Mayai ya Kwale Yanauzwa

Mayai ya Kwale Yanauzwa

1800

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2010
Posts
2,215
Reaction score
611
Wadau habari!kwa wale wenye kuhitaji mayai ya Kwale yanapatikana hapa Dar es salaam,kwa bei ya 20,000 kwa tray,punguzo lipo kutokana na idadi ya tray utakazochukua,kwa mwenye kuhitaji anaweza kuni PM au apige namba hii 0713670026, Asanteni
 
sasa biashara gani mpaka kwa PM, weka namba zako hadharani watu tukupigie wee bana biashara inafanyika gizani ennhe
 
sasa biashara gani mpaka kwa PM, weka namba zako hadharani watu tukupigie wee bana biashara inafanyika gizani ennhe

Umesomeka mkuu,ninarekebisha
 
Mkuu mmepata vibari? Ingawa vibari ni ishu sana ila ushauri wangu fuatilia wizara, utapata na utakuwa huru,
 
Mkuu mmepata vibari? Ingawa vibari ni ishu sana ila ushauri wangu fuatilia wizara, utapata na utakuwa huru,

Mkuu huyu mdau anaeuza ndio yupo on process,kuna paper amepata huku akiendelea kufuatilia/kusubiria
 
mkuu mie natafuta hao kware jike na dume wanapatikana.ili nijianda kutafuta kibali cha maliasili
 
mkuu mie natafuta hao kware jike na dume wanapatikana.ili nijianda kutafuta kibali cha maliasili

Kwale wapo vifaranga,ila ni wachache sana,piga 0713784634
 
Mkuu kuna njia moka ya short cut kabisa ambayo hata mimi nilikuwa siijuia na ni wachache wanao ijua na kuna mdau mmoja ndo ananisadia kuputa kibari na kilikuwa kitoke this week ila jamaa wako 8 88 Dodoma
 
Mkuu kuna njia moka ya short cut kabisa ambayo hata mimi nilikuwa siijuia na ni wachache wanao ijua na kuna mdau mmoja ndo ananisadia kuputa kibari na kilikuwa kitoke this week ila jamaa wako 8 88 Dodoma

Embu ianike hapa mkuu kwa faida ya wadau wote,au inahitaji kuingia chemba (PM)
 
Wadau habari!kwa wale wenye kuhitaji mayai ya Kwale yanapatikana hapa Dar es salaam,kwa mwenye kuhitaji apige namba hizi 0713784634 na 0784784634
Mkuu imebidi nichimbuke mtandaoni nimeshuhudia biashara kubwa ya ufugaji wa ndege hawa nchi za wengine, nimekuta maelezo yanayoonesha ubora wa mayai ya kwale kuwa uko juu kuliko mayai ya kuku japo ni madogo kwa saizi na ni tiba ya msululu wa magonjwa ikiwamo kuongeza kumbukumbu na kuongeza nguvu za kijinsia (zile zinazotafutwa sana kwa waganga). Mkuu naomba nijuzwe mwamko na soko la Kwale hapa kwetu TZ hali ikoje watu tuanze kujiingiza huko??!!
 
Mkuu imebidi nichimbuke mtandaoni nimeshuhudia biashara kubwa ya ufugaji wa ndege hawa nchi za wengine, nimekuta maelezo yanayoonesha ubora wa mayai ya kwale kuwa uko juu kuliko mayai ya kuku japo ni madogo kwa saizi na ni tiba ya msululu wa magonjwa ikiwamo kuongeza kumbukumbu na kuongeza nguvu za kijinsia (zile zinazotafutwa sana kwa waganga). Mkuu naomba nijuzwe mwamko na soko la Kwale hapa kwetu TZ hali ikoje watu tuanze kujiingiza huko??!!



Mkuu ni kweli kabisa,hawa ndege mayai yao na nyama yao ni deal sana kwa nchi za Europe,Asia America yote south and north,kuna mdau aligusia pia hata India na South Africa mayai na nyama ya hawa ndege demand iko juu!kwa hapa East Africa,naona kama kawaida wenzetu Wakenya walishachangamkia fursa hiyo zamani sana na kwao biashara ya mayai ya kwale na nyama yake sio kitu kigeni tena maana mpaka kwenye ma supermarket yao vinauzwa,kama ujuavyo uzito unaotutawala Watanzania,wenzetu uanza na sisi ufuata,kwa hiyo kwa hapa kwetu soko la kwale na umuhimu wa mayai yake ndio limeanza kuchomoza,na hata kwenye maonesho ya nane nane kuna mdau alikua anauza mayai ya kwale na kwa kweli aliuza sana pale Morogoro!so kama unataka kuchangamkia fursa hiyo sio mbaya mkuu
 
Mkuu imebidi nichimbuke mtandaoni nimeshuhudia biashara kubwa ya ufugaji wa ndege hawa nchi za wengine, nimekuta maelezo yanayoonesha ubora wa mayai ya kwale kuwa uko juu kuliko mayai ya kuku japo ni madogo kwa saizi na ni tiba ya msululu wa magonjwa ikiwamo kuongeza kumbukumbu na kuongeza nguvu za kijinsia (zile zinazotafutwa sana kwa waganga). Mkuu naomba nijuzwe mwamko na soko la Kwale hapa kwetu TZ hali ikoje watu tuanze kujiingiza huko??!!

Mkuu ni kwamba hata huku kuna watu wanayahitaji sana hayo mayai na niliwahi kuwauliza baadhi ya watu fulani fulani, na kwa Arusha kuna watu hubidi waagize nje hayo mayai kwa kibari,

Ila Tatizo kubwa na kikazwa kikubwa ni Mali Asili, huwezi fanya biashara ya hawa ndege bila kibali, na hata unao wauzia hihitaji kibali chako wewe cha kuwafuga hawa ndege, so kikwazo kiko hapo,

Kuhusu ku export, kuna soko kweli nchi za nje kama China, japani, South Africa na kwingineko, Ila kwa Ku export kidogo napo kuna utata Mfano kwenye Nchi kama Japani na China ambazo zinaongoza kwa kula Kware wana Aina zao za Kware, Kware wanao fugwa Japani si sawa na wanao fugwa China, so sijui wa huku kwetu inakuwa vipi.

Kikwazo Namba moja ni Kibali, Na kwa Wizara ya Mali asili, Kibali cha kuuza hawa Ndege nje ni the same na kibali cha Kuuza wanyama poli hai nje ya Nchi, na wote tunajua Ugumu wa kupata kibali cha kuuza wanayama hai nje ya nchi, Kwa Nchi kama Kenya wao ile shirika lao la Wanya Pori KENYA WILDLIFE SERVICE huwa lina kitengo kabisa cha kuwasaidia wanao taka kufuga Hawa kware, Kanga na Mbuni, na mbuni wanafugwa sana Kenya na mayai yao yana soko kubwa sana nje ya nchi hasa Egg shell yake, N kwa wenzetu vibali vya kufuga haviko complicated kama Bongo.

Tanzania kuna Mlolongo wa kufa mtu nilijarubu siku moja na ule mlolongo kwa kifupi ni wa kuzuia watu wasifuge, kwa sababu huwezi niambia mimi leo kwamba kabla ya kupata kibali inabdi nifanye Epumbuzi wa kimazingira, niwe na mtu anagalau mwenye Certificate ya maswala ya wanyama, niwe sijui na nini, kuna mambo mengi plus fees ambayo iko interm of USD,

Ila kuna Mdau mmoja aliniambia altenative ya kupata kibali cha kuwafuga ndo nasikilizia hiyo njia ikiwa Ok nitawajuza kwa sasa siwezi kwa sababu ndo kwanza inafanyiwa kazi na kama ikifanikiwa niwajuza hiyo njia ambayo inaweza kuwa ni simple sana
 
Mkuu 1800 na Mkuu Chasha nawashukuru sana kwa kujali na kujibu swali langu. Mara baada ya kusoma thread hii niliingia kwenye mtandao, You tube, nikashuhudia ufugaji mkubwa huko Asia, yaani kwale wanafugwa kama utitiri! Ndipo nikaandika hapa kuulizia maana nilikuta hadi video clip ya mfugaji wa Kenya akilelezea faida ya mayai ya Kwale mbele ya banda lake. Lakini kama haitoshi nikasema hebu nisearch tena JF labda kuna thread nyingine ya Kwale, nikakutana na thread nyingine tena iliyoanzishwa na Mkuu 1800, ilibidi nikae vizuri nitulie maana kumbe hii kitu ilikuwa imeshaongelewa kwa kireeefu, na michango miingi, na mimi mara zote nilikuwa nikiangalia thread hii ya mayai ya kwale nilikuwa naipita tu, nilikuwa naona ni mzaha tu, hakika ukitaka kujua utamu wa ngoma ingia ucheze.

Pamoja na kumshukuru mleta thread hizi Mkuu 1800 na wachangiaji wengine wote kwa namna ya pekee nimpongeze sana Mkuu Chasha! Kweli Mkuu unamsuli imara katika kufuatilia ishu, umemwaga post nyingi kuhusu Kwale na kutoa uzoefu wako kadri nafasi ilivyokuruhusu na bado umeendelea kwa kirefu kunielimisha hapa! Mungu akuzidishie mafanikio kwa moyo wako wa kupenda kushea na waTz. Ila kusema kweli ishu ya vibali imenitia hasira na kujichukia kuwa Mtanzania, hakika walio nje ya Tanzania wanapotutazama watanzania nadhani tunaonekana kama tuko primitivu sana!

Wasomi wote watakaosoma maandishi yangu hapa watambue kuwa wengi wa wasomi Tz ni wasomi tu lakini hawajaelimika maana watu hawatumii elimu zao kuboresha maisha ya watanzania, wasomi wengi wanafanya kazi bila reasoning ya kitaaluma na kutumia common sense! Kwa mfano kuweka vibali vya ufugaji na biashara ya Kwale kundi moja na uzito uleule kama vibali vya simba hii ni nini? Kutoa vibali siyo ishu kama vibali hivyo vingekuwa vinapatikana kwa uwazi na uhakika, lakini kuweka utaratibu wa vibali usiotekelezeka, ambavyo undani wake ni kama hawataki mambo hayo yafanyike ni maendeleo gani haya!

Hata hivyo Mkuu Chasha inaelekea kuna ubaguzi na pengine ni mwendelezo wa tatizo letu sugu la rushwa Tz maana ninajiuliza yule aliyeleta Kwale kwenye maonyesho ya nane nane ujumbe wake kwa taifa ni nini iwapo vibali vyake haviwezi kupatikana?

Watanzania tunaweza kujivuna na kujipiga kifua sana tuwapo ndani ya nchi yetu kwamba tuko juu kwa hili na lile lakini ukitoka nje ya nchi ukichanganyika na watu wa mataifa mbali mbali unagundua wenzetu wako mbali sana. Nahisi nchi zote east africa Tz ndiyo ni usiku zaidi. Ndiyo maana kwa kuona hivyo Kenya, Uganda na Rwanda wameona watu-avoid waendelee na shirikisho lao maana ukitazama kuanzia janga la bandari ya Dar ni kwamba Tz bado tuko gizani sana. Simulizi lako la mizengwe ya vibali uliyoandika hapa Chasha umenilegeza kabisa najiona kama mtanzania bado siko huru!! Kenya wako mbali sana na kamwe tusijilinganishe nao sisi tulipouvaa ujamaa kisha tukautupa na kuanza upya wao tayari walishafika mbali sana kwenye kila jambo ndiyo maana wanaonekana wako aggresive sana kwenye business.
 
Mkuu 1800 na Mkuu Chasha nawashukuru sana kwa kujali na kujibu swali langu. Mara baada ya kusoma thread hii niliingia kwenye mtandao, You tube, nikashuhudia ufugaji mkubwa huko Asia, yaani kwale wanafugwa kama utitiri! Ndipo nikaandika hapa kuulizia maana nilikuta hadi video clip ya mfugaji wa Kenya akilelezea faida ya mayai ya Kwale mbele ya banda lake. Lakini kama haitoshi nikasema hebu nisearch tena JF labda kuna thread nyingine ya Kwale, nikakutana na thread nyingine tena iliyoanzishwa na Mkuu 1800, ilibidi nikae vizuri nitulie maana kumbe hii kitu ilikuwa imeshaongelewa kwa kireeefu, na michango miingi, na mimi mara zote nilikuwa nikiangalia thread hii ya mayai ya kwale nilikuwa naipita tu, nilikuwa naona ni mzaha tu, hakika ukitaka kujua utamu wa ngoma ingia ucheze.

Pamoja na kumshukuru mleta thread hizi Mkuu 1800 na wachangiaji wengine wote kwa namna ya pekee nimpongeze sana Mkuu Chasha! Kweli Mkuu unamsuli imara katika kufuatilia ishu, umemwaga post nyingi kuhusu Kwale na kutoa uzoefu wako kadri nafasi ilivyokuruhusu na bado umeendelea kwa kirefu kunielimisha hapa! Mungu akuzidishie mafanikio kwa moyo wako wa kupenda kushea na waTz. Ila kusema kweli ishu ya vibali imenitia hasira na kujichukia kuwa Mtanzania, hakika walio nje ya Tanzania wanapotutazama watanzania nadhani tunaonekana kama tuko primitivu sana!

Wasomi wote watakaosoma maandishi yangu hapa watambue kuwa wengi wa wasomi Tz ni wasomi tu lakini hawajaelimika maana watu hawatumii elimu zao kuboresha maisha ya watanzania, wasomi wengi wanafanya kazi bila reasoning ya kitaaluma na kutumia common sense! Kwa mfano kuweka vibali vya ufugaji na biashara ya Kwale kundi moja na uzito uleule kama vibali vya simba hii ni nini? Kutoa vibali siyo ishu kama vibali hivyo vingekuwa vinapatikana kwa uwazi na uhakika, lakini kuweka utaratibu wa vibali usiotekelezeka, ambavyo undani wake ni kama hawataki mambo hayo yafanyike ni maendeleo gani haya!

Hata hivyo Mkuu Chasha inaelekea kuna ubaguzi na pengine ni mwendelezo wa tatizo letu sugu la rushwa Tz maana ninajiuliza yule aliyeleta Kwale kwenye maonyesho ya nane nane ujumbe wake kwa taifa ni nini iwapo vibali vyake haviwezi kupatikana?

Watanzania tunaweza kujivuna na kujipiga kifua sana tuwapo ndani ya nchi yetu kwamba tuko juu kwa hili na lile lakini ukitoka nje ya nchi ukichanganyika na watu wa mataifa mbali mbali unagundua wenzetu wako mbali sana. Nahisi nchi zote east africa Tz ndiyo ni usiku zaidi. Ndiyo maana kwa kuona hivyo Kenya, Uganda na Rwanda wameona watu-avoid waendelee na shirikisho lao maana ukitazama kuanzia janga la bandari ya Dar ni kwamba Tz bado tuko gizani sana. Simulizi lako la mizengwe ya vibali uliyoandika hapa Chasha umenilegeza kabisa najiona kama mtanzania bado siko huru!! Kenya wako mbali sana na kamwe tusijilinganishe nao sisi tulipouvaa ujamaa kisha tukautupa na kuanza upya wao tayari walishafika mbali sana kwenye kila jambo ndiyo maana wanaonekana wako aggresive sana kwenye business.

Mkuu ni kweli kabisa, Viongozi wetu wana mawazo ya kizamani sana, na sijajua hizo Ajira milion 1 zinapatikana vipi kwa staili hii,

Mfano mwingine ni Mbuni, Mayai ya mbuni hasa ile shell yake ina soko la kbwa sana nje ya nci kwa kwenda kutngenzea mapambo inachorwa chorwa na kuuzwa, na nchi kama South Africa wanawafuga sana na hata kenya, Huku Bongo wanaweza kuhusisha na ucawi ukianza kufuga Muni
 
Mkuu imebidi nichimbuke mtandaoni nimeshuhudia biashara kubwa ya ufugaji wa ndege hawa nchi za wengine, nimekuta maelezo yanayoonesha ubora wa mayai ya kwale kuwa uko juu kuliko mayai ya kuku japo ni madogo kwa saizi na ni tiba ya msululu wa magonjwa ikiwamo kuongeza kumbukumbu na kuongeza nguvu za kijinsia (zile zinazotafutwa sana kwa waganga). Mkuu naomba nijuzwe mwamko na soko la Kwale hapa kwetu TZ hali ikoje watu tuanze kujiingiza huko??!!


Topic nzuri, ila siwafahamu hawa kwale naomba link niwaone, asante
 
Topic nzuri, ila siwafahamu hawa kwale naomba link niwaone, asante

Wanafanana sana na kuku tuwafugao majumbani, ila wao hawana rangi nyingi, asilimia kubwa sana wana rangi moja na size hutofautiana kidogo toka sehemu moja na nyingine. Ni kuku waliokataa kukaa mjini.
 
mmmmh! kweli hii ni JF!!!!!!! nawaheshimu wote kwa hili, kifupi mm nimgeni kidogo kwenye masuala ya ufugaji kwa maana sijapata kufuatilia mambo zaidi ya haya ya vibali, ila kiukweli napenda sn kufuga hasa Kuku na ndege wote kiujumla, ila kweli sheria zetu zipo hovyo wangetoa vbali wengi tungejiajiri na tungepata maendeleo yetu na ya taifa kwa ujumla! nadhan kuna haja ya kubadilisha hizi sheria mm naona walizuia sn zamani coz kam wangeruhusu sn zamani kweli ndege hawa wangeisha au wange kuwa lulu zaidi ya leo, yani matumizi yangezidi uwezo wa wao kuzaliana. kwa ujio na upatikanaji wa incubator machine sasa ingefika wakat wangekuwa kama kuku tuu watu wanzalisha na kuuza kwa biashara kuliko kuwaweka ndege katka kundi 1 na vibali vya wanyama pori! ndio wabunge tunaowachagua wayajue haya na kuweza kutunga sheria za kubadilisha mambo ya msingi kama haya kwa tija ya wananchi na Taifa!
 
Mkuu vipi mayai bado yapo?nilikua nasoma faida za quails eggs kimataifa,dah ukweli haya mayai ni muhimu sana kwa afya zetu,je kama bado yapo tray moja unauzaje mkuu?na unapatikana wapi?
 
Mkuu vipi mayai bado yapo?nilikua nasoma faida za quails eggs kimataifa,dah ukweli haya mayai ni muhimu sana kwa afya zetu,je kama bado yapo tray moja unauzaje mkuu?na unapatikana wapi?

Mayai yapo mkuu,ni Tsh 20,000/= kwa tray,ni affordable kabisa,maana kwenye maonesho ya nanenane Morogoro walikua wanauza 3,000/= kwa moja!mayai yapo Dar,ila kama unataka tray zaidi ya tano nijulishe mapema
 
Ungetuwekea picha maana wengine hata hatujui kwale wanafananaje.
 
Back
Top Bottom