Max Rioba adai ameshindwa kufanya kazi na Young Dee Kwa kuwa hana Nidhamu

Wana muda kwenye hiyo Label?

Wamesaidiwa vipi kujitangaza na kusikika?
Mbona kila siku anasikika Young D tu?
Unaweza kunitajia ngoma zako kali zinazoelewaka hao uliowataja hapo juu?

Unaniuliza unamjua fulani unamjua fulani kwanini ukuniuliza kama namjua Young D?
Kwanini Hao unaonilazimisha niwajue hawapo hata kwenye nusu ya level za Young D?
Ukijiuliza hivyo utajua kuna shida mahali.

Vitu vingine havikwepeki na huwezi kutumia nguvu kubwa kuvikwepa labda kuwe na tatizo mahali.
Wewe kama nani mpaka umpangie Max muda wa kusign wasanii awatakao?
Unamsaidia hata majani ya chai??
Sasa usipangie watu cha kufanya huo ni ushamba kiwango cha changarawe,
Sasa skiza, Ukimtoa Young D, wasanii wote waliobaki akiwemo Max( max nae ni msanii wa mdb kama ulikuwa hujui) huimba pamoja, so lile ni kundi kama unavyoona Yamoto, Yeye ndio ameamua iwe ivyo, wasanii wengine wawe wanatoa nyimbo kwa kundi alafu wengine wawe wanaimba kote( solo & group)
Na kuhusu nyimbo zao nimeshazitaja nyingi tu, ila kwakuwa wewe sio mfuatiliaji wa muziki basi baki na Ujinga wako,
kwanza MZARAMO NA MUZIKI WAPI NA WAPI, bro hii sio singeli.
 
Hapa ndio JF, Hadanganywi mtu
Safi sana kwa kuja maana wabongo siku hizi mtu humfahamu kiundani lakini mtu anavyo muongelea kama vile anamjua sana na siki hizi kuita watu mapunga bila ushahidi ndiyo fashion.
Asante kwa kutuhabarisha
 
Safi sana kwa kuja maana wabongo siku hizi mtu humfahamu kiundani lakini mtu anavyo muongelea kama vile anamjua sana na siki hizi kuita watu mapunga bila ushahidi ndiyo fashion.
Asante kwa kutuhabarisha
Tupo pamoja mkuu
 
Mbongo mpe kichwa cha Habari tu,,,kwa kuunganisha Dots tu hatujambo.



Chai nyiiingi kila mtu anamjua mtu.
 
Nimesikitika kuona huyu huyu max leo hii anapata kashfa kisa dee,.....na sitoshangaa akirudia tena kumsaidia. Max anamchukulia dee zaidi ya msanii, anamchukulia kama mdogo wake kabisa ndiyo maana anaumia sana kumuona dee vile
Mkuu tatizo watu humu wako very +ve,wanawaza vitu vya ajabu ajabu tu,wengine wanaenda mbali zaidi na kusema kuna uhusiano wa kishoga
 
Wallah tena huu uhusiano wa Young D Na Max sio uhusiano wa mtu Na meneja wake kuna kitu kikubwa sana nyuma yao.

Young D alivyotoka kwa Lamar akachukuliwa Na Max toka wakati huo Max Na Lamar wana bifu huku Young D Na Lamar picha haziendi kabisa.

Na ugomvi wa Max Na Young D umefumuka baada ya Young D kurudiana Na Tunda...Kinachoonekana Max anachukizwa Young D akiwa kwenye mahusiano Na wasichana.

Kingine cha kujiuliza kwanini hiyo Label ya Max iwe na msanii mmoja tu miaka yote?!
Kwanini hakuna wasanii wengine zaidi ya Young D?
Kwanini Max anamwaga mpaka machozi kumlilia Young D?!

Maswali ni mengi muda ni mchache
 
Back
Top Bottom