Wakati natoka Zenji leo kwenye boti nilikaa na mdada mmoja,mara ya kwanza ni kama anajishuku kunisemesha mi namcheki tu,tulipokaa vizuri akatoa noti ya sh 2000/= imeungua moto upande,akaniambia,'kaka nimeshikishwa hii noti bila kujua,nawezaje kuitoa?
Nikamwambia nenda kanunue chochote humu ndani watapokea tu,basi akarudi na chipsi zile zilizokaushwa na pili pili kibao.
Akaniambia kaka karibu tule ila pili pili nyingi sijui kama utaweza,unajua sometimes mtu akikukaribisha basi hata kuonja usimvunje moja,nikaonja.
Dah ndo ikawa kuonja onja,mara "kaka sijui hi chipsi itaishaje furaha yangu tule iishe maana ina pilipili"
Tukaendelea mdogo mdogo,mara "unakunywa soda gani siyo vizuri maana naona yenyewe kama haiendi" dah sasa hiyo lafudhi,aliporudi nikamwuliza we kabila gani,akaniambia mi mnyamwezi kwetu Ulyankulu Tabora.
Mara kasinzia gafla kaniwekea mkono,nilisisimka mwili na ninavyopenda black beauties,'memory ikanijia nikachukua ticket ya Azam nikaigeuza nikasoma makosa kwa wasafiri nikasoma namba 10 "(kufanya mapenzi fidia ni sh 50,000)"
Nikasimama,mara akagutuka "kaka sijui ndugu zangu watanipokea kweli sina uhakika" nikamwambia usijali wanaweza kwepo tu.
Sasa wakati Wa kutoka tukajikuta tumebaki wa mwisho.
Wakuu inaonekana Mnyamwezi ni wife material wanajali wanaume,wenye uzoefu please!