Tegelezeni
JF-Expert Member
- Dec 31, 2009
- 268
- 124
Kama ukichunguza kwa mfuatano, tukio la hivi karibuni la Lulu kuhusishwa na mauaji ya Kanumba, siamini kama hilo linaweza kuzusha mshangao.
Binti kama Lulu kwanza amelelewa na malezi ya upande mmoja, yaani kalelewa na mama yake tu ..na wakati bado akihitaji malezi ya karibu kutoka kwa mama yake, akavutwa na watengeneza filamu wa Bongo walioibuka kama uyoga .tamaa ya fedha na kutafuta rasilimali watu rahisi inamkumba binti huyu kwa kigezo cha kuwezeshwa kujiajiri ili apate kusoma kwa ustawi wa maisha yake na familia yake.
Binti huyu anafinyangwa kitabia na jamii hii ya waigizaji waliokimbilia cheap popularity baada ya kushindwa kuendelea na masomo au kufukuzwa shule kutokana na tabia zisizofaa.
Taaluma ya filamu hapa nchini haiongozwi na watu wenye taaluma hiyo, bali wababaishaji na watu walioshindwa maisha .na kutokana na ugeni wetu katika jambo hilo (Mkumbuke kwamba kwa takriban miaka 27 ya utawala wa chama kimoja tulikuwa hatujui TV ni kitu gani) tasnia hiyo ikajizolea umaarufu na ikawa ndio njia rahisi kwa wale wasio na elimu kujiingizia kipato si haba.
Hao ndio tunaowaita kioo cha jamii ambao walimchukua binti huyu Lulu na kumuingiza katika mkumbo huo pasipo kumlinda, aliachwa huria akawa hashikiki na kuandikwa kwake magazetini sio kwa mema bali kwa mabaya anayoyatenda kukampa kichwa na kujiona yuko juu ya kila mtu.
Kwa yaliyotokea ingawa inasikitisha lakini hilo ni funzo kwetu kwamba tunahitaji busara na hekima ya hali ya juu sana katika kukuza vipaji vya watoto wetu.
Binti kama Lulu kwanza amelelewa na malezi ya upande mmoja, yaani kalelewa na mama yake tu ..na wakati bado akihitaji malezi ya karibu kutoka kwa mama yake, akavutwa na watengeneza filamu wa Bongo walioibuka kama uyoga .tamaa ya fedha na kutafuta rasilimali watu rahisi inamkumba binti huyu kwa kigezo cha kuwezeshwa kujiajiri ili apate kusoma kwa ustawi wa maisha yake na familia yake.
Binti huyu anafinyangwa kitabia na jamii hii ya waigizaji waliokimbilia cheap popularity baada ya kushindwa kuendelea na masomo au kufukuzwa shule kutokana na tabia zisizofaa.
Taaluma ya filamu hapa nchini haiongozwi na watu wenye taaluma hiyo, bali wababaishaji na watu walioshindwa maisha .na kutokana na ugeni wetu katika jambo hilo (Mkumbuke kwamba kwa takriban miaka 27 ya utawala wa chama kimoja tulikuwa hatujui TV ni kitu gani) tasnia hiyo ikajizolea umaarufu na ikawa ndio njia rahisi kwa wale wasio na elimu kujiingizia kipato si haba.
Hao ndio tunaowaita kioo cha jamii ambao walimchukua binti huyu Lulu na kumuingiza katika mkumbo huo pasipo kumlinda, aliachwa huria akawa hashikiki na kuandikwa kwake magazetini sio kwa mema bali kwa mabaya anayoyatenda kukampa kichwa na kujiona yuko juu ya kila mtu.
Kwa yaliyotokea ingawa inasikitisha lakini hilo ni funzo kwetu kwamba tunahitaji busara na hekima ya hali ya juu sana katika kukuza vipaji vya watoto wetu.