Mawasiliano ni nguzo ya mapenzi bora

Daby

JF-Expert Member
Oct 26, 2014
33,648
75,737
Mawasiliano/communications.

Hili ni jambo tunalolipuuzia saana tunapokuwa katika mahusiano ya kimapenzi. Aidha ndoa nyingi au mahusiano mengi yamevunjika tu kwa aidha mwanandoa mmoja au wote kupuuzia mawasiliano au kumshirikisha mwenzi wake japo dogo alilonalo moyoni, ambalo lingeweza kumalizwa na mazungumzo.

Unapokuwa na tatizo na mwenza wako ukalificha.. kutomshirikisha kutaleta athari kubwa na hautajua imesababishwa na kutokuwepo kwa mawasiliano kwasababu unayapuuza.

Kwenye mahusiano kuna matatizo ya kuhisi kusalitiwa, matumizi ya pesa, kutokuridhika katika mapenzi, kudharauliwa, kutokushirikishwa katika maamuzi n.k. haya yote njia rahisi ya kuyamaliza ni [mawasiliano] kukaa chini na kuyazungumza na mwenzi wako na sio kuyaweka moyoni siku ukiudhika uyaseme kama malalamiko.

Mawasiliano yanapokuwepo baina ya wapenzi.... yaanasaidia kuaminiana, kuheshimiana, kusikilizana na kuvumiliana. Wewe dada mmeo/mwenza wako alipokukera ulimwambia kwa utaratibu baadae kuwa hubby ulinikera naomba tuyamalize? Au umeliweka moyoni siku akikukanyaga umkumbushie kwa kulia?

Wewe mwanamme mpenzi wako alipohisi unamcheat ulimkalisha chini mkayamaliza kila mmoja akabaki na amani pasipo na hisi hasi?

Tupende kuwasiliana katika mapenzi.... tutaboresha mahusiano yetu kwa ujenzi wa familia bora.

asalaaam.
 
Mawasiliano/communications.

Hili ni jambo tunalolipuuzia saana tunapokuwa katika mahusiano ya kimapenzi. Aidha ndoa nyingi au mahusiano mengi yamevunjika tu kwa aidha mwanandoa mmoja au wote kupuuzia mawasiliano au kumshirikisha mwenzi wake japo dogo alilonalo moyoni, ambalo lingeweza kumalizwa na mazungumzo.

Unapokuwa na tatizo na mwenza wako ukalificha.. kutomshirikisha kutaleta athari kubwa na hautajua imesababishwa na kutokuwepo kwa mawasiliano kwasababu unayapuuza.

Kwenye mahusiano kuna matatizo ya kuhisi kusalitiwa, matumizi ya pesa, kutokuridhika katika mapenzi, kudharauliwa, kutokushirikishwa katika maamuzi n.k. haya yote njia rahisi ya kuyamaliza ni [mawasiliano] kukaa chini na kuyazungumza na mwenzi wako na sio kuyaweka moyoni siku ukiudhika uyaseme kama malalamiko.

Mawasiliano yanapokuwepo baina ya wapenzi.... yaanasaidia kuaminiana, kuheshimiana, kusikilizana na kuvumiliana. Wewe dada mmeo/mwenza wako alipokukera ulimwambia kwa utaratibu baadae kuwa hubby ulinikera naomba tuyamalize? Au umeliweka moyoni siku akikukanyaga umkumbushie kwa kulia?

Wewe mwanamme mpenzi wako alipohisi unamcheat ulimkalisha chini mkayamaliza kila mmoja akabaki na amani pasipo na hisi hasi?

Tupende kuwasiliana katika mapenzi.... tutaboresha mahusiano yetu kwa ujenzi wa familia bora.

asalaaam.
Hili bandiko nimelipenda sana,nitalifanyia kazi aisee
 
Daby,
Kijana wangu , wote wana kuja maana, taarifa zilizopo wanadai kwa sasa wapo wanalinda kura huko Siha na Kinondoni.

Ila kwa bahati mbaya sana, kwenye vituo vingi viwavi wa kijani kibichi wameishafanya yao kwa msaada na ushauri wa kutoka kwa mkoa wa Mr. Slim.

Ila ni ujumbe mujarabu haswaaa.
 
Kuzungumza kwa kila tatzo au jambo kwenye uhusiano ni njia bora
Coz ipo tofaut ya kuongea na kuzungumza na weng hatuzungumz tunaongea tu
 
Daby,
Kijana wangu , wote wana kuja maana, taarifa zilizopo wanadai kwa sasa wapo wanalinda kura huko Siha na Kinondoni.

Ila kwa bahati mbaya sana, kwenye vituo vingi viwavi wa kijani kibichi wameishafanya yao kwa msaada na ushauri wa kutoka kwa mkoa wa Mr. Slim.

Ila ni ujumbe mujarabu haswaaa.

Kila kheri chifu watashindana ila hawatashinda.

Shukrani
 
Kuzungumza kwa kila tatzo au jambo kwenye uhusiano ni njia bora
Coz ipo tofaut ya kuongea na kuzungumza na weng hatuzungumz tunaongea tu
Bila shaka u mwalimu wa lugha.

Communicating.
Talking.
 
Back
Top Bottom