Mawaziri, RC na DC acheni hizi tabia

Nduka Original

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
1,012
816
Kuna tabia za viongozi wetu zinatia mauzi sana hapa Tanzania. Hawa mabwana wana tabia za kutopokea simu wala kujibu message. Unajuwa siyo mjifanye nyie ndio mko busy sana hata simu za wapiga kura wenu tena hamtaki kuzipokea. Mimi siyo mjinga ninanyue simu nikupigie simu wewe waziri, DC au RC kama sina kitu cha maana. Ndiyo maana productivity inakuwa mbovu katika shughuli zenu kwasababu mnakosa inputs za stake holders etc.

Mimi nafikiri si ustarabu kabisa na lazima mbadilike.
Na cha ajabu hii tabia huwa mna anza baada ya kuapishwa kabla ya hapo wala hamna shida tena ukibipiwa tu unapiga
 
Wapokee simu yako ya nini? Wewe si ulimuuzia kura yako na yeye alikulipa pombe au khanga, T-shirt au kofia ya kijani na njano, sasa biashara mlisha ifanya na mkamalizana, simu tena kwake ya nini? Huna thamani tena kwake, alichokitaka kwako alishakipata, waacheni watoto wa watu wale nchi! Sana sana usubiri hadi july 2015 hapo watakuwa tayari kupokea simu zako na sio sasa!
 
Back
Top Bottom