Maumivu ya mapenzi ni zaidi ya msiba

Maumivu ya mapenzi ni zaidi ya msiba

Mimi mkuu nilikuwa nahudumia gharama zote hadi ndugu zake na mama yake na hata kumpeleka mdogo wake shule lakini kilichonikuta ni ngumu kuelezea nimepigwa chini,shemeji zangu nao hawataki hata kupokea simu zangu isipokuwa kuna kaka yake mmoja tu ndo tumekuwa tukiongea toka nipigwe chini.
Polee saana mkuu,,
 
Polee saana mkuu,,
Ahsante mkuu lakini hii mambo ni ya kawaida tu maana hawa wanawake hawa tunaoishi wanaona karibu tu wanachanganywa na vitu vidogo tu vya anasa na kusahau yote aliyofanyiwa na mtu wake wa awali.
 
Hebu niadisie ilikuwaje maana sijui kwa nini upende hivyo.......dunia ina watu bil 9.5....na zaidi.....ukipenda huyo mmoja kiasi hicho hao wengine watapendwa na nani......?......

Hahahaha haka kamsemo nakapendaaa yaan ukijua hivyo hata hautasumbuka sanaaaa
 
Mimi nililia sana tena sana kitandani hadi nkapitiwa usingizi ilinisaidia kupunguza uchungu na hasira nilozokuwanazo.....nilipoamka nikaoga vizuriii nikaupara mwenyewe nikajitoa out na rafiki angu kipenzi .... Baada ya hapo mmmh kama sio mimi nikawa busy sana na kanisani mpaka Leo nakwambia nashine tu .....
Hongera kwa kujua Mungu ndio kimbilio letu wanadamu
 
Kupenda saanaaa ni mateso tu! Kaa kimachale bro!
 
Pole sana ila kwa ninavyojua mijanaume ya siku izi ilivyo lazima huyo mwanamke atakumbuka tena sana
 
Back
Top Bottom