Tanzania imetawaliwa na CCM, kwa miongo yote Hadi hivi Sasa! Maendeleo yapo ingawa siyo yaliyotarajiwa kufikiwa hadi sasa iwapo CCM kwa miongo hiyo yote ingekwepa Vita ya Uganda, Ukombozi wa Nchi za Afrika, Ufisadi, Uzembe kazini, uuaji wa Viwanda na mengineyo!
Kwa Sasa vyama vya upinzani vinapambana kushika hatamu. Na anayeongoza mapambano hayo Ni Chadema!
Kwa akili za mtu wa kawaida lazima ajaribu kujenga picha ya Hali inavyoweza kuwa iwapo Chadema atachukua Serikali
Haya Ni baadhi ya maono yangu.
1. Ujenzi wa miundombinu utaongezeka, ingawa si kwa kasi ya Magufuli, na hasa kwa awamu ya kwanza
2. Ufisadi holela utapungua utabakia ule wa mapapa
3. Mifumo ya majeshi yote itabadilika kidogo, hasa kutokana na mabadiliko makubwa wa viongozi wote wa majeshi
4. Uchawa wa watumishi wa serikali na raia utaendelea. Kadi za CCM za watumishi na maafisa mbalimbali zitatupwa na kadi za Chadema zitachukuliwa
5. Katiba haitabadilishwa
6. Wabunge wa CCM watatoa nondo kalikali bungeni, wakati huo wabunge wa Chadema watakuwa vilaza
7. Wabunge wa CCM baadhi yao wataunga juhudi za Chama tawala Cha Chadema
8.Mahakama na jeshi la polisi litakuwa watetezi wa Chadema
9. Mwamko wa maendeleo utapanda juu kwa kiwango kidogo hasa kwa awamu ya kwanza ya utawala, na maendeleo yataendelea kuzorota kwa awamu zinazoendelea ( Kumbuka Africa is Africa)
10. Mikataba mingi serikalini itafumuliwa hasa kutokana na ukweli kwamba imebeba maslahi ya watawala wa CCM
11. Mali nyingi za CCM zitataifishwa na kupelekwa serkalini
12. Muungano utatengenezwa upya, na tunaweza kushuhudia kila upande unaondoka na mbao zake (kitu ambacho si kibaya)
Hayo Ni baadhi ya ninayoyafikiri juu ya Tanzania ya Chadema
Wewe je, unaitazamaje Tanzania ya Chadema?
Weka uchama pembeni tumia akili yako binafsi isiyoongozwa na chuki au uchawa kwa CCM.
Kwa Sasa vyama vya upinzani vinapambana kushika hatamu. Na anayeongoza mapambano hayo Ni Chadema!
Kwa akili za mtu wa kawaida lazima ajaribu kujenga picha ya Hali inavyoweza kuwa iwapo Chadema atachukua Serikali
Haya Ni baadhi ya maono yangu.
1. Ujenzi wa miundombinu utaongezeka, ingawa si kwa kasi ya Magufuli, na hasa kwa awamu ya kwanza
2. Ufisadi holela utapungua utabakia ule wa mapapa
3. Mifumo ya majeshi yote itabadilika kidogo, hasa kutokana na mabadiliko makubwa wa viongozi wote wa majeshi
4. Uchawa wa watumishi wa serikali na raia utaendelea. Kadi za CCM za watumishi na maafisa mbalimbali zitatupwa na kadi za Chadema zitachukuliwa
5. Katiba haitabadilishwa
6. Wabunge wa CCM watatoa nondo kalikali bungeni, wakati huo wabunge wa Chadema watakuwa vilaza
7. Wabunge wa CCM baadhi yao wataunga juhudi za Chama tawala Cha Chadema
8.Mahakama na jeshi la polisi litakuwa watetezi wa Chadema
9. Mwamko wa maendeleo utapanda juu kwa kiwango kidogo hasa kwa awamu ya kwanza ya utawala, na maendeleo yataendelea kuzorota kwa awamu zinazoendelea ( Kumbuka Africa is Africa)
10. Mikataba mingi serikalini itafumuliwa hasa kutokana na ukweli kwamba imebeba maslahi ya watawala wa CCM
11. Mali nyingi za CCM zitataifishwa na kupelekwa serkalini
12. Muungano utatengenezwa upya, na tunaweza kushuhudia kila upande unaondoka na mbao zake (kitu ambacho si kibaya)
Hayo Ni baadhi ya ninayoyafikiri juu ya Tanzania ya Chadema
Wewe je, unaitazamaje Tanzania ya Chadema?
Weka uchama pembeni tumia akili yako binafsi isiyoongozwa na chuki au uchawa kwa CCM.