mbadala wa ndoa

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,876
2,744
ni ndoa chache zenye uwezo wa kuishi bila mitafaruku ya ajabu katika kipindi chote cha kuwa wawili. vipindi vya mapenzi na uchumba huwa tofauti na kipindi cha kuwa ndani ya ndoa. watu husema mengi tu juu ya wenza wao ikiashiria kuchokana ila kwa vile wako ndoani hawana namna. sijaoa ila hayo maisha nimeshayapitia. kipindi cha mitafaruku ya hapa na pale kimbilio huwa ni kitulizo nje ya ndoa (uzinzi). i wish mke na mume wasingekuwa wanakaa nyumba moja kwa lazima kama mfumo wa sasa wa ndoa unavyodai. mume anaweza kuishi kimara na mke tabata na wakawa wana maisha mazuri tu. kinacholeta wivu ni ile hali ya kujua sasa huyu yuko ndani ya himaya yangu (si mwanamke wala mwanaume). kila mmoja yuko kwenye himaya ya mwenzake. kwa nini mtu anafurahia kuwa na hawara? mke kaachwa, wanandoa wamepigana, mume kaachwa, mke/mume kazini, watoto wanateseka, mtoto hamjui baba/mama. imebaki kuvumiliana tu. why? hakuna mbadala wa mfumo huu wa ndoa? kwani ndoa ni kanuni isiyobadilika? hapa jamvini najua mpo mliohitilafiana na wenza wenu. kwa nini mnaishi kimungumungu hadi kifo kiwatenganishe? raha mara nyingi ndani ya ndoa ni suala ma masaa na siku, ila wakati wote mwingine ni kuwindana. tujadilini labda tunaweza kupata mfumo mbadala wa maisha ya sasa ya ndoa. try to think
 
ni ndoa chache zenye uwezo wa kuishi bila mitafaruku ya ajabu katika kipindi chote cha kuwa wawili. vipindi vya mapenzi na uchumba huwa tofauti na kipindi cha kuwa ndani ya ndoa. watu husema mengi tu juu ya wenza wao ikiashiria kuchokana ila kwa vile wako ndoani hawana namna. sijaoa ila hayo maisha nimeshayapitia. kipindi cha mitafaruku ya hapa na pale kimbilio huwa ni kitulizo nje ya ndoa (uzinzi). i wish mke na mume wasingekuwa wanakaa nyumba moja kwa lazima kama mfumo wa sasa wa ndoa unavyodai. mume anaweza kuishi kimara na mke tabata na wakawa wana maisha mazuri tu. kinacholeta wivu ni ile hali ya kujua sasa huyu yuko ndani ya himaya yangu (si mwanamke wala mwanaume). kila mmoja yuko kwenye himaya ya mwenzake. kwa nini mtu anafurahia kuwa na hawara? mke kaachwa, wanandoa wamepigana, mume kaachwa, mke/mume kazini, watoto wanateseka, mtoto hamjui baba/mama. imebaki kuvumiliana tu. why? hakuna mbadala wa mfumo huu wa ndoa? kwani ndoa ni kanuni isiyobadilika? hapa jamvini najua mpo mliohitilafiana na wenza wenu. kwa nini mnaishi kimungumungu hadi kifo kiwatenganishe? raha mara nyingi ndani ya ndoa ni suala ma masaa na siku, ila wakati wote mwingine ni kuwindana. tujadilini labda tunaweza kupata mfumo mbadala wa maisha ya sasa ya ndoa. try to think

Mziwanda... hii ni changamoto ya ukweli lakini fikiria haya:
-Ndoa ni muunganiko wa hiari kufuatana na tafsiri ya kisheria - ina maana hulazimishwi kuoa/kuolewa katika hali ya kawaida.
-Ndoa huzaa mambo mengi - wanandoa huweza kusababisha kuleta viumbe wengine duniani na hawa wanahitaji kuhudumiwa.Sheria inakulazimisha uwajibike katika hili na huwezi kutelekeza wajibu huu.
- Ndoa huwafanya wahusika kujikuta kwenye hali inayopelekea kupoteza haki fulani kwa maana umimi na kuwa vyetu, chetu, sisi.Ina maana kubwa sana na kujinasua ina gharama zake
-Kutegemeana na mila, desturi na imani za kidini, wanandoa huweza kujikuta wako kwenye pingu za maisha na kuachana ni ngumu.Hapo mtu ndio hulazimika kuvumilia hadi kifo kiwatenganishe!
-Hakuna uhusiano usio kuwa na migongano- hata ndugu wa tumbo moja hutofautiana.Kwa wanandoa bahati mbaya vyanzo vya ugomvi vinaweza kuwa vingi zaidi na vyenye kuumiza zaidi kuliko uhusiano wa kawaida.
Having said that..... binadamu naye kwa hulka huvunja sheria, kanuni na taratibu pale yanapomzidia lakini hii humgharimu vibaya sana.
-Mbadala wa ndoa utamaanisha kufumua mfumo mzima na itakuwa siyo ndoa tena.
Huu ni mtazamo wangu tu!
 
Sidhani kama kuna mbadala wa ndoa.. Ndoa ni kuvumiliana humohumo mpaka kifo kinawatenganisha.. Mme/Mke kuwa na uhusiano pembeni, inawezekana ikawa sio mtafaruku wa ndoa.. Kuna mambo mengi ambayo huwafanya wanandoa kwenda nje ya ndoa zao. Kubwa zaidi ni tamaa ya mwili na sio kingine.. Mind you ALICHOKIUNGANISHA MUNGU, MWANADAMU ASIKITENGANISHE.

Those who have big problems during the 1st days of their marriage. Huwa wanamaliza na ndoa nzuri sana uzeeni.
 
Ni kweli ndoa ni muunganiko wa hiari, lakini hii hiari inanipa mashaka. Ukitaka kukodi ukumbi enzi hizi ujiandae miezi 6 kabla maana kila jmosi kuna harusi. Sasa hawa wanahiari kwenda kukabiliana na probability? Hata sheria hutoa tafsiri potofu ya vitu, ndio maana katiba pia hurekebishwa. Katiba ingeweka kifungu cha ndoa za mikataba mngeona mabadiliko ya ajabu kwenye ndoa. Mtu unaangalia kama kuna ulazima wa kuongeza mkataba au la. Hapo wabishi wangeshika adabu. Huu mtindo wa leo unaomhakikishia mwanandoa umoja wa kudumu ndio unaoleta kiburi na kuchokana ukifikiria kuwa huyu ndio nitakuwa nae maisha yaliyobakia. Sheria ya ndoa nayo ingetazamwa upya
 
Ni kweli ndoa ni muunganiko wa hiari, lakini hii hiari inanipa mashaka. Ukitaka kukodi ukumbi enzi hizi ujiandae miezi 6 kabla maana kila jmosi kuna harusi. Sasa hawa wanahiari kwenda kukabiliana na probability? Hata sheria hutoa tafsiri potofu ya vitu, ndio maana katiba pia hurekebishwa. Katiba ingeweka kifungu cha ndoa za mikataba mngeona mabadiliko ya ajabu kwenye ndoa. Mtu unaangalia kama kuna ulazima wa kuongeza mkataba au la. Hapo wabishi wangeshika adabu. Huu mtindo wa leo unaomhakikishia mwanandoa umoja wa kudumu ndio unaoleta kiburi na kuchokana ukifikiria kuwa huyu ndio nitakuwa nae maisha yaliyobakia. Sheria ya ndoa nayo ingetazamwa upya

Na maumivu pia pale itakapotokea wewe bado unampenda mwenzi wako halafu mwenzio keshakamatwa na kucheche hataki kurenew mkataba.

But thinking of it................ itakuwaje when it comes to suala la maendeleo? Mtajenga pamoja kwa muda huo wa mkataba au kila mmoja atakuwa anachuma vyake?
 
Mziwanda... hii ni changamoto ya ukweli lakini fikiria haya:
-Ndoa ni muunganiko wa hiari kufuatana na tafsiri ya kisheria - ina maana hulazimishwi kuoa/kuolewa katika hali ya kawaida.
-Ndoa huzaa mambo mengi - wanandoa huweza kusababisha kuleta viumbe wengine duniani na hawa wanahitaji kuhudumiwa.Sheria inakulazimisha uwajibike katika hili na huwezi kutelekeza wajibu huu.
- Ndoa huwafanya wahusika kujikuta kwenye hali inayopelekea kupoteza haki fulani kwa maana umimi na kuwa vyetu, chetu, sisi.Ina maana kubwa sana na kujinasua ina gharama zake
-Kutegemeana na mila, desturi na imani za kidini, wanandoa huweza kujikuta wako kwenye pingu za maisha na kuachana ni ngumu.Hapo mtu ndio hulazimika kuvumilia hadi kifo kiwatenganishe!
-Hakuna uhusiano usio kuwa na migongano- hata ndugu wa tumbo moja hutofautiana.Kwa wanandoa bahati mbaya vyanzo vya ugomvi vinaweza kuwa vingi zaidi na vyenye kuumiza zaidi kuliko uhusiano wa kawaida.
Having said that..... binadamu naye kwa hulka huvunja sheria, kanuni na taratibu pale yanapomzidia lakini hii humgharimu vibaya sana.
-Mbadala wa ndoa utamaanisha kufumua mfumo mzima na itakuwa siyo ndoa tena.
Huu ni mtazamo wangu tu!

Mkulu,

Yaani ninakukubari! na nina kuheshimu mno,just for this useful post.
Mimi nimeoa muda mwingi tu nyuma na kila siku ya iendayo ni namwona Mungu kwenye maisha yangu ya ndoa.
Sio kwamba hakuna kutofautiana kwenye ndoa yangu,la hasha! Lakini kwenye ugomvi na kutofautiana huko na mjua Mungu zaidi na nina mshukuru Mungu kwa kunipa huyu mwenzangu.
Ndoa ni mpango wa mungu,hakuna mbadala wa hili kama lingekuwapo basi lingeonekana katika umri huu wa Dunia hii (zaidi ya miaka Milioni Nyingi)
 
katika nadharia za social reconstruction, kunaweza kupatikana mbadala wa ndoa za mfumo wa sasa.

kuna uwezekano wa kutenganisha uongozi wa ndoa na utendaji a ndoa.

migogoro mingi ya ndani ya ndoa ingeweza kupungua kama uongozi na utendaji vingetenganishwa mfano usingesikia upuuzi kama "tunagombana na mke wangu kwa sababu ni mchafu sana" katika mfumo huu mbadala, anakuwepo home secretary ambaye anakuwa ni home executive yaani ataajiriwa na kuwa na mkataba maalum wa utumishi wake na atawajibika kuajiri kama italazimu watumishi wengine wa kumsaidia kwa kibali maalum cha viongozi wa nyumba (wanandoa) na atakuwa na bajeti ya kila mwezi (aliyoipendekeza mwenyewe na kuidhinishwa na wanandoa) ambayo ataisimamaia kuhudumia familia, ndugu na jamaa wote, bajeti ambayo itachangiwa na wanandoa wote mume na mke kulingana na uwezo wao. Huyu sectrtary atawajibika kusimamia shughuli zote za kawaida na za maendeleo zitakazoamuliwa na wanandoa (uongozi) na atatoa hesabu ya matumizi na hesabu zake kukaguliwa kila mwaka.

Mfumo huu utaondoa kabisa wezekano wa magomvi madogomadoo yatokanayo na utendaji. Mfumo unaowahusisha ma-house girl tuliona sasa unamfanya mama uendelea kuwa mkuu wa timu ya watendaji ndani ya nyumba na ndio maana bado kuna kulaumiawa kwingi kwa mapungufu ya utendaji hata kama yanatokana na matendo ya moja kwa moja ya ma-house girl.

Uu si mfumo mgeni hapa duniani, mfano matajiri wakubwa na viongozi wakubwa (kama marais) karibu wote hutumia mfumo huu, na umesaidia sana kupunguza igogoro ya ndoa kwa watu wa kada hizi.

Tatizo la mfumo huu ni gharama za kuuendesha, kwani walio na uwezo mdogo wa kifedha watashindwa kumudu kuuendesha, lakii wenye uchumi mzuri wanaweza kunufaika sana wakitmia mfumo huu.
 
katika nadharia za social reconstruction, kunaweza kupatikana mbadala wa ndoa za mfumo wa sasa.

kuna uwezekano wa kutenganisha uongozi wa ndoa na utendaji a ndoa.

migogoro mingi ya ndani ya ndoa ingeweza kupungua kama uongozi na utendaji vingetenganishwa mfano usingesikia upuuzi kama "tunagombana na mke wangu kwa sababu ni mchafu sana" katika mfumo huu mbadala, anakuwepo home secretary ambaye anakuwa ni home executive yaani ataajiriwa na kuwa na mkataba maalum wa utumishi wake na atawajibika kuajiri kama italazimu watumishi wengine wa kumsaidia kwa kibali maalum cha viongozi wa nyumba (wanandoa) na atakuwa na bajeti ya kila mwezi (aliyoipendekeza mwenyewe na kuidhinishwa na wanandoa) ambayo ataisimamaia kuhudumia familia, ndugu na jamaa wote, bajeti ambayo itachangiwa na wanandoa wote mume na mke kulingana na uwezo wao. Huyu sectrtary atawajibika kusimamia shughuli zote za kawaida na za maendeleo zitakazoamuliwa na wanandoa (uongozi) na atatoa hesabu ya matumizi na hesabu zake kukaguliwa kila mwaka.

Mfumo huu utaondoa kabisa wezekano wa magomvi madogomadoo yatokanayo na utendaji. Mfumo unaowahusisha ma-house girl tuliona sasa unamfanya mama uendelea kuwa mkuu wa timu ya watendaji ndani ya nyumba na ndio maana bado kuna kulaumiawa kwingi kwa mapungufu ya utendaji hata kama yanatokana na matendo ya moja kwa moja ya ma-house girl.

Uu si mfumo mgeni hapa duniani, mfano matajiri wakubwa na viongozi wakubwa (kama marais) karibu wote hutumia mfumo huu, na umesaidia sana kupunguza igogoro ya ndoa kwa watu wa kada hizi.

Tatizo la mfumo huu ni gharama za kuuendesha, kwani walio na uwezo mdogo wa kifedha watashindwa kumudu kuuendesha, lakii wenye uchumi mzuri wanaweza kunufaika sana wakitmia mfumo huu.

Mkulu MGOMBEA,

Umenifurahisha sana,bado nafiriki kuna uwezekano unajaribu ku-plot some sort of a play (drama)
Sasa......,inawezekana kabisa kwa mtazamo wa mbadala huu uliotuwekea hapa aliyekua Raisi wa Marekani Bill Clinton mbadala huu ulikua hautumiki ndio maana akazama kwa Monica Rewensky.....?
 
Mkulu MGOMBEA,

Umenifurahisha sana,bado nafiriki kuna uwezekano unajaribu ku-plot some sort of a play (drama)
Sasa......,inawezekana kabisa kwa mtazamo wa mbadala huu uliotuwekea hapa aliyekua Raisi wa Marekani Bill Clinton mbadala huu ulikua hautumiki ndio maana akazama kwa Monica Rewensky.....?

sio drama mkuu, ukiujaribu, it works!

kama ni ugomvi mtagombana kwa mambo yenu ya chumbani lakini katika magomvi yatokanayo na masuala ya utendaji, mtakuwa mmeishayaepuka moja kwa moja!
 
ni ndoa chache zenye uwezo wa kuishi bila mitafaruku ya ajabu katika kipindi chote cha kuwa wawili. vipindi vya mapenzi na uchumba huwa tofauti na kipindi cha kuwa ndani ya ndoa. watu husema mengi tu juu ya wenza wao ikiashiria kuchokana ila kwa vile wako ndoani hawana namna. sijaoa ila hayo maisha nimeshayapitia. kipindi cha mitafaruku ya hapa na pale kimbilio huwa ni kitulizo nje ya ndoa (uzinzi). i wish mke na mume wasingekuwa wanakaa nyumba moja kwa lazima kama mfumo wa sasa wa ndoa unavyodai. mume anaweza kuishi kimara na mke tabata na wakawa wana maisha mazuri tu. kinacholeta wivu ni ile hali ya kujua sasa huyu yuko ndani ya himaya yangu (si mwanamke wala mwanaume). kila mmoja yuko kwenye himaya ya mwenzake. kwa nini mtu anafurahia kuwa na hawara? mke kaachwa, wanandoa wamepigana, mume kaachwa, mke/mume kazini, watoto wanateseka, mtoto hamjui baba/mama. imebaki kuvumiliana tu. why? hakuna mbadala wa mfumo huu wa ndoa? kwani ndoa ni kanuni isiyobadilika? hapa jamvini najua mpo mliohitilafiana na wenza wenu. kwa nini mnaishi kimungumungu hadi kifo kiwatenganishe? raha mara nyingi ndani ya ndoa ni suala ma masaa na siku, ila wakati wote mwingine ni kuwindana. tujadilini labda tunaweza kupata mfumo mbadala wa maisha ya sasa ya ndoa. try to think

Wewe unataka waishi Kishetanisheta au kiibilisi ibilisi
 
mlete mada amezungumzia zaidi mambo ya chumbani na sio maswala ya utendaji,sisi wanaume hatujihusishi sana na mambo ya how things are done in the house we leave those to the wives.
But the issues here ni sex,wivu,cheating of all kinds na mambo mengine yatokanayo na muunganiko wa wa mke na mume (kwa ujumla wake )
 
mlete mada amezungumzia zaidi mambo ya chumbani na sio maswala ya utendaji,sisi wanaume hatujihusishi sana na mambo ya how things are done in the house we leave those to the wives.
But the issues here ni sex,wivu,cheating of all kinds na mambo mengine yatokanayo na muunganiko wa wa mke na mume (kwa ujumla wake )

mkuu ujue kuwa mambo ya nje hayaathiri sana ndoa kama unavyodhani, bali mambo ya ndani. na matatizo mengi ya ndoa huanzia ndani. mbona wakati wa uchumba mambo huwa shwari ila wakati w ndoa mambo ndio huanza kuvurugika? nadhani hapo ulipasahau
 
Na maumivu pia pale itakapotokea wewe bado unampenda mwenzi wako halafu mwenzio keshakamatwa na kucheche hataki kurenew mkataba.

But thinking of it................ itakuwaje when it comes to suala la maendeleo? Mtajenga pamoja kwa muda huo wa mkataba au kila mmoja atakuwa anachuma vyake?

hapo tena ndio panapokuja mtihani. ila, kuwe na ndoa za aina mbili: za mikataba na za kudumu. mtu anaweza kuchagua aina ya ndoa aitakayo
 
ni ndoa chache zenye uwezo wa kuishi bila mitafaruku ya ajabu katika kipindi chote cha kuwa wawili. vipindi vya mapenzi na uchumba huwa tofauti na kipindi cha kuwa ndani ya ndoa. watu husema mengi tu juu ya wenza wao ikiashiria kuchokana ila kwa vile wako ndoani hawana namna. sijaoa ila hayo maisha nimeshayapitia. kipindi cha mitafaruku ya hapa na pale kimbilio huwa ni kitulizo nje ya ndoa (uzinzi). i wish mke na mume wasingekuwa wanakaa nyumba moja kwa lazima kama mfumo wa sasa wa ndoa unavyodai. mume anaweza kuishi kimara na mke tabata na wakawa wana maisha mazuri tu. kinacholeta wivu ni ile hali ya kujua sasa huyu yuko ndani ya himaya yangu (si mwanamke wala mwanaume). kila mmoja yuko kwenye himaya ya mwenzake. kwa nini mtu anafurahia kuwa na hawara? mke kaachwa, wanandoa wamepigana, mume kaachwa, mke/mume kazini, watoto wanateseka, mtoto hamjui baba/mama. imebaki kuvumiliana tu. why? hakuna mbadala wa mfumo huu wa ndoa? kwani ndoa ni kanuni isiyobadilika? hapa jamvini najua mpo mliohitilafiana na wenza wenu. kwa nini mnaishi kimungumungu hadi kifo kiwatenganishe? raha mara nyingi ndani ya ndoa ni suala ma masaa na siku, ila wakati wote mwingine ni kuwindana. tujadilini labda tunaweza kupata mfumo mbadala wa maisha ya sasa ya ndoa. try to think

Ndoa zinabadilika. Zamani, kabla dini hazijaingia, dhana ya ndoa ilikuwa tofauti sana na ilivyo sasa katika jamii nyingi za kiafrika (Tanzania ikiwemo).

Katika jamii nyingi, ndoa za wake wengi ilikuwa sio 'dhambi'. Ingawa mfumo huu ni mbaya na haukubaliki (kwa mawazo ya sasa), lakini ulikuwa unampa uhuru mwanaume kuoa atakavyo tofauti na sasa. Hivyo katika 'mji', baba (mwenye mji) alikuwa na nyumba yake na kila mke alijengewa nyumba yake na watoto wakubwa na nyumba yao (hivyo mji unakuwa na nyumba at least tatu!). Hii ilipunguza kwa kiasi kikubwa mwanaume kuwa chini ya himaya mwanamke mmoja (kama ilivyo sasa).

Jingine ni separation kati ya wanawake na wanaume. Kulikuwa hakuna kukutana kwa mara kwa mara kati ya wanawake na wanaume katika social activities kama ilivyo leo. Kumbuka hakukuwa na shule kwa maana tunayoijua leo au kazi za maofisini nk ambazo zinawakutanisha wanaume na wanawake katika njia ambayo inarahisisha sana kufanyika kwa zinaa. Kutengishwa huku kulifanya iwe vigumu kufanya zinaa kama ilivyo sasa. Kama umempenda binti route ya kumpata ilikuwa ni kuoa(hata kama ni mke wa pili au tatu) na si vinginevyo!

Nimesema hayo machache, kujaribu kuonesha kuwa huwezi kuitizama ndoa peke yake kama unataka kuleta mabadiliko. Ni lazima uangalie social system yote na mabadiliko ni lazima yawe kwenye system nzima. Mimi naamini mabadiliko haya yanatokea yenyewe taratibu kadri muda na driving factors zote kwenye social system zinavyobadilika.
 
katika nadharia za social reconstruction, kunaweza kupatikana mbadala wa ndoa za mfumo wa sasa.

kuna uwezekano wa kutenganisha uongozi wa ndoa na utendaji a ndoa.

migogoro mingi ya ndani ya ndoa ingeweza kupungua kama uongozi na utendaji vingetenganishwa mfano usingesikia upuuzi kama "tunagombana na mke wangu kwa sababu ni mchafu sana" katika mfumo huu mbadala, anakuwepo home secretary ambaye anakuwa ni home executive yaani ataajiriwa na kuwa na mkataba maalum wa utumishi wake na atawajibika kuajiri kama italazimu watumishi wengine wa kumsaidia kwa kibali maalum cha viongozi wa nyumba (wanandoa) na atakuwa na bajeti ya kila mwezi (aliyoipendekeza mwenyewe na kuidhinishwa na wanandoa) ambayo ataisimamaia kuhudumia familia, ndugu na jamaa wote, bajeti ambayo itachangiwa na wanandoa wote mume na mke kulingana na uwezo wao. Huyu sectrtary atawajibika kusimamia shughuli zote za kawaida na za maendeleo zitakazoamuliwa na wanandoa (uongozi) na atatoa hesabu ya matumizi na hesabu zake kukaguliwa kila mwaka.

Mfumo huu utaondoa kabisa wezekano wa magomvi madogomadoo yatokanayo na utendaji. Mfumo unaowahusisha ma-house girl tuliona sasa unamfanya mama uendelea kuwa mkuu wa timu ya watendaji ndani ya nyumba na ndio maana bado kuna kulaumiawa kwingi kwa mapungufu ya utendaji hata kama yanatokana na matendo ya moja kwa moja ya ma-house girl.

Uu si mfumo mgeni hapa duniani, mfano matajiri wakubwa na viongozi wakubwa (kama marais) karibu wote hutumia mfumo huu, na umesaidia sana kupunguza igogoro ya ndoa kwa watu wa kada hizi.

Tatizo la mfumo huu ni gharama za kuuendesha, kwani walio na uwezo mdogo wa kifedha watashindwa kumudu kuuendesha, lakii wenye uchumi mzuri wanaweza kunufaika sana wakitmia mfumo huu.

Ndugu yangu....
aSANTE KWA KULETA HII DIMENSION katika mjadala. Huu utaratatibu siyo mgeni sana japo ni wachache sana hapa Tanzania ( wazawa) wanamudu lakini upo.Kwa uzoefu kidogo... unapokuwa na huyu mtu ujue hatakuwa sehemu ya ndoa bali ni member of household staff! Matatizo yenu ya ndoa yako palepale! Uchafu/usafi wa nyumba, ubora wa chakula, usimamizi wa watoto uelewe siyo tatizo kubwa sana linaloharibu ladha ya ndoa.If anything hivi ni vijisababu tu vya kukoleza ugomvi.

Kama wewe uko kwenye ndoa utakubaliana nami kuwa, ikiwa hakuna ugomvi au migogoro, basi hutaona upungufu kivile wa mwenzio.Pale mnapokuwa na migogoro, ndipo utaona mambo mengine yakiibuliwa - mara ohh siku hizi hata hujali kupika na ndio maana chakula kinachelewa, hakina ubora, hujali watoto n.k hata kama mwenzio ndio wa kwanza kukuvurugia utaratibu uliojiwekea ili tu umpe kampani!
Matatizo ya ndoa ni very complex and complicated kama ilivyo ndoa yenyewe!
 
Back
Top Bottom