MotoYaMbongo
JF-Expert Member
- Jan 7, 2008
- 2,146
- 884
Aluta continua Ma Dr.
Basi madaktari wakikinukisha hiyo tar 3......
Vichwa panzi waongo utawasikia "Rais si aliahidi kulishughulikia suala lao kwenye hotuba ya juzi"...
Utafikiri bado tupo kwenye zama za ahadi.
mimi ni daktari wa binadamu-medical dokta, sipendi kuona kuwa madaktari ni wabinafsi, katika medical practice, kazi inafanyika katika timu, ila mara nyingi kiongozi wa timu ni daktari, anasaidiwa na support staff wote kama manesi, wafamasia, mafundi maabara, na wengine wengi. Kila kitu kwa mgonjwa ni order ya daktari, mfano, mchome sindano hii, mpe dawa hii, mpime malaria, mpige xray, mpige mionzi hii nk, hakuna kinachofanyika bila order ya dr, support staff yeyote anaweza kumsaidia mgonjwa kwa uzoefu lakini si utaratibu, popote pale mfamasia anasoma prescripition iliyoandikwana daktari aliyesajiliwa ndio atoe dawa, kwa hiyo yote kazi hii ya medical ina team leader au driver.
Nikija kwenye maslahi, yaongezeke proportionally kwa wanaojua hesabu, wote waongezewe, pia sekta nyingine za nchi hii, napinga sana ubaguzi wa maslahi ulioanzishwa na fisadi mkapa, ndio aliyetufikisha hapa. Madaktari wasingegoma kama nchi hii ingekuwa na usawa na nchi ya haki. Tusibaguane, katika kada za afya au nyingine ndani ya nchi hii., kila mtu ni muhimu katika kada yake ndani ya nchi hii,
Ndugu wana jamii!
Sitaki kuamini kuwa serikali imefanya kosa katika kuwaita kada nyingine, tatizo ni tafsiri ya neno daktari. Kiserikali, kutokana na matatizo ya huko nyuma, neno daktari linamaana ya kada zote za afya kutokana na mfumo udaktari uliopo wizara ya afya, ambapo hata kada zingine kama za nurse, famasia ati kurugenzi zinaongozwa na daktari. Sasa, serikali inalitambua hilo ndio maana, haiwezi kuboresha maslahi ya madaktari bila ya kuziboresha kada zingine.HAIWEZEKANI. Nao pia wana madai yao, ndio maana hata wauguzi wanadai kurugenzi yao, famasi kadhalika, sasa mnataka madaktari ndio wawasemee???? huko nyuma wakati wa Raisi mwinyi, mgomo ulitokea, na baada ya serkali kukubali matakwa ya madaktari, maslahi yaliboreshwa kwa madaktari tuu, hii ilileta shida sana pae manesi walipogoma. Na kiukweli, kada zote za afya zinafanya kazi kama timu ya pamoja na hakuna aliye juu ya mwingine, tatizo ni saikolojia ya madaktari wa tanzania kujiona wako juu kuliko taaluma zingine, nenda ulaya, mgonjwa hawezi kupatiwa dawa kama haijapitiwa na mfamasia, n.k , hivyo wasijione ni special sana, kada zote zinaumuhimu, leo manesi wakisema hatufanyi kazi, madaktari mnaweza kufanya kazi peke yenu???? mlipogoma, vifo si vingi sana kama manesi wakigoma.
Acheni ubinafsi, ndio sababu hata manesi wataka idara yao, na si kila kitu paka mganga mkuu hata kama kinahusu taaluma nyingine.
Mmmm!
Lugha inaonyeha wewe ni Dr lakini wa miti shamba.
Umeongea vizuri mkuu.kuna kitu umemiss mkuu
kuna madai ya mara moja... hayo hayatatuliwi kwa long term discussions na kuhusisha kada nyingine, maana yake ni kwamba serikali ilitakiwa itatue hayo kwanza (kama ilivyozungusha waraka wa kupandisha call allowances)
halafu kuna madai ya wana sekta wote - hayo ni lazima yaje baada ya emergency
huwezi kuwa na nyumba inavuja paa lake, na ni vmua ya masika ukasema ngoja nitafute fundi wa makapeti, vitasa, mabati, umeme, sink, rangi, na mapambo.... first thing first!!!
BTW, kuna watu pale wanaowakilisha sekta ya afya, wanatumiwa kuua fani mojawapo for years na wanajua wapo upande upi
drs. wameona mbali mengine tuwaachie wenyewe, kwani si ya kuweka hapa