Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi,
Nimewahi kuzungumzia baadhi ya kauli za rais wetu Mhe. Dr. John Pombe Magufuli kuwa ni kauli za vitisho, kibabe na kidikiteta, ambapo kauli ya leo ni hii ya kuwatisha baadhi ya mawaziri na makatibu watakaosika kulalamikia fedha za ndogo za OC (other charges) zinazopelekwa kwenye wizara zao ni ndogo na hazitoshi!, amewaambia wale wotewanaoona fedha wanazopewa ni ndogo na haziwatoshi, waache kazi!, amesema kuna watu wanalalamika!, anasema ametuma 'watu' wawarekodi walalamika hao, akipata tuu ushahidi, kuwa ni kweli wanalalamika, then atawatimua kazi!.
Hili limekaaje?!. Hii sio kauli ya vitisho, kuwa watendaji hawa wakuu?!, yaani kiasi chochote watakachopewa na serikali, no matter ni kidogo kiasi gani, hawaruhusiwi kucomment chochote bali wapokee na kunyamaza kimya!.
Huku si ni kuwafunga midomo mawaziri na makatibu wakuu wao?!, kitendo cha rais kesema amewatumia 'watu' wawarekodi, ni uthibitishoa usiotia shaka kuwa freedom of "expression is at crossroad!". Hii inaitwa suppressing opinion za mawaziri, makatibu wakuu na watendaji wakuu, ambazo ndizo hatua za awali za viongozi wote madikiteta duniani, hutoa kauli za kuwafanya waogopwe!. Ukiona mwenzako ananyolewa, wewe anza kutia maji tia maji, stage ya pili haiwezi kuwa ni kwenye media?!.
Tanzania yetu hii kusema ukweli madudu yalizidi, kiasi kwamba tukafika mahali nchi yetu ilihitaji kiongozi mwenye traits za udikiteta ili mambo yaende!. Mungu kasikia kilio cha Watanzania, katupatia rais Dr. John Pombe Magufuli, ambaye ni benevolent dictator, Watanzania tupewe nini tena?!.
Paskali
Nimewahi kuzungumzia baadhi ya kauli za rais wetu Mhe. Dr. John Pombe Magufuli kuwa ni kauli za vitisho, kibabe na kidikiteta, ambapo kauli ya leo ni hii ya kuwatisha baadhi ya mawaziri na makatibu watakaosika kulalamikia fedha za ndogo za OC (other charges) zinazopelekwa kwenye wizara zao ni ndogo na hazitoshi!, amewaambia wale wotewanaoona fedha wanazopewa ni ndogo na haziwatoshi, waache kazi!, amesema kuna watu wanalalamika!, anasema ametuma 'watu' wawarekodi walalamika hao, akipata tuu ushahidi, kuwa ni kweli wanalalamika, then atawatimua kazi!.
Hili limekaaje?!. Hii sio kauli ya vitisho, kuwa watendaji hawa wakuu?!, yaani kiasi chochote watakachopewa na serikali, no matter ni kidogo kiasi gani, hawaruhusiwi kucomment chochote bali wapokee na kunyamaza kimya!.
Huku si ni kuwafunga midomo mawaziri na makatibu wakuu wao?!, kitendo cha rais kesema amewatumia 'watu' wawarekodi, ni uthibitishoa usiotia shaka kuwa freedom of "expression is at crossroad!". Hii inaitwa suppressing opinion za mawaziri, makatibu wakuu na watendaji wakuu, ambazo ndizo hatua za awali za viongozi wote madikiteta duniani, hutoa kauli za kuwafanya waogopwe!. Ukiona mwenzako ananyolewa, wewe anza kutia maji tia maji, stage ya pili haiwezi kuwa ni kwenye media?!.
Tanzania yetu hii kusema ukweli madudu yalizidi, kiasi kwamba tukafika mahali nchi yetu ilihitaji kiongozi mwenye traits za udikiteta ili mambo yaende!. Mungu kasikia kilio cha Watanzania, katupatia rais Dr. John Pombe Magufuli, ambaye ni benevolent dictator, Watanzania tupewe nini tena?!.
Paskali