Steven mushi mushi
JF-Expert Member
- Jul 25, 2016
- 533
- 741
Hii tabia ya wifi kuingilia ndoa za ndugu zao na kuleta mtafaruku ambao wakati mwingine kupelekea kwa ndoa nyingi kuvunjika inazidi kushamiri kila uchao.
Utakuta hawa mawifi ndo chanzo cha migogoro katika ndoa nyingi na wakati mwingine kuwapangia ndugu zao kipi wawafanyie na kipi wasiwafanyie wake zao na wakati mwingine kuanzisha matabaka kwa kumpenda mke wa ndugu flani na kumtenga mke wa ndugu mwingine kwasababu sisizo za msingi, kwa mfano utakuta wanamchukia mke wa ndugu flani kutokana na either mmewe anampenda sana au kwasababu hapendi kuwaskiliza wao.Utakuta mtu anapendana na anaishi vizuri na mke wake lakini mawifi wanaanza kutafuta maneno kwa ajili ya kuwatenganisha na wakati mwingine mwanaume usipokuwa makini basi utakuta ndoa yako inasambaratika.
Dada zangu chonde chonde hebu badilikeni kama ndugu yako ana mke wake na wanapendana waache waishi kwa amani kwani wamechaguana wao na sio kuanza maneno yasiyo na tija mara sijui huyu hapa kwetu anatujazia tu choo, mara ni mvivu, mara sijui lazima tumkomoe kwa kumchonganisha na mmewe kwasababu tangia aje hapa kwetu upendo wa ndugu yetu umepungua kwetu au yeye ndo anapendwa zaidi na sababu nyingine sisizo na msingi ambazo mwishowe husababisha ndoa kuwa na mgogoro na wakati mwingine hata kuvunjika.
Na sisi wanaume kama umeoa ishi kwa upendo na mkeo mjenge maisha yenu na sio kuanza kusikiliza maneno ya uchonganishi kwa mkeo kutoka kwa baadhi ya ndugu na wazazi maana baadae utajajuta na ikumbukwe kuwa ndoa ni ya wawili na usikubali ndugu au wazazi kuingilia ndoa yenu kwasababu zao binafsi na uwe makini na maneno yanayoweza kukuchonganisha na mwenza wako kutoka either kwa wazazi, ndugu, jamaa na marafiki na ukumbuke huyo ni mkeo uliyemchagua na ni jukumu lako kumlinda na kumtunza.
Utakuta hawa mawifi ndo chanzo cha migogoro katika ndoa nyingi na wakati mwingine kuwapangia ndugu zao kipi wawafanyie na kipi wasiwafanyie wake zao na wakati mwingine kuanzisha matabaka kwa kumpenda mke wa ndugu flani na kumtenga mke wa ndugu mwingine kwasababu sisizo za msingi, kwa mfano utakuta wanamchukia mke wa ndugu flani kutokana na either mmewe anampenda sana au kwasababu hapendi kuwaskiliza wao.Utakuta mtu anapendana na anaishi vizuri na mke wake lakini mawifi wanaanza kutafuta maneno kwa ajili ya kuwatenganisha na wakati mwingine mwanaume usipokuwa makini basi utakuta ndoa yako inasambaratika.
Dada zangu chonde chonde hebu badilikeni kama ndugu yako ana mke wake na wanapendana waache waishi kwa amani kwani wamechaguana wao na sio kuanza maneno yasiyo na tija mara sijui huyu hapa kwetu anatujazia tu choo, mara ni mvivu, mara sijui lazima tumkomoe kwa kumchonganisha na mmewe kwasababu tangia aje hapa kwetu upendo wa ndugu yetu umepungua kwetu au yeye ndo anapendwa zaidi na sababu nyingine sisizo na msingi ambazo mwishowe husababisha ndoa kuwa na mgogoro na wakati mwingine hata kuvunjika.
Na sisi wanaume kama umeoa ishi kwa upendo na mkeo mjenge maisha yenu na sio kuanza kusikiliza maneno ya uchonganishi kwa mkeo kutoka kwa baadhi ya ndugu na wazazi maana baadae utajajuta na ikumbukwe kuwa ndoa ni ya wawili na usikubali ndugu au wazazi kuingilia ndoa yenu kwasababu zao binafsi na uwe makini na maneno yanayoweza kukuchonganisha na mwenza wako kutoka either kwa wazazi, ndugu, jamaa na marafiki na ukumbuke huyo ni mkeo uliyemchagua na ni jukumu lako kumlinda na kumtunza.
