wala si realistic na ndio inakuwa mwanzo wa misery.
 
Kwa mawazo yenu wadau ningependa kuona ni jhnsi gani mtu anaepuka misery na kuwa furahani wakati wote kama katika kipindi cha uchumba. Tukiongelea mikataba itabidi mfumo wa maisha uwe tofauti na huu wa sasa kwa maana mikataba yaweza ponya upande mmoja na kuanzisha gonjwa upande mwingine
 
Kwa mawazo yenu wadau ningependa kuona ni jhnsi gani mtu anaepuka misery na kuwa furahani wakati wote kama katika kipindi cha uchumba.

Sio rahisi sana uhusiano ukabaki kama ilivyokuwa kipindi cha uchumba. Kipindi cha uchumba kina malengo tofauti na yale ya baada ya kuoana (naweza kufanya analogy ya kipindi cha uchumba na kipindi cha kampeni katika siasa!).

Kwa ajili ya mjadala huu naweza kugawa maisha ya ndoa katika hatua tau/vipindi vitatu:

Hatua ya kwanza (tuiite 'pretence and learning'): Inaanzia kwenye uchumba mpaka say mwaka mmoja au miwili baada ya ndoa. Hapa uhusiano unakuwa mzuri sana kwa sababu kila mmoja anajaribu kumpendeza mwenzake na kumuonesha kuwa yeye ni chaguo bora/sahihi (hii kwa walio wengi inaambatana na uongo/pretence kwa wingi sana). Kuna maelewando na kusameheana. Baadhi ya kasoro au mapungufu 'yanafichwa' au 'yanavumiliwa'. Hapa ndo utaona maua, kadi na vitu kama hivyo baina ya wapenzi.

Lakini kadri stage hii inavyoendelea wanandoa wanaanza kuonesha 'rangi' zao halisi na/au kuona 'rangi' halisi ya mwenza wake. Kwa kujibu swali lako, ni vema katika stage hii ukapunguza pretence na kuweka wazi vitu unavyoona ni kasoro/mapungufu kwa kadri uwezavyo (kumbuka sio rahisi kuiepuka pretence kwa 100%).

Hatua ya pili (hii tuiite 'reality'): Hapa wanandoa wameshafahamiana (mazuri na mabaya) na wanatoka kwenye pretence na kuingia kwenye reality (a spade will be called a spade!). Kila mmoja anabehave kiuhalisia kabisa (anaonesha 'rangi' yake bila woga). Sasa level hii huchukuwa muda mrefu sana na ndio kipindi cha matatizo mengi ya ndoa hasa hasa kama kuna vitu vingi 'vilifichwa' au 'havikuonekana' katika level ya kwanza.

Hatua ya tatu (hii tuiite 'maturity'): Katika kipindi hiki tayari wanandoa wameshapitia mikimiki yote ya hatua ya pili. 'Majeraha' mengi tayari 'yamepona'! Hiki ni kipindi kitamu na cha shukrani. Unasema "bila mama/baba nanii, nisingekuwa hapa". Laikini hili litategemea jinsi mlivyoweza kushughulikia matatizo katika hatua yenu ya pili. kumbuka 'majeraha' mengine yanaweza kusababisha 'ulemavu' hivyo bado kukawa na kinyongo na kulaumiana. Uzuri wa kipindi hiki wanandoa wanakuwa wameshakubali hali halisi whether ni mbaya au nzuri na wanaweza kuvumilia.

Binafsi nipo hatua ya pili na mambo sio rahisi hivyo lakini namshukuru mungu ndoa yangu bado imesimama:)!
 
Sio rahisi sana uhusiano ukabaki kama ilivyokuwa kipindi cha uchumba. Kipindi cha uchumba kina malengo tofauti na yale ya baada ya kuoana (naweza kufanya analogy ya kipindi cha uchumba na kipindi cha kampeni katika siasa!).

Kwa ajili ya mjadala huu naweza kugawa maisha ya ndoa katika hatua tau/vipindi vitatu:

Hatua ya kwanza (tuiite 'pretence and learning'): Inaanzia kwenye uchumba mpaka say mwaka mmoja au miwili baada ya ndoa. Hapa uhusiano unakuwa mzuri sana kwa sababu kila mmoja anajaribu kumpendeza mwenzake na kumuonesha kuwa yeye ni chaguo bora/sahihi (hii kwa walio wengi inaambatana na uongo/pretence kwa wingi sana). Kuna maelewando na kusameheana. Baadhi ya kasoro au mapungufu 'yanafichwa' au 'yanavumiliwa'. Hapa ndo utaona maua, kadi na vitu kama hivyo baina ya wapenzi.

Lakini kadri stage hii inavyoendelea wanandoa wanaanza kuonesha 'rangi' zao halisi na/au kuona 'rangi' halisi ya mwenza wake. Kwa kujibu swali lako, ni vema katika stage hii ukapunguza pretence na kuweka wazi vitu unavyoona ni kasoro/mapungufu kwa kadri uwezavyo (kumbuka sio rahisi kuiepuka pretence kwa 100%).

Hatua ya pili (hii tuiite 'reality'): Hapa wanandoa wameshafahamiana (mazuri na mabaya) na wanatoka kwenye pretence na kuingia kwenye reality (a spade will be called a spade!). Kila mmoja anabehave kiuhalisia kabisa (anaonesha 'rangi' yake bila woga). Sasa level hii huchukuwa muda mrefu sana na ndio kipindi cha matatizo mengi ya ndoa hasa hasa kama kuna vitu vingi 'vilifichwa' au 'havikuonekana' katika level ya kwanza.

Hatua ya tatu (hii tuiite 'maturity'): Katika kipindi hiki tayari wanandoa wameshapitia mikimiki yote ya hatua ya pili. 'Majeraha' mengi tayari 'yamepona'! Hiki ni kipindi kitamu na cha shukrani. Unasema "bila mama/baba nanii, nisingekuwa hapa". Laikini hili litategemea jinsi mlivyoweza kushughulikia matatizo katika hatua yenu ya pili. kumbuka 'majeraha' mengine yanaweza kusababisha 'ulemavu' hivyo bado kukawa na kinyongo na kulaumiana. Uzuri wa kipindi hiki wanandoa wanakuwa wameshakubali hali halisi whether ni mbaya au nzuri na wanaweza kuvumilia.

Binafsi nipo hatua ya pili na mambo sio rahisi hivyo lakini namshukuru mungu ndoa yangu bado imesimama:)!

big up kwa maono hayo. kwa maoni haya na mengine, ndoa inakuwa kama kipande/sehemu ya mwili wa mtu. mfano rangi, nywele, sura, au umbo. sasa kama hupendi kimojawapo kati ya hivyo kwenye mwili wako huna jinsi ya kukiepuka zaidi ya kukubali tu hali halisi. ndoa ni mpango/mfumo wa maisha ambao inaonekana hauwezi kuepukwa pamoja na mapungufu yake. binafsi nisingependa maishani nije kujutia kwa nini nilioa. kwa upande mwingine ni vigumu kuishi bila ya mwenza kwa namna Mungu alivyotuumba. katika kuhakikisha kuwa tunakabili mihamko yetu, tunakuwa na wenza ambao inafuata taratibu kuwa nao. kwa inavyoonekana, bila kufuata utaratibu itakuwa ni balaa katika tasnia nzima ya mahusiano. kwa vile ndoa ni mpango wa Mungu basi hauna mbadala? na inavyoonekana huu mfumo wa sasa unajaribu tu kupunguza maafa ambayo yangesababishwa na kutokuwepo kwa ndoa japo ndoa nayo ni sehemu ya matatizo. the best solution hapa ni kuwa na uvumilivu
 
Ni kweli ndoa ni muunganiko wa hiari, lakini hii hiari inanipa mashaka. Ukitaka kukodi ukumbi enzi hizi ujiandae miezi 6 kabla maana kila jmosi kuna harusi. Sasa hawa wanahiari kwenda kukabiliana na probability? Hata sheria hutoa tafsiri potofu ya vitu, ndio maana katiba pia hurekebishwa. Katiba ingeweka kifungu cha ndoa za mikataba mngeona mabadiliko ya ajabu kwenye ndoa. Mtu unaangalia kama kuna ulazima wa kuongeza mkataba au la. Hapo wabishi wangeshika adabu. Huu mtindo wa leo unaomhakikishia mwanandoa umoja wa kudumu ndio unaoleta kiburi na kuchokana ukifikiria kuwa huyu ndio nitakuwa nae maisha yaliyobakia. Sheria ya ndoa nayo ingetazamwa upya


MUME SIO BABA YAKO AKUNG'ANG'ANIE AU MKE SIO MAMA YAKO AKUNG'ANG'ANIE Pls listen to your heart, days are numbered
 
niliwaza sana haya zamani lakini kuna kipindi kinakuja chenyewe pale unapohitaji msaidizi katika maisha


Eti, FL akusaidie nini????? Money?, pleasure? sex? company or what?? better to stay single if you want to get rid of marriage calamities
 
katika nadharia za social reconstruction, kunaweza kupatikana mbadala wa ndoa za mfumo wa sasa.

kuna uwezekano wa kutenganisha uongozi wa ndoa na utendaji a ndoa.

migogoro mingi ya ndani ya ndoa ingeweza kupungua kama uongozi na utendaji vingetenganishwa mfano usingesikia upuuzi kama "tunagombana na mke wangu kwa sababu ni mchafu sana" katika mfumo huu mbadala, anakuwepo home secretary ambaye anakuwa ni home executive yaani ataajiriwa na kuwa na mkataba maalum wa utumishi wake na atawajibika kuajiri kama italazimu watumishi wengine wa kumsaidia kwa kibali maalum cha viongozi wa nyumba (wanandoa) na atakuwa na bajeti ya kila mwezi (aliyoipendekeza mwenyewe na kuidhinishwa na wanandoa) ambayo ataisimamaia kuhudumia familia, ndugu na jamaa wote, bajeti ambayo itachangiwa na wanandoa wote mume na mke kulingana na uwezo wao. Huyu sectrtary atawajibika kusimamia shughuli zote za kawaida na za maendeleo zitakazoamuliwa na wanandoa (uongozi) na atatoa hesabu ya matumizi na hesabu zake kukaguliwa kila mwaka.

Mfumo huu utaondoa kabisa wezekano wa magomvi madogomadoo yatokanayo na utendaji. Mfumo unaowahusisha ma-house girl tuliona sasa unamfanya mama uendelea kuwa mkuu wa timu ya watendaji ndani ya nyumba na ndio maana bado kuna kulaumiawa kwingi kwa mapungufu ya utendaji hata kama yanatokana na matendo ya moja kwa moja ya ma-house girl.

Uu si mfumo mgeni hapa duniani, mfano matajiri wakubwa na viongozi wakubwa (kama marais) karibu wote hutumia mfumo huu, na umesaidia sana kupunguza igogoro ya ndoa kwa watu wa kada hizi.

Tatizo la mfumo huu ni gharama za kuuendesha, kwani walio na uwezo mdogo wa kifedha watashindwa kumudu kuuendesha, lakii wenye uchumi mzuri wanaweza kunufaika sana wakitmia mfumo huu.

Duuuuuuu! Mgombe Ubunge labda uko kwenye kampeni za ubunge zaidi kuliko thread yenyewe inavyosema. Ugomvi ndani ya ndoa unatokana na sababu za msingi. Hizo ulizozisema ni chembe tu ya sababu halisi. Waliopo kwenye ndoa mtasaidia hapa. Mapenzi sio fedha, mali mliyonayo wanandoa. Mapenzi ni mapenzi kati yenu ninyi wawili tu hakuna tarishi mtakayemwajiri awe ndio muuaarobaini wa matatizo ya ndoa yenu. Tatizo kubwa ni yale matatizo yanayomfanya mwenzi wako ajione anadhurumika kimapenzi hapo ndipo huwa hapatoshi.
 
MUME SIO BABA YAKO AKUNG'ANG'ANIE AU MKE SIO MAMA YAKO AKUNG'ANG'ANIE Pls listen to your heart, days are numbered

kuna ruba ndugu yangu wala usipime. tuulize tuliong'ang'aniwa hadi tukavunja simu na ilipobidi tukafika polisi. listening to your heart makes you a bit soft. just reasoning and thinking. the heart will follow
 
Back
Top Bottom