Magulumangu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 3,047
- 452
Kuandamana siwezi,nguvu ya uma mi sina,
Kama vina huviwezi,heri kuwa maumuna,
Malengaze kuwa enzi,nipe jamvi wetu mwana,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
Mzee Mwanakijiji,bonyeza hicho kitufe,
Poromosha kama uji,nipe tafu sije nife,
Masanilo mchungaji,Lukansola mwana ife,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
Sugu wetu malaria,Aspirini dawa yake,
Babukijana silia,unga mkono babake,
Quinine sijetupilia,Field masha iwe mwake,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
mapenzi yalifuata,malenga walikuwepo,
mapicha mmeyafunta,Cereb kama upepo,
Inteligenti majita,siasa jukwaa lipo,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
byashara nayo spoti,malenga mmemnyonga,
elimu lugha si sapoti,eti ndani ya malenga,
utani sheria chati,dokita wote wachanga,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
La kitaifa jukwaa,hapo nakufagilia,
utaifa haujakwaa,malenga sikilizia,
malenga wote imezaa,kamwe sijakadiria,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
najua tupo wengi,vina kuvipangilia,
msukuma hata mangi,unguja vilianzia,
musoma na usangi,ujiji nakuhadhithia,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
Kama vina vinagoma, Lizzy atakufundisha,
karamu haitagoma,hata uanzie insha,
usinitupe harama,mwenzio nimeshaisha,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
hapa ndipo mwisho wangu,nipe jukwaa nichane,
najifisha sina kwangu,leo huku kama chane,
nipe nichane mawingu,hata usiku manane,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
Kama vina huviwezi,heri kuwa maumuna,
Malengaze kuwa enzi,nipe jamvi wetu mwana,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
Mzee Mwanakijiji,bonyeza hicho kitufe,
Poromosha kama uji,nipe tafu sije nife,
Masanilo mchungaji,Lukansola mwana ife,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
Sugu wetu malaria,Aspirini dawa yake,
Babukijana silia,unga mkono babake,
Quinine sijetupilia,Field masha iwe mwake,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
mapenzi yalifuata,malenga walikuwepo,
mapicha mmeyafunta,Cereb kama upepo,
Inteligenti majita,siasa jukwaa lipo,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
byashara nayo spoti,malenga mmemnyonga,
elimu lugha si sapoti,eti ndani ya malenga,
utani sheria chati,dokita wote wachanga,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
La kitaifa jukwaa,hapo nakufagilia,
utaifa haujakwaa,malenga sikilizia,
malenga wote imezaa,kamwe sijakadiria,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
najua tupo wengi,vina kuvipangilia,
msukuma hata mangi,unguja vilianzia,
musoma na usangi,ujiji nakuhadhithia,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
Kama vina vinagoma, Lizzy atakufundisha,
karamu haitagoma,hata uanzie insha,
usinitupe harama,mwenzio nimeshaisha,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,
hapa ndipo mwisho wangu,nipe jukwaa nichane,
najifisha sina kwangu,leo huku kama chane,
nipe nichane mawingu,hata usiku manane,
Maxence nakuomba,nipe na mimi uwanja,