Maumivu yananitesa

Maumivu yananitesa

Ni mambo mengi, lakini kikubwa tunagombana kisa hataki tukapime afya, akikosea hataki nimrekebishe ila ikitokea kwa bahati mbaya nimekosea hata kidogo tu au msg nmemjibu tofauti basi anasema tuachane eti mimi sitaki kuwa chini yake.

Kingine yeye ni mwanaume lakini hataki sex hata nikimwambia ansema sio priority yake,nikimuliza kwa nia nzuri tu isije ukawa una tatzo. basi ndo amezira eti nmemtukana. Yaani mpaka naihi nae kwa kuogopa badala ya kufurahi.

_
pamoja na hayo yote nampenda sana naumia sana,

_Aaah, pole sana mwaya sasa nimefahamu. Kwa ushauri wangu sasa nakushauri utulie usiendelee kumtumia sms au kujaribu kumpigia simu. Najua inauma sana lkn mi ninaamini kuwa kama na yeye anakupenda hasira zikimwisha atakutafuta mwenyewe usijaribu ku force utazidi kumuudhi. Lkn pia hata siku moja unapomuona mwenzako hajisikii kufanya mapenzi jaribu kumbembeleza, kumfariji badala ya kumsimanga na kumwambia maneno ya kuzidi kumuumiza mfano ni hilo neno ulilomwambia eti ana tatizo ukweli sio zuri. ni kama kusema vile hawezi kukufanya jambo ambalo wanaume wengi hawapendi kulisikia. Poa basi, cool down endelea kufanya shughuli zako naamini kama umeshamuomba msamaha atakurudia tu.
 
_Aaah, pole sana mwaya sasa nimefahamu. Kwa ushauri wangu sasa nakushauri utulie usiendelee kumtumia sms au kujaribu kumpigia simu. Najua inauma sana lkn mi ninaamini kuwa kama na yeye anakupenda hasira zikimwisha atakutafuta mwenyewe usijaribu ku force utazidi kumuudhi. Lkn pia hata siku moja unapomuona mwenzako hajisikii kufanya mapenzi jaribu kumbembeleza, kumfariji badala ya kumsimanga na kumwambia maneno ya kuzidi kumuumiza mfano ni hilo neno ulilomwambia eti ana tatizo ukweli sio zuri. ni kama kusema vile hawezi kukufanya jambo ambalo wanaume wengi hawapendi kulisikia. Poa basi, cool down endelea kufanya shughuli zako naamini kama umeshamuomba msamaha atakurudia tu.

asante sana kwa ushauri, hata mimi najutia mno kuwambia hivyo, limemuumiza sna nami nimemwomba msamaha kwa dhati.
 
pole cn ant uyo atakua hana mapenz na wew fanya kumsahau asije kukuaribia malengo yko.
 
mimi nilipoachana na mtu niliumwa hadi kulazwa..........hapo mimi ndo nilimwacha, lakini kwa jinsi nilivyompenda niliugua

Well, kumbe pamoja na kunipiga kibuti kwa mbwembwe vile uliumwa mpaka ukalazwa?? 🙂

Za masiku tele Bibie?
 
Kwani yeye ndo mwanaume pekee duniani??

Huyo anakutafutia sababu za kukuacha,
Endelea na maisha yako
 
Kwanza jiulize akiwa ameathirika ungekubali akuoe hivyo hivyo? Kama anakutendea hivi hajakuoa ukiolewa utakuwa na amani? Sikia kumwacha mtu kumbuka mabaya zaidi aliyokutendea hutamtamani kamwe
 
Katika Elimu ya psychology inasema kwanza lazima uuthamini utu wako maumivu unayoyapata kumbuka yeye hayapati. Pia unapoteza muda kulia kumbuka yawezekana yeye anamwanamke mwingine na hata ukifa watakao kuwa wamepoteza ni wazazi wako Sio yeye by the way yeye ataoa mwingine.
Pia shida ya wanawake walio wengi kutokujithamini wenyewe obviously unajiona kama hutapendwa ukitathmini umri wako. Sikia LAKI you need to trust yourself Sio kutaka mwingine akuamini.
 
Well, kumbe pamoja na kunipiga kibuti kwa mbwembwe vile uliumwa mpaka ukalazwa?? 🙂

Za masiku tele Bibie?
ha haaa, chezeya mapenzi weye????????
ni bora hukujua enzi zile, ungenichekaje!
lakini si umeona imesaidia maana bado tu marafiki?
 
wagombanao hawapatani kwa simu. inabidi mkutane mkae muongelee ugomvi wenu. aksante
 
Ahhhiiiiìiiiii shemeji hata wewe? Usimwage mdogo wangu. Yarekebisheni hayo matofauti yenu kisha mtakaa kwa amani.
 
tatizo ni nini? kama amuna sababu ya msingi ya nyie kufanyiana hivyo ma dear just do other thing achana nae..... hivi kuchuniana inakuwaje sijawahi fanya huo mchezo aiseeeeeeee. mimi ningekuwa nimeshajichanganya na kuachana nae

umeachana na mimi?
 
Back
Top Bottom