Mawifi ni noma! wiki hii kulitokea msiba wa mtu wa dola, ni mzaliwa wa mkoa wa Mara, walienda kuzika na jana mjane amerudi town, niliguswa kwenda kumpa pole kama jirani yangu. wakati tunaongea akaniambia kuwa kumbe wakati mumewe amezidiwa dada yake alimshawishi kaka yake (marehemu) amkabidhi hati ya nyumba, hivyo walipokuwa kwenye kikao cha ukoo baada mazishi alishangaa kuona wifi yake anasema "hati ya nyumba hii kaka alinipa alivyokuwa anaumwa, alisema kuwa ana wasiwasi akifariki unaweza kuuza nyumba". duuuuuuuuu ! hao ndio mawifi