Maudhi ya mke, funguka

Maudhi ya mke, funguka

Kikubwa, kabla huaoa piga goti vya kutosha na ukishaoa piga goti pia vya kutosha ... heshima na adabu ya ndoa ni kitu cha pande mbili, kabla hujaheshimiwa na mke kukutii cha kwanza jiheshimu na uwe mtii, jinsi ulivyoandika mada yako kwanza inaonesha hujaoa and like MKE ni kitu tu umekileta nyumbani kwa ajili ya matumizi yako.

Kumbuka, unapopiga goti kwa ajili ya kumuomba MUNGU mke wa kufanana nawe, mke naye at the same time amekuwa akimuomba MUNGU mume wa kumfaa na kufanana naye so si lazima yeye tu ndo afuate tabia zako bali wewe pia unatakiwa ufuate tabia zake. Usisahau kanuni hii : Stranger+Rafiki+Uhusiano+Uchumba+Ndoa=Mke so kama huko kote ulipita mwisho wa siku ukaamua kujitwisha then hilo lako ... wanaume tupunguze kulalamika na tu deal na changamoto zetu za kwenye ndoa.

Mke ni binadamu kama binadamu wengine, tofauti ni jinsia tu, so kama wewe unakosea yeye pia anayo nafasi ya kufanya makosa tena kumbuka wao wana disadvantage in mood swing due to the monthly hormonal changes so weka room kwa ajili ya hiyo kitu. Kikubwa, kama couples msisahau kurekebishana kwa heshima na upendo na kusamehe, coz kwangu asiyesamehe ndiye anayepata hasara zaidi kuliko hata yule asiyesamehewa.

Aiseee!!! Safi sana, kama wewe ni mwanaume ubarikiwe kuliko wanaume wote duniani.

Ni kweli wanawake tunaongea sana lakini hatuongei hivihivi tunaongea tukichokozwa,ukikosa adabu jua mkeo ni mara mbili yako,ila wanaume ndo wenye maneno mabaya sana akiongea neno moja tu linaenda kuchoma mpka kwenye uvungu wa moyo.

BTW Matatizo au hayo maudhi hayafanani hata kidogo kila mtu ana changamoto zake na hayo maudhi yanayotokea ndo yanatukamilisha tukawa wakamilifu.

Halafu utajadilije tatizo wakati tatizo lenyewe halijakupata,mnaingia kwenye ndoa na defense mechanism nyiingi sanaa mguu nje mguu ndani cheche tu ilitokea ushakimbia mpaka unataka kuvunja miguu utafikir ni bomu limelipuka,mnayachokonoa matatizo wenyewe yakija mnapiga kelele wakat ni vitu mlivyovipanga wenyewe.
 
Wanaume wengi Tunakufa mapema Na mashinikizo ya damu kutokana na karaha za wanawake believe it or leave it
 
hahaaaaa leo kazi ipo.....ngoja nirudi kuleeeeeeee kwa miss chagga ndio kumenoga..
 
Mwanamke kabla hajaolewa,ni mkalimu kweli kweli.Ni kama kondakta wa daladala,wakati wa kupanda utabembelezwa sana.Sasa subiri muda wa kushuka.utasikia mara huniridhishi,Kibamia,najuta kuolewa na wewe.Mbwembwe zote za kparty,sendoff,zilifanywa na wewe wewe
 
1.sijui ilikuwaje hadi mimi kuolewa na wewe sikupendi hadi basi tu.
2. mwanaume gani wewe??kati ya wanaume nawe utasema ni mwanaume.pole sana
3.Mimi siyo mwanamke wa hadhi yako nenda katafute mwanamke wa type yako siyo mimi
hayo ni baadhi tu ya maneno ya kelo.. afu hapo anaongea yuko serious ..ukimwambia achaache hayo maneno anakaza tu na kuzidisha..
mimi naishia hapo
mmh! huyu anakuwa anatania au ni serious ? mbona kazi ipo kama ndio hivi
 
mmh! huyu anakuwa anatania au ni serious ? mbona kazi ipo kama ndio hivi

hataniwi mtu hapo..na ukicheche ukimwita mke wangu anakujibu mbele za watu nani mke wako hapa???
 
hataniwi mtu hapo..na ukicheche ukimwita mke wangu anakujibu mbele za watu nani mke wako hapa???

Pole mkuu mwambie Mungu ashughulike na ndoa yako maana huyo ndiye mwanamke aliyetoka ubavuni mwako mwambie Mungu amshughulikie amrekebishe na wewe urekebishwe ili yeye afit kwenye ubavu wako
 
Pole mkuu mwambie Mungu ashughulike na ndoa yako maana huyo ndiye mwanamke aliyetoka ubavuni mwako mwambie Mungu amshughulikie amrekebishe na wewe urekebishwe ili yeye afit kwenye ubavu wako

haya ni majanga ya wengi mkuu..ila sometime to forget is the best revenge
 
Maudhi ya Mke yanaenda sambamba na maudhi ya Mume , Haiwezekani Mwanaume wewe
1- Ukiwekewa chakula hapo unakulaaa mpaka unaramba sahani , halafu hata Ahsante Mke wangu kwa chakula hakunaa
2- Haiwezekani nakutayarishia Nguo ya kuvaa badala yake unaacha unakwenda kuvaa Mtisheti na Msuruali wa rangi moja kama bachela !
3-Haiwezekani nakukaribisha kwa tabasamu na kukupa pole na kazi ingawa hata mimi nimetoka kazini halafu unausugua tu hata kujibu hujibu !
4- Haiwezekani nikuombe hela la saloon kwa deko kama mume wangu halafu uniambie Mshahara wako unafanya nini? ohooo unnecessary

Utategemea sisi tutaendelea kunyenyekea tu ! No way Baby ....:sorry:
 
Utakuta msichana mrembo kipindi mnaanza ....mkishaingia kuishi nyumba moja, .......ule usafi wote unatoweka ghafla......na kero zingine zinazo sababishwa na mazoea.......ukiulizwa utaambiwa ....."Bwana eeeeeh kama umenichoka tupotezeane tuachane kwani lazima kuishi pamoja?!"...........Halafu hapo mtu ndio unataka kuweka kambi unataka kuachana na kuhangaika na vicheche!Dah mademu wa siku hizi kusema ukweli ni vilaza kwenye kumanage ndoa zao.......i hope soon serikali watatoa diploma na degree ya wife material ili hawa waliopitwa na unyago waliokuwa wanapata mabibi zetu wakaelimike warudi kwenye mstari familia ziimarike.

mlianza wenyewe kusupot utandawaz ooo wa zaman niwashamba hawako uptodate,unyago mbaya wanakatwa ule utamu,wenyewe mnakumbuka unyago hatari. FGM ilikuwa inapractiziwa but walifundishwa kazi kwelikwel akikuibia mune harudi japo hujakatwa uko airtel tangu mwanzo
 
1.sijui ilikuwaje hadi mimi kuolewa na wewe sikupendi hadi basi tu.
2. mwanaume gani wewe??kati ya wanaume nawe utasema ni mwanaume.pole sana
3.Mimi siyo mwanamke wa hadhi yako nenda katafute mwanamke wa type yako siyo mimi
hayo ni baadhi tu ya maneno ya kelo.. afu hapo anaongea yuko serious ..ukimwambia achaache hayo maneno anakaza tu na kuzidisha..
mimi naishia hapo

mwanamke mpk aseme hvyo mkuu kipo ulichomfanya ina mana anakurupuka tu na kusema ayoo??
 
Back
Top Bottom