..Mawaziri saba watoswa.....

 
Matatizo ya CCM na serikali yake si matatizo ya mtu mmoja mmoja.Hata Lowassa alionewa tu kwani tangu aondolewe na kuwekwa Pinda kuna nini kimebadilika?Halafu Nape ana ugomvi gani na Chiza?Kwenda kutembelea Ruvuma ukiwa huna pesa wala majibu kwa matatizo ya wakulima itasaidia nini?Wao wote ni CCM kwa nini wasiitane na kuhojiana badala ya kupanda majukwaani na kupakana matope?Ukichunguza hapa utagundua wizara kama ya kilimo ni wizara za kiutendaji zaidi sasa serikali isipoinject pesa za kutosha huko ni lazima waziri aonekane "mvaa tai".Na hata hawa akina engeneer Chiza ni watu ambao historically ni watendaji kuliko wanasiasa.Usipowawezesha kufanya kazi zao hautawasikia kwenye porojo za kisiasa watakaa kimya tofauti na akina Wassira.Hivi ni watu wangapi wamepita pale kilimo?wamefanya nini tofauti na Chiza?wangapi wamepita pale elimu?wamefanya nini tofauti na Kawambwa?Nape kabla hujawavaa mawaziri,mwambie tu na aliyewateua kuwa yeye pia na chama chake ni mzigo mzito kwa taifa na hata hao mawaziri chama chao na ukiritimba wake ni mzigo mzito kwao!wanaogopa kusema tu ngoja tuwasaidie!kwa hiyo kama kujiuzulu ulipaswa kuanza wewe,na Kinana na mwenyekiti wenu!acha unafiki na sifa za kijinga.Msifikiri watanzania bado ni wale wale unaoweza kuwapulizia maskioni wakaanza kucheka kwa starehe ya kupuliziwa maskio huku ukiingiza vidole kwenye mifuko yao uwaibie no!no!no!matatizo ya serikali hii ni collective responsibility ya CCM.Anza wewe Nape kujiuzulu.
 
Kitu kinachonifanya niwachukie wabunge kuwa mawaziri ni kwamba,wabunge wetu wote ni wanasiasa,"much talkative"less action,wengi wapo hapo muda mrefu wakila vinono,si rahisi kufahamu changamoto zilizopo mezani kwa sasa,infact wamelewa sifa na fedha"


Mengine yanabaki kuwa maneno ya kupeana matumaini hewa!!!!!
Hapa ndipo penye shida; mawaziri hawatakiwi kuwa wabunge wala kuwa na uhusiano karibu na vyama
 
Baada ya hapo nimesikia vibaka wa buku 7 Lumumba wanajiandaa kuja na threads nyingi kwamba CCM ni mfano wa kuigwa kwa kufanya maamzi magumu. Hebu watazame jinsi wanavyojipanga kuleta umbeya!!
Hahaaa nimecheka sana, namuona Simiyu yetu kavua shati pale...
 
sasa huu umekuwa mchezo wa kuigiza yaani kila kukicha baraza la mawaziri linararuliwa na kuunda jipya sasa hii tafsiri yake nini, ina maana hapo ile sera ya chama kwanza mtu baadae ndo madhara yake haya sasa
 
Hv kuna waliobaki ccm wanafaa kuwa mawaziri..!? Kwa waliobaki hata profesa majimarefu ataukwaa uwaziri. Kwa muda mfupi karibu wabunge wote wasomi ndani ya ccm wamejaribiwa kuwa mawaziri.
 
Hivi baraza la Mawaziri wanafanya vikao mara ngapi kwa mwaka, mwezi au week? Na je katika vikao hivyo huwa mawaziri au makatibu wakuu huwa wanatoa taarifa za utendaji wa wizara zao? Na je JK huwa analizika na taarifa hizo?
Tatizo kubwa hapa ni JK ndo wakuajibishwa wa kwanza kama CC muna ubavu. Baba kiguu na njia kila Siku hata hajui maendeleo ya watoto wake shuleni (mawaziri)
 
ukiona mtoto wa jirani amekutukana ujue si bure ametumwa na mzazi wake. Nape amepata wapi ujasiri wa kumsema Kawambwa tena wazi wazi? Hili nalo ni picha jingine nataka kuona mwisho wake, je JK ataweza kuwatosa watoto wa kwao? Na je kama waliokuwepo wote akili zao zimedumaa, nani ataweza kuziba mapengo hayo yaliyojitokeza?
 
Haya sasa Jk anakaribishwa kuzungumza msibani, ngoja tuone hapa.......
 
Wana majembe kibao, Mfn. Komba, Nkamia na wengine wengi.
 
Hata wafanyeje, hiki chama kishaoza wala hakinunuliki!!!!!!
 

Sababu za kuwajibishwa ziambatane na ushahidi wa wazi.
 


- Kichwa cha habari na habari yenyewe ni vitu viwili tofauti na ndilo gazeti kuu la wenzetu huko upande wa pili, vipi Kapuya viliishia wapi?

Le Mutuz
 
Hapa hakuna kitakachofanyika, hiyo ndiyo imetoka tena. Unaposema Chama cha Mapinduzi kinatoa maagizo ya utekelezaji kwa serikali una maana gani wakati boss wa chama ndiye huyo huyo boss wa serikali. Kwa tafsiri rahisi ni kwamba Mwenyekiti wa CCM Mh. Jakaya kikwete anatoa maagizo ya utekelezaji kwa serikali inayoongozwa na Mh. Jalaya Kikwete it doesn't make sense. CCM na Serikali ni taasisi mbili tofauti na lazima ziongozwe na watu wawili tofauti ili kuwe na uwajibikaji na kwamba ikiwezekana Mwenyekiti wa chama amuwajibishe Rais wa nchi. Nchi hii ndivyo ilivyo unaweza kukuta Mwenyekiti wa shirika fulani ndiye huyo huyo mtendaji mkuu wa shirika hilo hilo, uwajibikaji uko wapi na nani ana wajibika kwa nani. Majanga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…