Nyetk
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 1,648
- 1,701
Heshima kwenu wakuu.
Mimi ni mteja wa miaka mingi wa DSTV, huduma za MultiChoice Africa na kwa kweli napenda sana chaneli zao nyingi. Kama ilivyo kwa watanzania wengi mimi ni mpenzi mkubwa wa mpira na michezo kwa ujumla na bila shaka tunajua kwamba kampuni hii imejiuza zaidi kupitia chaneli zake murua za Super Sports.
Hivi sasa nimechoshwa mno na ukiritimba wa kampuni hii unaotokana na wao kuwa ndio wauzaji pekee (wanaojulikana huku) wa chaneli kipenzi cha wengi. Nakerwa sana ninapokuwa nimelipia mwaka mzima halafu wananikatia matangazo wakati wowote wanapojisikia eti salio lako limekwisha hata kama bado miezi sita. Ni kweli ukienda kulalamika watakuongezea kwenye akaunti yako zile siku walizokata, lakini hiyo hairejeshi adha unayoipata na watumiaji wenzako (wageni, wateja, nk) mathalani kama kulikuwa na tukio live muhimu kulifuatilia likipita limepita na hicho ndicho kinakera. Wakati mwingine unaleta fundi abani kama shida ipo kwenye network yako na unalazimika kumlipa.
Ni nafuu "monopoly" hii katika bidhaa hizi ingeondoka manaa Tanzania inakuwa motoni sasa; kila mahali tumebanwa na "monopoly zisizo na tija – kwenye siasa kero, kwenye uchumi kero, hata kwenye burudani pia? Wanabodi anayejua kampuni mbadala wa DSTV anijuze niwapige chini hawa haki ya nani!
Mimi ni mteja wa miaka mingi wa DSTV, huduma za MultiChoice Africa na kwa kweli napenda sana chaneli zao nyingi. Kama ilivyo kwa watanzania wengi mimi ni mpenzi mkubwa wa mpira na michezo kwa ujumla na bila shaka tunajua kwamba kampuni hii imejiuza zaidi kupitia chaneli zake murua za Super Sports.
Hivi sasa nimechoshwa mno na ukiritimba wa kampuni hii unaotokana na wao kuwa ndio wauzaji pekee (wanaojulikana huku) wa chaneli kipenzi cha wengi. Nakerwa sana ninapokuwa nimelipia mwaka mzima halafu wananikatia matangazo wakati wowote wanapojisikia eti salio lako limekwisha hata kama bado miezi sita. Ni kweli ukienda kulalamika watakuongezea kwenye akaunti yako zile siku walizokata, lakini hiyo hairejeshi adha unayoipata na watumiaji wenzako (wageni, wateja, nk) mathalani kama kulikuwa na tukio live muhimu kulifuatilia likipita limepita na hicho ndicho kinakera. Wakati mwingine unaleta fundi abani kama shida ipo kwenye network yako na unalazimika kumlipa.
Ni nafuu "monopoly" hii katika bidhaa hizi ingeondoka manaa Tanzania inakuwa motoni sasa; kila mahali tumebanwa na "monopoly zisizo na tija – kwenye siasa kero, kwenye uchumi kero, hata kwenye burudani pia? Wanabodi anayejua kampuni mbadala wa DSTV anijuze niwapige chini hawa haki ya nani!