Mauaji ya watu 3 Ilala - Dar

Mauaji ya watu 3 Ilala - Dar

fimbombaya

Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
47
Reaction score
12
Nimepita hapa maeneo ya ilala karibu na club ya wazee, kuna mauaji yametokea kwa watu wawili kupigwa risasi na muuaji nae kajiua,pia wawil wamejeruhiwa. Taarifa zaid ntawajuza.


Kwa mujibu wa shuhuda wa Clouds FM.

Mauaji hayo yamefanyika maeneo ya Ilala, kataja maeneo kwa jina lake maarufu (bahati mbaya sikudaka vizuri). Inadaiwa kuna gari ilikua inatoka ndani ya geti kutoka ikiwa na dereva mwanaume, abiria mwanamke mbele, na abiria wengine wawili wakiwa seat ya nyuma.

Pembeni hapo kulikua na jamaa kasimama. Inadaiwa alishushwa hapo dakika chache toka katika tax, walipotokeza abiria hao kupitia gari yao alitoa silaha yake na kupiga risasi gari akilenga zaidi abiria wa mbele pande zote kisha na nyuma. Baada ya kumaliza hapo muuaji huyo naye alijipiga risasi na kufariki hapo hapo.

Dereva na abiria wake wa mbele wamefariki dunia, huku abiria wa nyuma mmoja mama mtu mzima kajeruhiwa na risasi mgongoni na dada mwingine kujeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni.

--------------------------------
Ni maeneo ya Club ya wazee!! ilala Amana. kuna jamaa kapiga watu wawili risasi kwenye gari na kuwauwa hapo hapo na kujeruhi wengine wawili na kisha kujimaliza yeye mwenyewe. hii habari ni kwa mujibu wa breaking news ya mawingu FM.

hii imetokea saa moja na nusu hivi kutoka sasa ni maeneo ya ilala Boma, lilikuwa gari dogo ambalo lilismama ili kusubiri kufungiuliwa geti kisha ikaja pick up akashuka mkaka akamfyatua risasi ya ubongo dereva, wa hiyo gari ndogo kisha akamfyatua mwanamama alokuwa kushoto kisha akawa pasi abiria wawili walokuwa wamekaa kiti cha nyuma.

kisha ajifyatua yeyey mwenyewe toka kidevuni hadi utosini.

sikutaka kushuhudia zaid manake nisije nikajikuta napatapao ya shavu nikasepa mdogo mdogo.



Ilala4.jpg





Ilala1.jpg





Ilala2.jpg



ilala3.jpg


Mapema leo asubuhi milio ya risasi zaidi ya kumi ilisikika eneo la Ilala Bungoni karibu na baa maarufu ya Wazee (Club ya Wazee), watu watatu wakiripotiwa kufariki kutokana na tukio hilo linaloelezwa kuwa limetokana na wivu wa kimapenzi.


Dereva mmoja wa tax kituo cha Bungoni ambaye alikuwa shuhuda wa kwanza, alisema mapema leo asubuhi alipata mteja aliyehitaji kupelekwa sehemu, ila kabla hawajafika huko walipokuwa wanataka kwenda jamaa ambaye ndiye alikuwa ni muuwaji alimuomba akatishe safari na kumtaka ampeleke sehemu nyingine.

Kwa mujibu wake dereva huyo aliendelea kusimulia, alimpeleka jamaa mpaka aneo la tukio hilo kwenye nyumba iliyopo pembeni mwa Hotel mpya iitwayo MM.

Mara baada ya kufika hapo, jamaa alitoa sh. 5,000 na kumkabidhi dereva ila cha kushangaza ni kitendo cha jamaa huyo kutoa bastola wakati akiwa anaelekea kwenye geti la nyumba, aliendelea kusimulia dereva huyo.

Wakati jamaa anaelekea getini mlango ulifunguliwa na gari aina ya Toyota Surf ilitoka ikiwa na watu wanne ndani, mwanaume mmoja ambaye ndiye aliyekuwa akiendesha gari mama mmoja na wadada wawili.

Jamaa akiwa na bastola alianza kuwashambulia watu waliokuwa ndani ya gari hilo na kumpiga risasi dereva na mdada mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Carol, hii ni kwa mujibu wa dereva huyo na mara baada ya kuona hivyo hivyo ikabidi akimbie.

Vyanzo vingine vinaeleza kuwa katika tukio hilo jamaa pia limpiga risasi ya mgongoni mama wa mwanamke aliyemuua na pia alimpiga msichana mwingine risasi ya mguu.

Mtuhumiwa na dereva aliyekuwa akiendesha gari walifariki palepale huku msichana mmoja akielezwa kufariki akiwa njiani kuelekea hospitali.

Bado haijafahamika moja kwa moja chanzo cha mauwaji hayo licha ya watu wengi ambao nilipata bahati ya kuongea nao wakilihusisha tukio hilo na mambo ya kimapenzi.
 
Ndo nasikiliza clouds wameiongelea hiyo kwakweli ni jambo ambayo limesikitisha sana
 
Mimi nimepita hapo muda si mrefu risasi zilipolia watu walifikiri ni majambazi na walijaribu kufuatilia ili kuwadhibiti, watu walikuwa wengi sana kila upande kuzunguka eneo la tukio. Hapakuwa na askari polisi na hata wale wa usalama barabarani wanaokuwa pale Bungoni hawakuonekana.
 
Mbona habari zinadai kwamba mtu kamuua dada yake na shemeji yake...daaaah hii dunia bhana ni noma ..RIP waliokufa.
 
Hivi hizi silaha watu wanaazimana au zinatolewa kwa kufuata taratibu?
Wapumzike kwa amani marehemu na hao majeruhi wapate nafuu ya haraka
 
Nimepita, ngoja nikapate updates za Kapuya.
 
Mfanyabiashara wa magari wa mwanza amemuua dada wa mchumba wake na yeye kujimaliza,kisa wivu wa mapenzi na kumjeruhi mchumbake,na mtu mwingine,. Source radio wapo na Masau bwire.
 
NI MAUAJI YA KUTISHA SANA YALITOKEA ILALA,NJE YA "M"HOTEL,JAMAA ALIKUJA SOFTLY HUKU AKINYWA SUPU KAMA HAKUNA ANALOTAKA KUFANYA! KWELI KILLER HAS NO CLEAR FACE,R I P alls
 
Watu wengine hamnazo unajiua kisa mapenzi!

Ni maeneo ya Club ya wazee!! ilala Amana. kuna jamaa kapiga watu wawili risasi kwenye gari na kuwauwa hapo hapo na kujeruhi wengine wawili na kisha kujimaliza yeye mwenyewe. hii habari ni kwa mujibu wa breaking news ya mawingu FM.
 
itv wametangaza pia.
turudi kwenye issue ya kapuya ndio habari ya mujini kwa sasa
 
Back
Top Bottom